Mapendekezo kuhusu maboresho ya Haki Jinai

Mapendekezo kuhusu maboresho ya Haki Jinai

nkobagu

Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
26
Reaction score
11
Nawasalimu wote,

Nianze kwa kumpongeza mheshimiwa Rais SSH kwa hatua anazochukua kuleta maboresho katika mfumo wa "Haki-Jinai", katika hili nimeona ana nia ya dhati kuleta mabadiliko chanya.

Nikiwa mhanga wa mfumo uliopo wa haki jinai nimeshuhudia mabadiliko kadhaa yaliyoanza kufanyika ikiwemo kubadilisha baadhi ya vifungu vya sheria ambapo baadhi ya makosa/tuhuma mtuhumiwa anakamatwa tu pale upelelezi umekamilika ili usikilizaji wa kesi uanze mara moja ili haki itendeke (kwa mujibu wa sheria).

Sanjali hilo kasi ya usikilizaji kesi imeongezeka hivyo kupelekea kupungua mahabusu magerezani ikilinganishwa na enzi za " mwenda zake".

Hivi karibuni amenzindua tume itakayopitia mfumo wa haki-jinai ili kuleta maboresho katika mfumo mzima; hoja ni kwamba nikiwa mhanga wa mfumo wa haki jinai uliopo na ukizingatia tume hiyo imesheheni vigogo wastaafu ambao sidhani kama wanajua madhila ya wahanga wa mfumo wetu wa haki-jinai, ninaomba yeyote kati yetu anajua namna gani ninaweza kupeleka maoni yangu kwenye tume (ikiwezekana ana kwa ana) ninaamini ninazo input ikizingatia nilisweka gerezani (kama mahabusu) kwa miaka mitatu kwa makosa ya "kutengenezwa".

Naomba kuwasilisha.
 
Nawasalimu wote,

Nianze kwa kumpongeza mheshimiwa Rais SSH kwa hatua anazochukua kuleta maboresho katika mfumo wa "Haki-Jinai", katika hili nimeona ana nia ya dhati kuleta mabadiliko chanya.

Nikiwa mhanga wa mfumo uliopo wa haki jinai nimeshuhudia mabadiliko kadhaa yaliyoanza kufanyika ikiwemo kubadilisha baadhi ya vifungu vya sheria ambapo baadhi ya makosa/tuhuma mtuhumiwa anakamatwa tu pale upelelezi umekamilika ili usikilizaji wa kesi uanze mara moja ili haki itendeke (kwa mujibu wa sheria).

Sanjali hilo kasi ya usikilizaji kesi imeongezeka hivyo kupelekea kupungua mahabusu magerezani ikilinganishwa na enzi za " mwenda zake".

Hivi karibuni amenzindua tume itakayopitia mfumo wa haki-jinai ili kuleta maboresho katika mfumo mzima; hoja ni kwamba nikiwa mhanga wa mfumo wa haki jinai uliopo na ukizingatia tume hiyo imesheheni vigogo wastaafu ambao sidhani kama wanajua madhila ya wahanga wa mfumo wetu wa haki-jinai, ninaomba yeyote kati yetu anajua namna gani ninaweza kupeleka maoni yangu kwenye tume (ikiwezekana ana kwa ana) ninaamini ninazo input ikizingatia nilisweka gerezani (kama mahabusu) kwa miaka mitatu kwa makosa ya "kutengenezwa".

Naomba kuwasilisha.
Kweli Watanzania hatujui tunataka nini. Imagine uzi muhimu kama huu haujapata wachangiaji.
 
Kama hujafanikiwa kufikisha maoni yako moja kwa moja kwa tume,jaribu kuyaweka hapa jukwaani.Pengine wajumbe wa tume tuko nao hapa,wanaweza wakayafanyia kazi hata kama siyo yote.
 
Juzi hao watu wakukusanya maoni walofika hapa Shinyanga town kitu cha kushangaza walikutana na wadau (mashirika yasio ya kiserekali ) kwa Dakika 30 tu walikutania Ktk hotel ya virgmark .... Hili ni la kishangaza kidogo how come unakusanya maoni ya wadau kwa dak 30 tu ...
 
Back
Top Bottom