SoC04 Mapinduzi ya Usimamizi wa Taka: Teknolojia ya SMART DUMPSITES itakayotokomeza taka mitaa yote Tanzania

SoC04 Mapinduzi ya Usimamizi wa Taka: Teknolojia ya SMART DUMPSITES itakayotokomeza taka mitaa yote Tanzania

Tanzania Tuitakayo competition threads

FMH

New Member
Joined
May 1, 2024
Posts
1
Reaction score
1
Kuongezeka kwa idadi ya watu ulimwenguni kumesababisha ongezeko kubwa la uzalishaji wa taka ngumu na vimiminika katika mazingira yetu. Ambapo ni asilimia 40 tu ya taka ngumu zinahifadhiwa katika madampo (dumpsites) na asilimia 60 zinatupwa kiholela katika mazingira, hii ni kwa mujibu wa Sanga et al. (2022). Kadri taka hizi zinavyozidi kuongezeka kwenye mazingira, ndivyo madhara mbalimbali ya kiafya na kimazingira yanavyojitokeza, na kuacha jamii bila kuelewa chanzo cha matatizo hayo ni nini. Kwa mfano, ongezeko la matatizo ya kansa na matatizo ya mfumo wa fahamu yanachangiwa na uwepo wa taka zenye sumu kama vile metali nzito (heavy metals) katika mazingira. Hapa Tanzania, tunazalisha takribani tani milioni 12.1–17.4 za taka kwa mwaka, ambapo kiasi kikubwa cha taka kinatupwa kwenye mazingira bila utaratibu na kiasi kingine kinapelekwa kwenye madampo, hii ni kwa mujibu wa Singh, S. G. (2021). An Assessment of the Solid-Waste-Management Ecosystem.

Kutokana na ongezeko kubwa la taka ngumu na changamoto mbalimbali za usimamizi wake hapa Tanzania, Hali hii inahitaji suluhisho la kisasa na endelevu. ni muhimu kuanzisha mbinu mpya na za kisasa za usimamizi wa taka, ambazo zitahakikisha hakuna taka zinazotupwa kiholela. Kwa kutumia teknolojia za kisasa kama vile urejeleaji (recycling), na matumizi ya nishati mbadala zinazozalishwa kutoka kwenye taka, Tanzania inaweza kufikia lengo la kuwa na dampo janja (Smart-Dumpsites) katika siku za usoni. Hii itawezekana tu kwa ushirikiano wa karibu kati ya serikali, sekta binafsi, na wananchi katika kubuni na kutekeleza mipango hii.

Dampo janja (Smart Dumpsites)
Ifuatayo ni ubunifu wa kiteknolojia (Smart Dumpsite)unaoweza kuwa tiba ya usimamizi na hatima ya taka ngumu katika mazingira yetu, ambao unaweza kutekelezwa katika kila halmashauri hapa Tanzania.

Eneo la Dampo
Eneo lililotengwa kama dampo kwa ajili ya kutupwa taka linatakiwa lifungwe mtambo wa gharama nafuu wenye uwezo wa kubagua taka kulingana na aina zake. Mtambo huu unaweza kubuniwa na kutengenezwa hapa hapa nchini Tanzania, ukizingatia vigezo vya kiufundi na kiuchumi vilivyopo.

