Boss la DP World
JF-Expert Member
- Dec 12, 2021
- 2,318
- 8,464
Ndugu zangu wanasimba wenzangu kwanza niwape pole kwa kuendelea kupoteza mwelekeo kwenye ligi na kuzidi kupishana na mpinzani wetu Yanga.
Kuna mambo kadha wa kadha nataka kuyaweka sawa ambayo tumeanza kupotoshwa na baadhi ya viongozi wa club...
1. Wameanza kusikika wakisema kombe la NBCPL halina mashiko, ndugu zangu wanasimba tusiwe wajinga kiasi hiki, kombe la ligi kuu lina maana kubwa sana na hadhi kubwa, msimu huu ilipaswa tulichukue mara ya 5 mfululizo, uzembe na ubishi wa baadhi ya viongozi wetu ndiyo umetufikisha hapa tulipo sasa.
2. Ahmed Ally asiingie kichwa kichwa na kutupa matumaini hewa eti bado tuna nafasi ya kutwaa ubingwa, hizo ni ndoto za mchana na kutufanya sisi ni watoto wadogo, anapaswa kuheshimu mashabiki maana bila sisi hata kibarua chake kitaota nyasi, wakati mwingine ni bora angechagua kukaa kimya kuliko kutupa matumaini hewa, ni Ahmed Ally ndiye alituhakikishia kuwa mechi ya jana tutashinda, baadhi ya mashabiki tumejikamua, tumesafiri mpaka Mwanza matokeo yake tumepata tulicho kipata.
Baada ya mchezo wa jana anaendelea kutuaminisha tuwe na subira tutashinda tarehe 28, namimi namuuliza kwa kikosi kipi na kocha yupi? Kwanini wanatuumiza hivi au nayeye anatumwa na Yanga? Maana akisimama mbele ya camera anaongea anacheka cheka utadhani tunaongoza ligi.
3. Pablo Franco sio kocha mwenye kiwango kinachotosha kuifundisha club yetu. Hapa tulipigwa pakubwa sana.
4. Mashabiki tunaumizwa sana na mwenendo wa timu, sisi sio wa kuitwa MAKOLO na watani, hili jina linakera ni lazima tuangalie cha kufanya vinginevyo mnatuumiza, tunalipia uana chama, tunasafiri Kwa pesa, tunalala hotel za gharama, tunakula chakula kwa gharama mwisho tunapata matokeo ya kijinga kabisa.
Viongozi wa SIMBA kama mmeshindwa tuachieni timu yetu, nimenusa aibu kubwa mbele yetu, msifanye tuamue kuamini maneno ya Haji Manara.
PABLO FRANCO SIO KOCHA, TAFUTENI KOCHA MCHUKUENI HATA JULIO JAMANIIII
Aaagh.
Kuna mambo kadha wa kadha nataka kuyaweka sawa ambayo tumeanza kupotoshwa na baadhi ya viongozi wa club...
1. Wameanza kusikika wakisema kombe la NBCPL halina mashiko, ndugu zangu wanasimba tusiwe wajinga kiasi hiki, kombe la ligi kuu lina maana kubwa sana na hadhi kubwa, msimu huu ilipaswa tulichukue mara ya 5 mfululizo, uzembe na ubishi wa baadhi ya viongozi wetu ndiyo umetufikisha hapa tulipo sasa.
2. Ahmed Ally asiingie kichwa kichwa na kutupa matumaini hewa eti bado tuna nafasi ya kutwaa ubingwa, hizo ni ndoto za mchana na kutufanya sisi ni watoto wadogo, anapaswa kuheshimu mashabiki maana bila sisi hata kibarua chake kitaota nyasi, wakati mwingine ni bora angechagua kukaa kimya kuliko kutupa matumaini hewa, ni Ahmed Ally ndiye alituhakikishia kuwa mechi ya jana tutashinda, baadhi ya mashabiki tumejikamua, tumesafiri mpaka Mwanza matokeo yake tumepata tulicho kipata.
Baada ya mchezo wa jana anaendelea kutuaminisha tuwe na subira tutashinda tarehe 28, namimi namuuliza kwa kikosi kipi na kocha yupi? Kwanini wanatuumiza hivi au nayeye anatumwa na Yanga? Maana akisimama mbele ya camera anaongea anacheka cheka utadhani tunaongoza ligi.
3. Pablo Franco sio kocha mwenye kiwango kinachotosha kuifundisha club yetu. Hapa tulipigwa pakubwa sana.
4. Mashabiki tunaumizwa sana na mwenendo wa timu, sisi sio wa kuitwa MAKOLO na watani, hili jina linakera ni lazima tuangalie cha kufanya vinginevyo mnatuumiza, tunalipia uana chama, tunasafiri Kwa pesa, tunalala hotel za gharama, tunakula chakula kwa gharama mwisho tunapata matokeo ya kijinga kabisa.
Viongozi wa SIMBA kama mmeshindwa tuachieni timu yetu, nimenusa aibu kubwa mbele yetu, msifanye tuamue kuamini maneno ya Haji Manara.
PABLO FRANCO SIO KOCHA, TAFUTENI KOCHA MCHUKUENI HATA JULIO JAMANIIII
Aaagh.