Mapato ya Zanzibar yafikia shilingi bilioni 2874, sawa na trilioni 2.874 kwa mwaka. Tanzania Bara tunayo ya kujifunza kutoka Zanzibar

Mkuu huyo akili yake ni nyepesi sana. Hivi kweli Unaweza sema uchumi wa mikoa Kama Dar na Mwanza upande kwa asilimia 7 Kama uchumi wa Rwanda kisa idadi ya watu na ukubwa vinakaribiana kulingana?
Kwani haiwezekani?! Nakumbuka miaka michache iliyopita uchumi wa California ulikuwa ni sawa na uchumi wa Ufaransa huku uchumi wa Los Angeles peke yake, ukiwiana na uchumi wa nchi mzima ya Malaysia! Na kwa sasa, nadhani California imeshaiacha Ufaransa including many other developed European countries.

Dar es salaam kwa mfano, kama haiizidi Zanzibar basi nitashangaa sana.
 
Sasa kama mshindi wa kiti cha urais anapatikana kwa kura chini ya 300000 huo si sawa na mkoa mmoja wa bara?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kumbuka znz ni nchi hivyo inakusanya mapato yote ya kodi na yasiyo ya kodi, import duties, ports,domestic revenues,tozo za serikali na taasisi zake, na mgao, tofauti na mikoa, haikusanyi kodi zaidi ya tozo za kawaida za serikali za mtaa.kama kungekuwa na mfumo wa znz mkoa kama Dar ungekuwa na asilimia zaidi sitini ya. mapato, Arusha $ za utalii zote etc
 
Nakubaliana na wewe juu ya kutaja vyanzo vya mapato.
Ukiacha vyanzo vya Customs, mikoa ya Tanzania Bara ina vyanzo vingi sana vya mapato ambavyo havipati msukumo stahiki kutoka Serikalini
 
Mkuu huyo akili yake ni nyepesi sana. Hivi kweli Unaweza sema uchumi wa mikoa Kama Dar na Mwanza upande kwa asilimia 7 Kama uchumi wa Rwanda kisa idadi ya watu na ukubwa vinakaribiana kulingana?
Lengo letu kama ni kujifunza kutoka Zanzibar, naamini yapo yenye manufaa.
Nimewahi kusoma kuwa mapato ya Jimbo la California, nchini Marekani, ni makubwa kuliko nchi kadhaa duniani.
Tanzania imejaliwa mito, maziwa, ardhi na maliasili kadha wa kadha.
Tukijipanga kuimarisha uzalishaji katika nyanja mbalimbali katika mikoa yetu, mapato yataboreka.
 
Mapato ya nchi unataka kuyahamishia mikoani? Akili yako na ya mzee wenu zinafanana.
Sina hakika na bandiko lako, kama ni sifa hasi au chanya.
Lakini mantiki iliyomo nimeielewa
 
Sawa haina shida. Mapato ni Mali ya muungano.
Vipi deni letu la tanesco ameshalipa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Binafsi, naamini lilikuwa jambo la aibu kulitangaza sana deni la Serikali ya Zanzibar kudaiwa na Tanesco.
Sote tunafahamu kuwa Taasisi nyingi za Serikali ya Muungano zinadaiwa sana na Tanesco.
Utangazaji wa madeni ya umeme ya Serikali na Taasisi zake kutoka kwenye Taasisi nyingine ya Serikali ilikuwa ukosefu wa nidhamu.
 
Sawa haina shida. Mapato ni Mali ya muungano.
Vipi deni letu la tanesco ameshalipa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Binafsi, naamini lilikuwa jambo la aibu kulitangaza sana deni la Serikali ya Zanzibar kudaiwa na Tanesco.
Sote tunafahamu kuwa Taasisi nyingi za Serikali ya Muungano zinadaiwa sana na Tanesco.
Utangazaji wa madeni ya umeme ya Serikali na Taasisi zake kutoka kwenye Taasisi nyingine ya Serikali ilikuwa ukosefu wa nidhamu.
 
Kasomee uchumi kwanza ndo uje uanze kupuyanga hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
Ninaheshimu sana elimu pamoja na Wasomi.
Lakini ukweli ni kwamba wazalishaji wa mazao na bidhaa hapa kwetu Tanzania siyo Wasomi.
Angalia Wakulima, Wafugaji, Wavuvi, Wachimba madini, na Wamachinga.
Kama kada hizi zitasaidiwa na hao Wachumi, kwa kupewa elimu halisi ya vitendo, hakika huo 'Uchumi unaosomwa Vyuo Vikuu' utaongezeka na kuimarisha Uchumi wa Nchi.
 
Bandiko lako lina hoja nzito na za msingi.
Wazo langu mimi ni jepesi.
Mathalani, mazao ya michikichi yakiongezeka mara mbili au mara tano, Uchumi wa nchi si utaimarika?
Nchi inaagiza mafuta mengi ya kula toka nje, kwa nini Mikoa yetu isiweke mkazo kwenye kilimo cha Michikichi huko Kigoma, Alizeti katika mikoa ya Kati na ya Kusini, na kadhalika.
Tunaona jinsi Rais Dr. Shein anavyofuatilia kilimo cha Karafuu, Mpunga, Mboga za Majani na kadhalika huko Zanzibar.
Huku kwetu ufuatiliaji unakuwa kama wa kufuata mkumbo.
Mwaka juzi kulikuwa na mkazo wa kilimo cha Mikorosho. Nani anafuatilia kama miche ile iliyogawiwa inaendelea kukua?
Zanzibar ufuatiliaji upo mpaka wakati wa mavuno.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…