Mapenzi si mafurusi

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
1,985
Reaction score
1,286
Katu hapandi farasi, yule mzoea punda,
Mpenda kwenda kasi, mwendo pole humshinda,
Amezoweshwa fenesi, doriani lamshinda,
Sitokalifisha nafsi, nafanya ninayopenda,
Loo! Nina wasiwasi, kwa mambo yanavyo kwenda.

Nipe gongo ya kiasi, nipate ipiga funda,
Na miraa ya Ramisi, kwa ubani naifunda,
Initoe wasiwasi, hata kipoe kidonda,
Niupate na wepesi, wa kumshukia nyonda,
Hivi ni kitu rahisi, kutamka "nakupenda"?

Niko na pepo za kusi, ni mbali ninapo kwenda,
Nimepanda mdungusi, kiasi nikose tunda,
Wenye kupendwa wakwasi, shida nzito huzishinda,
Akina kikaragosi, yetu tu yanatushinda,
Mkononi sina tasi, n’nani atanipenda?

Waja wataka fususi, hawana kitu kupenda,
Ubishi kama chunusi, natafuta pa kupanda,
Aso tabia za fisi, ndiye nitakaye mpenda,
Mwenye kujali nafsi, mafurusi kuyaponda,
Mapenzi ya wasiwasi, wallahi ni kama donda.

Moyo una wasiwasi, akili i'njia panda,
Huyu mja Ibilisi, ni jini msaka tenda,
Kila siku alhamisi, kwake siku huganda,
Si kuna siku nyepesi, na za kukaza mkanda?
kuna siku za furusi, na za mifuko kukonda.

Hili jua la utosi, kila mtu humtenda,
Hata mwenye ukwasi, pia laweza mponda,
Ya jini kuhama rasi, pale kiti anapo konda,
Mwayaiga pasi wasi, ya majini mwayatenda,
Kwa talasimu za ngisi, mioyo mnaiwinda.

Sina hofu sina wasi, tena nenda mwana kwenda,
Kitu changu kimepasi, hakiyumbi kimedinda,
Hupati tena nafasi, dagaa zangu kutanda,
Nimestushwa na unyasi, nyoka alinipa donda,
Nimestuka kirahisi, we endelea kutanda.

Njano5.
0784845394
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…