Maoni Yangu Kwa Msanii Roma na Hoja Yake Ya Album

Maoni Yangu Kwa Msanii Roma na Hoja Yake Ya Album

Linguistic

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2021
Posts
3,669
Reaction score
8,268
Kuna hili analosema Roma kuhusu albam kutouza, Je Mmeona na kusoma maoni yake Wakuu?
.
Mimi nikiwa km mdau wa music way back niseme Tu Sababu anazotoa Roma ndio maana siku hizi wasanii wanatoa Mixtapes then wanaita ni Album.
.
Sababu focus yao ni waende Mainstream na sio kutoa Album as Album tena Well Structured Album.

Naheshimu mawazo yake, Lakini sikubaliani na mtazamo anaojaribu kuleta.
.
Kwanza Ki Bongo Bongo ndio tunarudi kwenye mfumo wa Album ambao hapo nyuma ulipotea, Lakini tunavyorudi tumekutana na vitu kadhaa kubadilika.

Kwa sasa Wasanii wamekua wengi mnoo.Ngoma kila siku zinatoka.
.
Zamani enzi za Akina Sele⁩ Insp.Harun⁩, prof. J, Ngwear, Mchizi Mox nk nk tulikua tunasubiri ngoma mpya Jumamosi Clouds Fm, sahizi nani anafanya hivyo? Maisha yanakimbia na teknolojia imebadilisha vitu vingi.
.
Hiyo ni mojawapo ya sababu kuu ukifanya Album inakua ngumu kwa kila singo kwenda mjini unless uziwekee stori juu yake.
.
Mfano Mondi X Zuchu ngoma yao hata ingekua mbovu vipi lazima ingeenda mjini.
.
Album ya Barnaba Fasta Fasta ngoma ambayo imeenda mjini ni aliyofanya na Mondi, Japo nyingi ni kali ila stori nyuma yake.
.
So Barnaba hajawahi kutoa ngoma na Mondi (Kama amewahi nikumbushwe).
.
So basically ni kitu watu walikua na hamu ya kuona kinatokea, ni kama siku itokee kolabo ya Fid Q na Joh Makini au Nikki Mbishi na Roma mwenyewe [emoji16] Kwenye Album zao hizo lazima zitaenda mjini.
.
Hata kwa wenzetu mfano Jay Z kuwepo tu kwenye ngoma yako lazima iende mjini Wa Kwetu
.
Why? Simply Jamaa hafanyi sana kolabo halafu kumpata ni shida yaani kiufupi process nzima ya kumpata ni stori mtaani.
.
So ukifanya nae ngoma hata iwe mbaya lazima itaenda hata kama kuna ngoma nyingine kali zimo kwenye Album.

Zamani ilikua rahisi Album nzima ku trend kwa sababu wasanii walikua wachache alafu means za distribution zilikua limited, so mzigo ukitoka ni lazima upigishwe wote.
.
Kama zamani nilikua na uwezo wa kujifungia naanza kula Package za Albums,Yaani kama unatazama Movie hivi [emoji3]
.
Mwisho, Album zina umuhimu mkubwa tu (Sio lazima kila ngoma iende mjini, What matters ni Album kali),
.
[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
FB_IMG_1663218462442.jpg
 
Album hazilipi
Namkumbuka, stereo na album ya afrikan son

Sijui dizasta na verseteller kama imemlipa au katoa sadaka

"Mziki umeingia stress, kila nyumba ina msanii"
Roma
 
Album hazilipi
Namkumbuka, stereo na album ya afrikan son

Sijui dizasta na verseteller kama imemlipa au katoa sadaka

"Mziki umeingia stress, kila nyumba ina msanii"
Roma
Nadhani Wengi tunashindwa kuelewa Maana ya album.

Album sio mkusanyiko wa nyimbo zako Zote. Album ni themes wazee
 
Back
Top Bottom