Mapenzi ya utotoni...

EJM_

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2011
Posts
3,836
Reaction score
2,100
Nakumbuka nilipokuwa primary school tena darasa la pili tulikuwa na kale ka tabia ka kiume ka sijui ni kupenda au what ist called but ni kwamba unaweza kuwa una "wachumba" kumi ambao ni wewe peke yako unawaita wachumba maana hata wao wenyewe hawajui wala marafiki zako pia hawajui.

Sasa nilipata binti wa kwanza ambaye aliniita mpenzi nikiwa darasa la sita, stori yenyewe ilikuwa hivi

Kuna kibinti kilihamia shuleni kwetu na darasani kwetu kutoka shule ya jirani, kilikuwa kirembo kiasi chake na nakumbuka niliwahi kukifanyia kituko kikanipeleka kwa mwalimu nikapewa kichapo so nikakichukia fulani hivi. Sasa tulipoingia darasa la sita kikawa kimepata komunio ya kwanza kwenye mwezi wa sita hivi (rc watakuwa wanaijua hii) sasa kawaida huwa wanajipamba sana watoto wa enzi hizo so nakumbuka mama alialikwa kwenye sherehe ya hicho kitoto maana tulikuwa tunakaa jirani (mtaa wa chini na juu) so tukaenda, siku hiyo kile kitoto kikawa karibu sana na mimi tena kikanihonga na keki na kwenye dance kikaja kunifuata.

Sasa kesho yake tukaendelea na shule na nakumbuka tulikuwa tumemaliza mitihani so tukawa na wiki mbili za kucheza sana na kuzagaa nje (wale waliosoma zamani wataikumbuka hii) so kikaja kina rasta zake na ukweli kilikuwa kinaonekana bomba ile mbaya. Mh kwenye boys group ukawa mjadala na ghafla boys wote wakaanza kusema hiki kitoto kizuri na kila mmoja akajiapiza kumpata, i was one of them ila tukakubaliana kuwa atakayempata awaambie wenzake ili wasitishe mawindo.

To make the story short baadae nikajikuta nimebahatika ingawa sikumbuki ku muapproach, dah nakumbuka the whole school knew na tena na ile kura ya nani anatoka na nani ilipopigwa nilikuwa naongoza ingawa sikupewa adhabu maana mwalimu aliyeiitisha nilikuwa nafanya vizuri sana somo lake so tukawa washkaji sana tu so nikapona hilo soo na nafikiri nikawaponyesha na wenzangu wengine.

Mtindo wa mawasiliano ulikuwa simu za mezani, barua kwenye jalada la daftari na baadae washkaji zangu wakanitenga kwasababu walikuwa wanajua mwisho wa siku nitabaki na hako ka binti na washkaji zake wakamtenga so thats how my primary school love was. Ohhhh it ended kwenye kuitana mpenzi tu and nothing else............ na kupeana kadi zilizofutwa majina na kuandikwa la kwangu.

How was your primary school love?
 
Story nzuri.Mi nilikuaga mkorofi sana ukinitokeatu nakutukana kwa sauti kila mtu asikie. Nakumbuka kuna mmoja aliniandikiaga barua nikiwa std seven nikareply kwenye toilet paper akashika adadu.
 
I had a friend, anaitwa Frida tulikuwa majirani na family friends. Mchezo wetu ilikuwa ni kuwaahidi wavulana waje nyumbani halafu hatutokei. Kesho yake tunasimuliana nani alimshikisha pembe nani!

It was lot of fun. Halafu sex tuliona kitendo disgusting yaani tulifananisha na mtu akufanye wewe jalala la kumwaga uchafu wake!

Tuliendelea na hiyo mpaka form 2 mwenzangu alipoanza kuitazama sex kama kitu kingine. LOL
 
Mi nimecheka tu kwamba kadi anatumiwa dada yake, yeye anaiba, anafuta jina then anakutumia wewe mpenzi wake
 
Story nzuri.Mi nilikuaga mkorofi sana ukinitokeatu nakutukana kwa sauti kila mtu asikie. Nakumbuka kuna mmoja aliniandikiaga barua nikiwa std seven nikareply kwenye toilet paper akashika adadu.
Hahahahaaa kiukweli mi sikumtokea ila ilitokea tu automatically, we nguvu za kumtokea mtu ningezitoa wapi? nakumbuka wakati huo ungeniweka na msichana ambaye nilikuwa na feelings za kitoto naye ningeweza kuzimia
 

Hahahahaa baada ya kukua eeh? Dah mi it took longer than form two mpaka kuja kufanya, i was scared and didnt know what to do coz i never saw it done anywhere before.
 
