Maoni yangu kuhusu shughuli za uokoaji huko mkoani Kagera

Maoni yangu kuhusu shughuli za uokoaji huko mkoani Kagera

Linguistic

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2021
Posts
3,669
Reaction score
8,268
Wakuu haya Maoni yangu kuhusu shughuli za uokoaji.

1. Kwa hali ilivyo sasa hivi utegemezi wa Jeshi la Zimamoto pekee hautoshi kwenye majanga yanayohusisha ndege.

Inashauriwa tuwe na mfumo wa pamoja wa uokoaji (Integrated rescue operation system) utakaokuwa na Kikosi Maalum cha Uokoaji kikihusisha wataaam kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Jeshi la Zimamoto, Jeshi la Maji, Afya kwa ajili ya matibabu ya dharula na huduma ya kwanza na sekta nyungine kadri itakavyoonrksna inafaa.

2. Vikosii hivi maalum vya uokoaji viwepo maeneo yote nchini ngazi ya mikoa hususani kwenye maeneo ya nchi yenye viwanja vya ndege vilivyo karibu na mito mikubwa, maxima na bahari.

3. Vikosi hivyo maalum viwe na wataalam sahihi na wabobezi katika uokoaji na vifaa sahihi na vya msingi katika shughuli za uokoaji kwa ajili ya nchi kavu na majini.

Timu za Uokoaji zinatakiwa kuwa zimeiva kimafunzo na kufanya drills za mara kwa mara.

Pia utaalam wa wenyeji hasa wavuvi ambao wanajua mazingira ya majini kwa kuwa ndio eneo lao la kazi kila siku na wamekuwa na msaada mkubwa kwenye uokoaji unapaswa kuangaliwa upya na kuona unavyoweza kusaidia shughuli za uokoaji.

Kiufupi tunatakiwa kufanya uwekezaji wa kutosha kwenye suala la udhibiti majanga.

4. Utayari wa Vikosi vya Uokoaji kila wakati ni jambo muhimu sana ikizingatiwa kuwa kwa asili ya majanga ya ndege muda huamua mambo mengi ili kuepuka kulipuka kwa ndege, ukosefu wa hewa ya oksijeni ndani ya ndege, maji kuingia kwenye ndege kama imetua majini, n.k.

Utayari wa vikosi unatakiwa uwe wa hali ya juu na wa kila wakati.

5. Uratibu wa majanga unapaswa kuboreshwa ili taarifa sahihi ifike kwa wahusika sahihi kwa wakati muafaka haraka kadri iwezekanavyo.

Kwenye majanga karibu yote yaliyotokea ikiwemo hili la jana kuna "time lag" kubwa kutoka janga linapotokea au inapoonekana kuna mwelekeo wa kutokea janga na wahusika kupewa taarifa ili shughuli za uokoaji kuanza.

Majanga yatatokea ni wajibu wetu kujenga mfumo imara wa kudhibiti athari zake pindi yanapotokea ili tuokoe maisha ya watu wetu kwa kadri inavyowezekana.

Tutimize wajibu wetu, inawezekana.

Kiranga Mshana Jr Retired
 
Pia utaalam wa wenyeji hasa wavuvi ambao wanajua mazingira ya majini kwa kuwa ndio eneo lao la kazi kila siku na wamekuwa na msaada mkubwa kwenye uokoaji unapaswa kuangaliwa upya na kuona unavyoweza kusaidia shughuli za uokoaji.
Umeonga vema kabisa hapa. Hawa wavuvi wapewe training, periodic ones kuhusu uokoji kutumia zana zao za mitumbwi, makasia etc (kama serikali ina habari na utumiaji wa "primitive" zana za wavuvi, mana wa kwetu wanatia mashaka). Ikitokea kama hii wanakuwa na "big idea" waanzie wapi. Wanajua kina kifupi kiko wapi na kirefu kiko wapi, wanafanyaje wanapopatwa na misukasuko katika vina hivyo... can that be applied to the planer scenario?
 
Wakuu haya Maoni yangu kuhusu shughuli za uokoaji.

