Maoni kuhusu suala la wagonjwa walioshindwa kulipa gharama za matibabu hospitali ya Muhimbili

Maoni kuhusu suala la wagonjwa walioshindwa kulipa gharama za matibabu hospitali ya Muhimbili

Mparee2

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2012
Posts
3,092
Reaction score
5,386
Kutokana na malalamiko ya mara kwa mara ya watu kuhusu wagonjwa kuzuiliwa Muhimbili hata miezi mitatu na kuendelea sababu ya kushindwa kulipa deni.

Nashauri Waziri wa Afya atume watu (tume huru) wakapate ukweli kwa kupata taarifa ya Hospitali lakini pia kuongea na waathirika ili wapate ukweli; lakini muhimu zaidi ni kujua ukubwa wa tatizo Mfano; ningependekeza wapate Report ya kuanzia Jan 2022 hadi Nov 2023

Mfano;
1. Ni jumla ya watu wangapi wamezuiliwa (kwa mwezi) kwa kushindwa kulipa deni (wanaume/wanawake/watoto na kwa muda gani) na deni wanalo daiwa kwa makundi.

2. Ni maiti ngapi zinazuiliwa kwa kila mwezi; (kwa muda gani)

3. Ni wamama wangapi wenye watoto chini ya miaka mitano waliozuiliwa pale hadi leo (kwa muda gani)

4. Wana vigezo gani wanatumia kuzuia wagonjwa/Maiti na wamepata hayo mamlaka ya kuzuia kwa muda gani?

Nafikiri ipo haja pia ya kufanya hili zoezi hata kwa hospitali za Rufaa ili kuona ukubwa wa tatizo lakini pia itasaidia kujua jinsi maamuzi yanavyofanya huku chini
Taarifa zikiwa wazi Taasisis za dini na hata mashirika yanaweza kushiriki kuwanasua wenzetu
Inaumiza sana kusikia mtu amefiwa na mkewe/mumewe/mtoto halafu amezuiliwa asiende kumzika kwa kuwa hana uwezo wa kulipa deni hospitali😭 ?

Natamani hata hizi hela ndogo ndogo (5m/10m/20m nk) ikiwezekana zielekezwe huko kuwanasua wenzetu....
 
Habari wana jamvi,

Mimi na ndugu zangu ni wahanga wa hili jambo. Kuna ndugu yetu amefariki Muhimbili siku 3 zilizopita katika matibabu yake tunadaiwa milioni mbili.

Kama familia, tumejichanga lakini hyo hela haijatimia. Wamezuia mwili mpaka ilipwe.

Nauliza serikali, kwanini isiweke mfuko maalum wa kusaidia wagonjwa wasiojiweza kuwalipia gharama zao pindi wanapokufa?
 
Back
Top Bottom