ahh raha tupu
mpango mzima wa kuenda shule pamoja na kurud....wailes mpk mtaa wa mkuranga ahh mmeongeaaaaaaaaaa weeeeeeee njian ..mmefinyanaaa...ushapelekwa kwa babu chachandu kununuliwa mihogo ahh araha jaman....then badaye kumsindikiza madrasa na mimi ikifika j5 kwenda mafundisho chang'ombe nasindikizwa dahh rahaaa...BT NTHNG LIKE KUVULIANA CHUP...ni unamjali na nakujali...i thk ule moyo ungeendelea mpk kesho ningekuwa dahh...mke mwema bt dah sjui umeenda wap...NAUSAKAAAAAAAAAA😛ainkiller:
 
Mi nimecheka tu kwamba kadi anatumiwa dada yake, yeye anaiba, anafuta jina then anakutumia wewe mpenzi wake
Dah we acha tu nami nikaanza kuiba za uncle wangu nafuta naandika jina lake nampelekea.

Staili ya kupeana sasa, coz siku ukiletewa unaletewa kibao so kinakuwa kimzigo utasikia mkipishana tu unaambiwa kuna mzigo wako kwenye begi lako. Na we ukirudisha you do the same.

It was fun asee
 
Hahahahaaa kiukweli mi sikumtokea ila ilitokea tu automatically, we nguvu za kumtokea mtu ningezitoa wapi? nakumbuka wakati huo ungeniweka na msichana ambaye nilikuwa na feelings za kitoto naye ningeweza kuzimia


mhh mpk leo ugonjwa u unaendelea nao?
 
Nimependa hiyo ya kuiba card na kufuta jina lol....ila naimani ulikuwa unaelewa ni card ya nini manake daaah!
 
Hahahaha! Aisee lol. So zinaibwa zote za xmas, pasaka, eid, get well soon n.k. Kweli raha sana.
 
Hahahahaaa kiukweli mi sikumtokea ila ilitokea tu automatically, we nguvu za kumtokea mtu ningezitoa wapi? nakumbuka wakati huo ungeniweka na msichana ambaye nilikuwa na feelings za kitoto naye ningeweza kuzimia

Mi hata kumuona moyo unaenda mbio na njia nnabadilisha. Nadhani hata baba yangu sikuwa namuogopa hivyo, du!
 
That was a pure child heart ambao hauoni zaidi ya kile kinachotokea wakati huo

Dah si tulikuwa shule wote
kanisani wote
mafundisho wote

Halafu unajua wavulana huwa hatujaliwi sana huko majumbani so kale kabinti kalikuwa kakipewa hela ya shule ya wiki nzima mi ndio nakuwa benki
 

asa bado mnaliendeleza au mlishapotezana?
 
Hahahaha! Aisee lol. So zinaibwa zote za xmas, pasaka, eid, get well soon n.k. Kweli raha sana.
Tulikuwa tunajua bhana, na hata humo tulimokuwa tunaiba nyingi zilikuwa za mapenzi........... halafu nyingine tulikuwa tunatengeneza wenyewe unachora na vi kopa kopa
 
asa bado mnaliendeleza au mlishapotezana?
Tumemaliza shule tu likaishia pale, ila siku moja tulikutana kikazi baada ya miaka mingi sana dah tukasalimiana tu briefly and then i went to remember how we used to be tukiwa watoto
 
Mhh enzi hizo, nakumbuka pia cards zilikuwa zinapuliziwa perfume, ukiifungua inatoa manukato! Barua zilitawaliwa na kutumiana picha halisi na saa nyingine zile za kuchora za moyo na mkuki, pia nakumbuka maneno magumu ya kiingereza tuliyokuwa tunayatumia kwenye barua zetu kwa wapenzi baada ya kuanza sekondari, Loh!
 
Story nzuri.Mi nilikuaga mkorofi sana ukinitokeatu nakutukana kwa sauti kila mtu asikie. Nakumbuka kuna mmoja aliniandikiaga barua nikiwa std seven nikareply kwenye toilet paper akashika adadu.

Hahahaha....iliwahi kunitokea
 
story za utotoni zinauma maana unanikumbusha miaka 1985 nifanya kituko cha mwaka pale nilipokutana na msichana mmoja na kumpa thumuni alifurahi sana huyo msichana na kila alipokuwa ananiona hata shuleni alikuwa anapenda niwe naye karibu
 
mi nilipotinga darasa la tano nikapata kavulana ambako kalikuwa kanapendwa na wasichana wote nikAwa kinara darasa lote kuanzia mkondo A mpaka D ,too bad nilivyofika la sita kuingia la saba nikahamia mkoa mwingine nilikaa zaidi ya miaka kumi na mbili ndio tukaonana tena kale kaupendo baina yetu bado kapo though kila mtu ana mwenza wake tumebaki tu kuwa good friends
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…