Maoni ya Augustine Mrema kuhusu uzoefu wa Demokrasia ya Kenya

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
January 6 2019
Mzee Augustino Lyatonga Mrema anazungumzia mapungufu ya mfumo wa demokrasia. Anasema demokrasia ni kama mchezo wa kuigiza usioleta manufaa kwa nchi yeyote.

Anatoa mfano wa demokrasia ktk siasa za Kenya unaosifiwa ktk Afrika, lakini Mzee Augustino Mrema anabainisha mapungufu makubwa kuhusu mfumo huo wa demokrasia.

Demokrasia anayoiona Mzee Mrema ktk bara la Afrika ni kwa ajili ya uroho wa madaraka. Uchaguzi Kenya Raila Odinga alishindwa akakimbilia mahakamani. Mzee Mrema akakumbusha mahakama ikafuta ushindi wa Uhuru Kenyatta. Uchaguzi ukarudiwa lakini Mzee Mrema anasema ingawa Raila Odinga alishindwa tena ktk Uchaguzi wa marudio, Raila hakukubali matokeo ya pili pia.

Hapo Mzee Mrema ndipo anajiuliza nini faida ya demokrasia ikiwa kina Raila wanataka ushindi tu ndiyo wanaona demokrasia ipo.

Ampongeza Uhuru Kenyatta kutumia busara hata baada ya Raila kuapishwa kama 'rais wa watu', Kenyatta kama Rais wa Jamhuri ya Kenya akaamua kumwalika Raila Odinga washikane mkono maana Uhuru Kenyatta angetumia kiburi cha demokrasia nchi ingewaka moto.


Source : millard ayo
Mzee Augustino Mrema aliyasema hayo wakati akizungumzia kupinga hatua ya vyama vya siasa kuunga mkono raia kufungua kesi kupinga muswada mpya wa vyama vya siasa Tanzania
Kesi ya Kikatiba kuhusu kupinga muswada wa vyama vya Siasa ...
https://www.jamiiforums.com › threads


2 days ago · Kesi ya Kikatiba namba 31/2018, kuhusu mswada wa vyama vya Siasa iliyofunguliwa na Vyama
 
mzee lyatonga aendelee kula pension au tumgeuzie kikotoo,?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…