Maoni yangu: Kwanini wafanyakazi hawajaboreshewa maslahi yao awamu hii

Maoni yangu: Kwanini wafanyakazi hawajaboreshewa maslahi yao awamu hii

Mlalamikaji daily

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2014
Posts
744
Reaction score
1,621
Haya ni maoni yangu binafsi baada ya kutafakari kwa kina, kwanza siamini kwamba suala hili la kukaa miaka 7 bila kupandishwa madaraja na miaka 6 bila nyongeza ya kila mwaka kuwa ni suala la bahati mbaya! HAPANA! Upo msemo kuwa in politics nothing happen by accident!

Sasa twende sawa hapa, kama tujuavyo kamwe! kamwe! huwezi kumtawala mtu na kumfanya afanye unavyotaka huku akiwa ameshiba! Hivyo ukitaka mtu akunyenyekee, mnyime chakula, mnyime maji, halafu mletee chakula kidogo kidogo na maji kidogo kisha muahidi utamboreshea chakula chake wakati ujao! Hakika ataendelea kukutii na kukuheshimu kwa sababu mbili:

1. Kwanza atataka kulinda chakula chake hiki kidogo anachopata ili asife
2. Ataendelea kufanya kazi akiamini kuwa ipo siku ataboreshewa chakula chake

Nasikia eti wakati wa JK wafanyakazi walikuwa jeuri sana! Ndio maana haya yanawakuta.
Kwasasa hata kunyanyua shingo wengine hawawezi na wanafanya chochote kile ambacho BOSS atasema ili kulinda vibarua vyao.

Waliokwenda kusimamia uchaguzi kule Zimbabwe waliambiwa kuwa fanya ufanyavyo MWENYEWE ASHINDE, ole wako asishinde hivyo vyeti vyako utaenda kufungia mandazi.

Wewe unadhani wangefanyaje?

Kwa njaa hii wafanyakazi wanaweza kujikuta wanafanya chochote waambiwacho ili kulinda ugali huu mdogo.
 
Kwa jinsi gharama za maisha zilivyopanda, ni uonevu wa hali ya juu kuwanyima watumishi madaraja na nyongeza za mishahara.

Ufanisi wa kazi ni wa hali ya chini, na manung'uniko kila kona. Pia mtaani magenge mengi wanafunga kwa kukosa wateja.
 
Alisikika kiongoz mmoja wa serikali kuwa hawata tangaza kuongezwa kwa posho kwa watumishi wake ila jambo hilo litafanywa kimya kimya katika taasisi husika.
 
Ingekuwa ni kweli basi kuna watu wasingekuwa wanamtukuza mtukufu kabisa, maana sio kwamba wanalipwa ila wanamiminiwa.
 
Kila siku mada ni ileile, kwanini modes msiunganishe mada kama hizi na za wakati wa nyuma walau ikabakia kwenye thread moja?
 
Kwa taarifa yako wafanyakazi ni kundi la watu wenye akili na maarifa tele. Siyo watu wa kumtukuza mtu asiye na faida kwao.

Ukitaka mfanyakazi kokote duniani amkubali mwajiri wake, basi ni kwa mwajiri wake huyo tu kumtimizia huyo mfanyakazi mahitaji yake muhimu. Mfano kumlipa mshahara mnono, kumjali, kumheshimu, kumpa motisha, nk.

Kinyume na hapo, mwajiri utadharaulika tu na kuchukiwa na huyo mfanyakazi! Na ni jambo la kawaida sana kwa mwajiri kuhujumiwa muda wowote ule iwapo huyo mfanyakazi atapata nafasi ya kufanya hivyo kutokana na dhuluma unazo mtendea!!

All in all, tunamshukuru sana kwa kutufanya tuwe sugu.Enzi za JK tulibweteka sana. Tulitumia nguvu na muda wetu mwingi kazini. Wengi hatukuwa na akili ya kujiongeza! Maana kila baada ya miaka 3, daraja lilipanda. Kwa sasa wengi tunamiliki ofisi baada ya kuona mambo yanaenda ndivyo sivyo! Hivyo maisha yanaendelea. Ila kamwe hatutaacha kupigania haki zetu!
 
kila siku mada ni ileile, kwanini modes msiunganishe mada kama hizi na za wakati wa nyuma walau ikabakia kwenye thread moja?
Mbona unateseka sana! Umelazimishwa kufungua na kuisoma hii mada? Kiherehere tu kimekujaa. Hili ni jukwaa huru. Waache watu watoe maoni yao.

Wewe kama mada haikuhusu, pita kushoto. Nenda kwenye jukwaa lako la mavazi na mitindo! Hutaona ukifuatwa na mtu.
 