1. Kwa hali ilivyo sasa hivi utegemezi wa Jeshi la Zimamoto pekee hautoshi kwenye majanga yanayohusisha ndege.

Inashauriwa tuwe na mfumo wa pamoja wa uokoaji (Integrated rescue operation system) utakaokuwa na Kikosi Maalum cha Uokoaji kikihusisha wataaam kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Jeshi la Zimamoto, Jeshi la Maji, Afya kwa ajili ya matibabu ya dharula na huduma ya kwanza na sekta nyungine kadri itakavyoonrksna inafaa.

2. Vikosii hivi maalum vya uokoaji viwepo maeneo yote nchini ngazi ya mikoa hususani kwenye maeneo ya nchi yenye viwanja vya ndege vilivyo karibu na mito mikubwa, maxima na bahari.

3. Vikosi hivyo maalum viwe na wataalam sahihi na wabobezi katika uokoaji na vifaa sahihi na vya msingi katika shughuli za uokoaji kwa ajili ya nchi kavu na majini.

Timu za Uokoaji zinatakiwa kuwa zimeiva kimafunzo na kufanya drills za mara kwa mara.

Pia utaalam wa wenyeji hasa wavuvi ambao wanajua mazingira ya majini kwa kuwa ndio eneo lao la kazi kila siku na wamekuwa na msaada mkubwa kwenye uokoaji unapaswa kuangaliwa upya na kuona unavyoweza kusaidia shughuli za uokoaji.

Kiufupi tunatakiwa kufanya uwekezaji wa kutosha kwenye suala la udhibiti majanga.

4. Utayari wa Vikosi vya Uokoaji kila wakati ni jambo muhimu sana ikizingatiwa kuwa kwa asili ya majanga ya ndege muda huamua mambo mengi ili kuepuka kulipuka kwa ndege, ukosefu wa hewa ya oksijeni ndani ya ndege, maji kuingia kwenye ndege kama imetua majini, n.k.

Utayari wa vikosi unatakiwa uwe wa hali ya juu na wa kila wakati.

5. Uratibu wa majanga unapaswa kuboreshwa ili taarifa sahihi ifike kwa wahusika sahihi kwa wakati muafaka haraka kadri iwezekanavyo.

Kwenye majanga karibu yote yaliyotokea ikiwemo hili la jana kuna "time lag" kubwa kutoka janga linapotokea au inapoonekana kuna mwelekeo wa kutokea janga na wahusika kupewa taarifa ili shughuli za uokoaji kuanza.

Majanga yatatokea ni wajibu wetu kujenga mfumo imara wa kudhibiti athari zake pindi yanapotokea ili tuokoe maisha ya watu wetu kwa kadri inavyowezekana.

Tutimize wajibu wetu, inawezekana.

Kiranga Mshana Jr Retired
Kila kitu ulichoandika hapa kipo kwenye makabrasha ya mamlaka.. Kuna a complete paper work ya yote hayo.. Kinachotuumiza sisi ni utashi na maamuzi ya kisiasa
Tumeipa siasa thamani kubwa kuliko taaluma, hapo ni wazi weledi kwenye utendaji wowote utakuwa chini ya kiwango, maana maamuzi mengi yanafanywa kisiasa hata kwenye teuzi za nafasi nyeti na muhimu sana taaluma haizingatiwi sana bali kinachoangaliwa ni mitazamo ya kisiasa
 
Umeonga vema kabisa hapa. Hawa wavuvi wapewe training, periodic ones kuhusu uokoji kutumia zana zao za mitumbwi, makasia etc (kama serikali ina habari na utumiaji wa "primitive" zana za wavuvi, mana wa kwetu wanatia mashaka). Ikitokea kama hii wanakuwa na "big idea" waanzie wapi. Wanajua kina kifupi kiko wapi na kirefu kiko wapi, wanafanyaje wanapopatwa na misukasuko katika vina hivyo... can that be applied to the planer scenario?
Sasa leo hii Yule kijana aliyeibuka shujaa badala ya kumuacha eneo hilo na kumpa mtaji wanaenda kumficha jeshi la zimamoto

Huyu kijana ni Mjasriamali.Kwa nini mnataka awe Mwanajeshi ?Kama ni mtoto wa RC au Waziri hivi ndivyo mngefanya ? Mpeni heshima na mtaji wa kukuza kazi zake.Heshima itunze ndoto yake.Naona kama mna mpeleka speed sana shujaa wetu. Atakuja sema Yes kwa vitu alivyo takiwa kusema No
 
Back
Top Bottom