Mapenzi yamesababisha urafiki wetu uvunjike

Huu upupu Mura!!! Ningekugecha vibaya swain Wee tena kiroboto
 
So sad wot goes around comes around itakurudia kwa huyo huyo ana na rafik yko mwingine
 
Kuna wakati unaweza kuwa na mtu ilimradi tu, alafu akatokea yule mtu wa ndoto zako sasa, inakuwa haina jinsi, life isnt fair just like that. Wakati mwingine inabidi tuelewe tu japo ngumu kumesa.
Sasa mbona anasound like mtu ambaye haenjoy huo uhusiano, he was dragged into it na Anna. Smh

Fine watu wanakutana kupitia njia mbalimbali, inawezekana na wao hii ndo destiny yao (naomba isijenitokea njia ya hivi), ingawa mshkaji ni kama analiwa na "guilt" slowly, na he will never know peace hadi siku watakaposameheana na huyo rafiki yake otherwise hatoacha kujikuhukumu. Kinachonishangaza sijui kama ndo kuomba msamaha au kudeclare kwamba he is innocent, yeye amejiweka kama victim tu wa situation. Anna alimuomba namba; alianza kumtext, akamlazimisha wawe wanaonana posta daily, akamlazimisha wafanye mapenzi, akajihamishia kwake, akajibebesha mimba, akaanza kumtambulisha kwa ndugu zake without his consent, analazimisha kuweka uhusiano wao open, atamlazimisha na ndoa lol etc. Hivi huyu mwanaume yeye ni sanamu linaongozwa tu au ni mtoto mchanga, kwamba yeye hana ufahamu wa kujisimamia akasema hiki sikitaki? Me mtu irresponsible afu anajikuta he can't own up to his mistakes tutazinguana. Maana hata kwenye ndoa utakuwa unaletewa na watoto wa nje, afu still atasema yeye hakutaka tu ila hao wanawake ndo walimlazimisha*****.

Kuna vitu hatuvifanyi out of respect bana, kutembea na mpenzi wa rafiki yako, that's weird, haifai kwa kweli hata kama wameachana, let alone kumzunguka. By the way, IMO; Anna sounds like an opportunist, otherwise mwanamke wa kawaida tu asingeweza kumshobokea hivyo shemeji ake tena siku tu ya kutambulishwa, she stooped so low.
 
Yaani ipo siku utapata alichokipata rafiki yako na uchungu utakaousikia utakuwa mara mbili yake
Ila wanawake nao ni mashetani sana wana tamaa km mbwa huyo mwanamke alikubalije kuingia kwny mahusiano na mtu asiyempenda kw dhati? Matokeo yake anakuja kumwacha jamaa na kidonda kisichopona shetwani sana huyo mwanamke ni muuaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…