Hatua kwa Hatua za Uendeshaji wa Mtambo
  • Kupokea na Kuchambua Taka
Taka zinapowasili dampo, zinapimwa na kuchambuliwa awali ili kutenganisha taka za plastiki, chuma, karatasi, na taka zinazooza.
  • Kuchakata Taka Zinazooza
Taka zinazooza zinachakatwa na kubadilishwa kuwa mbolea ya asili kwa kutumia teknolojia ya kuchakata taka kama vile mtambo wa composting. Mbolea hii itauzwa kwa wakulima kwa gharama ndogo, mbapo kutokana na unafuu na upatikanaji wa mbolea kwa bei nafuu itawahamasisha wana jamii wenyewe kubagua taka zao wakiwa nyumbani au maeneo wanapozalisha taka.
  • Kuchakata Taka za Plastiki na Chuma
Taka za plastiki na chuma zinachakatwa na kubadilishwa kuwa bidhaa mpya ambazo zinaweza kurudishwa kwenye matumizi. Hii inaweza kufanywa kupitia teknolojia ya urejeleaji (recycling) ambapo plastiki zinaweza kusafishwa, kuyeyushwa, na kutengenezwa kuwa bidhaa mpya kama vile viti, meza, na vifaa vingine vya plastiki ambavyo pia vitauzwa kwa wanajamii kwa bei ya chini na wakati mwingine vinawza kupelekwa hata nje ya nchi kwa mauzo na kuongeza kipato cha halmashauri husika. Kipato hicho pia kinaweza kutumia kuendesha shughuli nzima ya ukusanyaji, na usafirishaji wa taka kutoka kwenye makazi na maeneo ya uzalishaji kwenda dampo janja (smart dumpsite)
  • Uchujaji na kutibu Maji Machafu (Leachate) kutoka kwenye taka
Ndani ya mtambo huo kuwe na sehemu maalum kwa ajili ya kuhifadhi na kutibu mchuzi (leachate) wenye sumu unaotokana na taka ngumu. Hii inaweza kufanyika kwa kupanda mimea maalum inayofyonza sumu hizo au kwa kutumia mfumo wa kibiolojia wa kusafisha maji kwa sisayansi phytoremediation. Kwahiyo sumu zitokanazo na taka hazitatapakaa kwenye mazingira yetu hivyo mimea tunayo itumia kwa chakula itakua salama na maji ya visima yatakua salama kutokana na upenyaji wa mchuzi huu wenye sumu chini ya ardhi. Hivyo basi magonjwa yasiyo ya kuambukiza yatokanayo na utupaji ovyo wa taka yatakua yamedhibitiwa na kuiacha jamii ikiwa na tabasamu.
  • Mabaki ya Taka pamoja na taka zingine zitumike Kutengeneza Gesi ya Methane
Mabaki ya taka ambazo zimechakatwa yasitupwe ovyo, badala yake yakusanywe pamoja na kuchakatwa kuwa gesi ya methane kupitia mchakato wa (anaerobic digestion) kuchakata pasipo hewa ya oksieni. Gesi hii inaweza kugawiwa kwa shule za bweni, jeshini na magereza na kusaidia kupunguza matumizi ya kuni na mkaa, hivyo kuchangia katika uhifadhi wa misitu na kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi au Ukaa.

Hivyo basi kama kila halimashauri itaamua kutumia techinologia hii, kutakua na usimamizi mzuri wa taka na jamii itahamasika kutilia maanani suala zima la usimamizi wa taka ngumu.

Faida zingine za moja kwa moja zitokanazo na tekinolojia hii ni pamoja na Kupunguza Uchafuzi wa Mazingira, Kuboresha Afya ya Umma, Kuwezesha Uchumi na kukuza uelewa kwa jimii yote juu ya maswala ya uhifadhi wa mazingira na namna rafiki ya kusimamia taka katika maeneo ya makazi na maeneo mengine ya uzalishaji wa taka.

NB: Tekinolojia hii inaweza kuanza kutumiaka kwenye halimahsuri zenye uzalishaji mkubwa wa taka kama (pilot study) harafu kwa awamu ya pili kuanzishwa kwenye halmashauri zingine zote


Marejeleo:
Sanga, V. F., Pius, C. F., & Fikira, K. (2022). Heavy metals pollution in leachates and its impacts on quality of groundwater around Iringa municipal solid waste dumpsite . 1– 24.

Singh, S. G. (2021). An Assessment of the Solid-Waste-Management Ecosystem.
 
Upvote 4
Back
Top Bottom