Mapambano dhidi ya UKIMWI

TAWIK

Member
Joined
Nov 6, 2018
Posts
60
Reaction score
87
Baada yakujionea takwimu za maambukizi ya ugonjwa mwezi huu sasa hebu tutete kidogo. Kiukweli serikali na mashirika yanahaha kupunguza ongezeko la maambukizi mapya ya UKIMWI kila kukicha lakini wapi. Licha ya kutoa elimu mbalimbali lakini bado somo halieleweki na hapa sasa hebu tuulizane tatizo ni NINI?.

Kiufupi mimi pia ni mwanajamii hivyo kwakua naishi na watu hebu nitoe sababu kadhaa ambazo naona huenda zikawa vikwazo vya kupambana na adui huyu. Sababu kubwa ni watu wengi hawajui thamani ya maisha. Kwa nchi nyingi za ulimwengu wa tatu ikiwemo Tanzania watu wengi hawajui thamani ya maisha hata ukiwa fukala. Kutokana na ugumu wa maisha watu hawa hawajala vitu vitamu, mavazi mazuri na hata usafiri. Hivyo ukiwasogezea karibu vitu hivi hurukwa na akili nakuona vinathamani kuliko hata uhai wao.

Mara kadhaa nimewasikia watu waliosogezewa starehe wakisema "KWANI UKIMWI KITU GANI" Watu hawa hawajui kama mtaji wa yote hayo ni uzima. Ila sio kosa lao ni UJINGA na UJINGA wao huo ndio unaowapa MARADHI. Pia ikumbukwe kuwa maladhi ndio engine inayosababisha UMASIKINI kwa watu wengi.

Sasa hebu Mimi nawewe tuisaidie serikali sio kupambana na ungonjwa hapana! Tuisaidie kupandikiza uelewa wa thamani ya maisha kwa watu hapo tutapunguza tatizo angalau. Wenzetu thamani ya uhai iko mbele sana! Si ajabu mzungu akamkuta kinyonga barabarani akamvukisha lakini sisi anakula tairi. Tutafute wanasaikolojia watuambie ni kwa VP binadam huthamini maisha yake. Sababu tulitegemea labda MTU akisoma lakini wapi.


KARIBUNI JAMANI JAHAZI LINAZAMA.
 
Wazo zuri, ila pia ushetani nao umezidi, watu ni ngono, ngono ngono tu.

Nadhani ifike mahala tumrudie Muumba na kwa wale waliokwisha upata wakiomba kwa imani watapokea uponyaji kwani hakika Mungu wetu hashindwi na chochote!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…