Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Kabla ya mapendekezo haya sheria ilikuwa inasema atakayekutwa na hatia ya kuomba rushwa ya ngono atakuwa ametenda kosa ambapo adhabu yake ni faini isiyopungua milioni 2 na isiyozidi milioni 10, ama kifungo kisichopungua miaka 5 na kisichozidi miaka 10 au vyote kwa pamajo.
Kwenye mapendekezo serikali imetaka kifungu hicho kibadilike ambapo mtoa rushwa na mpokea rushwa wote watawajibika kwa kosa hilo, lengo likiwa ni kumaliza vitendo hivi vya rushwa ya ngono.
Wanaharakati wa haki za binadamu wamejitokeza kupinga mapendekezo haya na kusema inamnyima haki mhanga kwa kufanya wanyamaze na hivyo vitendo hivyo kuendelea.
Ila tukija upande wa pili, kuna ambao wanakuwa kwenye mipango yao na mambo yakiharibika anaenda kumshtaki kuwa alimlazimisha kutoa rushwa ya ngono la sivyo angemyima stahiki zake. Je, hawa waachwe kutamba na sheria iendelee kuangalia upande mmoja?
Lakini pia kuna ambao wanalazimisha kutoa rushwa, jamaa anaingia kingi baadaye anaenda kuchomwa kuwa alilazimisha kupewa ngono ndio atoe haki, je, sheria kubaki kumuadhibu anayesemekana ameomba rushwa ambaye kwenye kesi hii ni mtu mwenye madaraka/mamlaka itakuwa sawa?
Yapi maoni yako Great Thinker wa JF?
Kwenye mapendekezo serikali imetaka kifungu hicho kibadilike ambapo mtoa rushwa na mpokea rushwa wote watawajibika kwa kosa hilo, lengo likiwa ni kumaliza vitendo hivi vya rushwa ya ngono.
Wanaharakati wa haki za binadamu wamejitokeza kupinga mapendekezo haya na kusema inamnyima haki mhanga kwa kufanya wanyamaze na hivyo vitendo hivyo kuendelea.
Ila tukija upande wa pili, kuna ambao wanakuwa kwenye mipango yao na mambo yakiharibika anaenda kumshtaki kuwa alimlazimisha kutoa rushwa ya ngono la sivyo angemyima stahiki zake. Je, hawa waachwe kutamba na sheria iendelee kuangalia upande mmoja?
Lakini pia kuna ambao wanalazimisha kutoa rushwa, jamaa anaingia kingi baadaye anaenda kuchomwa kuwa alilazimisha kupewa ngono ndio atoe haki, je, sheria kubaki kumuadhibu anayesemekana ameomba rushwa ambaye kwenye kesi hii ni mtu mwenye madaraka/mamlaka itakuwa sawa?
Yapi maoni yako Great Thinker wa JF?