Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,429
- 1,047
Kumekuwepo na ongezeko la kasi ya ajabu la wageni kutoka nchi za Uturuki, Pakistan, Syria, India na China nchini Tanzania. Wageni hawa hutawakuta mahotelini wala kwenye nyumba za wageni (Guest Houses) bali wanakusanyana kwenye nyumba za mitaani zenye mageti makubwa na ulinzi mkali. Katika kutafiti ongezeko hili nimebaini vyanzo vifuatavyo kuwa miongoni mwa njia za walowezi wanaofulika nchini:
- Maonyesho yasiyo na msimu maalumu ambayo sasa yameigeuza Dimaond Jubilee kutoka kuwa ukumbi wa sherehe na kuwa soko la kudumu.
- Chuo cha St. Joseph ambacho umekuwa mlango wa kuingiza Wahindi lukuki kwa kisingizio cha kuja kufundisha. Imefika pahala sasa Kibamba ni Parokia ya Wahindi.