Mishahara imeongezwa kimya kimya mkuu maana ukitangaza wapemba, mangi nao wataongeza bei za bidhaa.
 
Kusema kwamba pesa ipo ya kutosha na Serikali inawanyima nyongeza wafanyakazi ili kuwakomoa,sio kweli,Maghufuri na utawala wake haiitaji kuwakomoa wafanyakazi Ili aibe, afanye ufisadi. Hilo limethibitishwa na uchaguzi wa 2020,hakujali watu wanasema nini, ameiba uchaguzi,na hao wafanyakazi hata Kama wasingempa kura,angeiingia tu Madarakani.

Ni kwamba pesa imeperekwa kwenye miradi, SGR, Ndege,stigres gorge,mishahara ya wafanyakazi sio kipaumbele,
Hata hiyo miradi Mingi imetumia pesa, na Haina tija.

Mfano Dodoma, kuna soko kubwa, soko la "Ndugai"limejengwa kwa pesa nyingi,lakini mpaka sasa hivi, halitumiki kabisa
 
Tatizo watanzania tulizoea kuishi kiujanja ujanja Ndio maana tunaumia
Tii sheria bila shuruti
Lipa kodi
Utafaidi matunda ya awamu hii ya Rais mwema mwenye Moyo wa huruma na upendo kwa RAIA wake
Vinginevyo utaumia sana maana mianya ya wapiga dili imeziba kabisa
 
Tatizo watanzania tulizoea kuishi kiujanja ujanja Ndio maana tunaumia
Tii sheria bila shuruti
Lipa kodi
Utafaidi matunda ya awamu hii ya Rais mwema mwenye Moyo wa huruma na upendo kwa RAIA wake
Vinginevyo utaumia sana maana mianya ya wapiga dili imeziba kabisa
Ujinga tuu unakusumbua
 
Tatizo watanzania tulizoea kuishi kiujanja ujanja Ndio maana tunaumia
Tii sheria bila shuruti
Lipa kodi
Utafaidi matunda ya awamu hii ya Rais mwema mwenye Moyo wa huruma na upendo kwa RAIA wake
Vinginevyo utaumia sana maana mianya ya wapiga dili imeziba kabisa
Utakuwa mtoto wa mama wewe. Ungekuwa unapambana kama sisi wenzako, usingeandika huu ugoro wako.
 
Kama wafanyakazi wenyewe ndio Hawa wenye kauli za "njoo kesho au faili halionekani" hata hicho kidogo wanachopata kingepunguzwa tu.
 
Haya ni maoni yangu binafsi baada ya kutafakari kwa kina, kwanza siamini kwamba suala hili la kukaa miaka 7 bila kupandishwa madaraja na miaka 6 bila nyongeza ya kila mwaka kuwa ni suala la bahati mbaya! HAPANA! Upo msemo kuwa in politics nothing happen by accident!

Sasa twende sawa hapa, kama tujuavyo kamwe! kamwe! huwezi kumtawala mtu na kumfanya afanye unavyotaka huku akiwa ameshiba! Hivyo ukitaka mtu akunyenyekee, mnyime chakula, mnyime maji, halafu mletee chakula kidogo kidogo na maji kidogo kisha muahidi utamboreshea chakula chake wakati ujao! Hakika ataendelea kukutii na kukuheshimu kwa sababu mbili:

1. Kwanza atataka kulinda chakula chake hiki kidogo anachopata ili asife
2. Ataendelea kufanya kazi akiamini kuwa ipo siku ataboreshewa chakula chake

Nasikia eti wakati wa JK wafanyakazi walikuwa jeuri sana! Ndio maana haya yanawakuta.
Kwasasa hata kunyanyua shingo wengine hawawezi na wanafanya chochote kile ambacho BOSS atasema ili kulinda vibarua vyao.

Waliokwenda kusimamia uchaguzi kule Zimbabwe waliambiwa kuwa fanya ufanyavyo MWENYEWE ASHINDE, ole wako asishinde hivyo vyeti vyako utaenda kufungia mandazi.

Wewe unadhani wangefanyaje?

Kwa njaa hii wafanyakazi wanaweza kujikuta wanafanya chochote waambiwacho ili kulinda ugali huu mdogo.
kuweni wavumilivu.
lkn pia waziri wa fedha aliahidi kulipa malimbikizo yenu ya mishahara ili kupunguza ukali wa maisha.
jambo la msingi fanyeni kazi kwa bidii.

hivi lkn na nyinyi wizara ya fedha, Katibu Mkuu kwa nini mnakalia haki za watumishi wenu?! kwa nini msilipe madai yao?!
kukalia haki za watu ni dhambi kubwa sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom