Mapenzi yananiua

Tatizo kubwa la wanawake huwa mnakabidhi mioyo yenu pasipo kusoma mchezo

Mi naona bora afe tu


hahahaha, yaani kuna watu wanapekenyuaga matatizo maishani mwao, hapo ndio mwanzo wa kuharibikiwa na maisha kama hajui, akibugi step tu imekula kwake na atajuta maisha yake yote, hapa bado hayajamuua asubiri mbeleni.
 
Ndugu yangu pole sana...........ushauri wangu ni kuwa usikilize moyo wako,na kamwe usikubali kushinikizwa na kitu au mtu yeyote yule,free yourself from any circumstance whatsoever which envisages a little bit of a blackmail or something,do not want the baby to be a shield to someones blackmail...............huu ni mtazamo wangu tu,you have the decision.
 
AshaD=FaizaFoxy!! So yupoyupo sana tu hapa!! Id zote 2 anazitumia!!
 
Just a pre caution, umesema huyo wa kwanzaa(mjamzito) ulikua nae kwasababu ulidhani kua unampenda
sasa kua makini manake inawezekana hata huyo wa pete bado huna uhakika kua ndie unaempenda.
hivi vitu me naviogopa kama nin!
 

...kaka huna msimamo kaka,....acha kuchezea mioyo ya binadamu wenzio.
Hivyo visingizio vya usongo wa mawazo, ujauzito, ujana, mtoto ...yote ni katika kuficha madhambi yako.

Wote huwafai kwani hujui nini unalotaka maishani.
Jipe muda. Endelea kutoa mahitaji na matumizi kwenye kumlea mwanao.
Sikiliza moyo wako, utapokuwa tayari tafuta Mke ambaye utampenda na kumuoa ili uishi nae milele
sio kwa sababu za usongo wa mawazo, ujauzito, mama wa mtoto au ujana wa kuvishana pete.
 
unajua bro ,mm sijapenda ulivyo fanya sio. kama nitakukera samahani, na madhali umeweka bayana kutaka ushauri subir nikueleze kweli, ,, why? ulimpa mimba uyo dada na hukua ukimpenda? nini malengo yako kwake? umesha haribu maisha yake ,, na hukua na love juu yake hata kidogo,unajua man hapa ndipo munapo kosea.. hiyo ni parnishment na ni saiz yko munatakiwa mujifunze na makosa,, dada wa watu alikusabilia bcz alikua amini na alikupenda,kumbe ww unampenda mwengine,, ata kua mm siwez kukusamehe daima,, samahani wanajamii lakin nahis kama ,, niliofanyiwa mm hivi ,, au mtu afikirie awe mwanamke kama mm afanyiwe hivyo nn ata hisi???
 
Hajui maana ya kupenda na kutamani.................yaani jogooo akishawika tu unamvisha mtu pete!! Duh si watakufilisi sasa? sina msaada kwako hata punje maana hata ulivyowamimba sisi (mimi) sikuwepo bana. Kwani Ndomu bei gani na huyu naye keshokutwa ukija hapa na kutuambia hukumpenda ila shetani alikupitia tutakuelewaje? Bana eee wakubalie wote ukae nao....bahati gani hio mdogo wangu unaichezea? sisi wengine tunabanwa hata pa kutokea hatuna sasa wewe unao wawili baada ya kushukuru unaleta longolongo.....faida yake kubwa ni kwamba una uhakika wa chakula kila siku maana "mvua" zikinyesha kijiwe hiki unahamia kijiwe kile unaendelea kula msosi and vice vers is true. Ila ole wako wote "MVUA" ziwe zinanyesha msimu mmoja...utakoma maaana kwanza wanakuwaga wakali na kisirani bila sababu yoyote inayojulikana kijamii; sasa ukichanganya visirani vya wote wawili!!!! haya bana take care just kidding Mpwa, fanya uamuzi sahihi.
 
Vaa mask ya Sadam Hussein au Gadaffi. Mtoto ni zaidi ya pete hata kama humpendi mama yake. cha kufanya wapige chini wote aza upya. Ujana wako umeutumia vibaya.
 
Pole sana,ila ulifanya uzembe sana kwenda kavu kavu kwa huyo usiyempenda,itabidi umuoe huyo unayempenda kama atamtambua huyo mtoto.Mweleze ukweli huyo demu uliyezaa nae atambue hata kama ukimuoa bado humpendi.
 
Dah! Una wakati mgumu kweli aisee, washirikishe ndugu zako unaowaamini uweze kutatua kesi hiyo.....
 
Siku zote naamini ndoa itadumu tu kama chanzo chake kilikuwa ni upendo na si huruma. Ila hao wanawake wote wawili ni characters. Yani wanakugombea. Eti wanasema watarogana. aaah. Ungekuwa na moyo wa chuma ningekushauri uwapige chini wote wawili utaoaje wanga bwana! Utalishwa mauchafu wewe mpaka uwe taahira! Yeyote utaye muoa lazima akupe limbwata utulie maana kama washahapa kurogana unadhani watarogana wao tu wewe wakuache?

Tafuta wife material bwana hachana na hao wadada hawakufai.
 

Wakishindwa kurogana wao watamroga yeye ili wote wakose! Kilichopo ni kwamba atumie akili ya ke na busara alizonazo kuchagua the best way (si unawaambia tu ukweli). Labda niulize: Una < 18 years??????
 
Jamaa ndio ameishakiri kua kakosea, anachoomba mumsaidie afanye nini?? Au amuone Pinda akapate ushauri wa maamuzi Magumu???
 
In maana bado unawakula wote?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…