Mapinduzi ya Zanzibar - Januari 12, 1964

P...

MWANAHISTORIA ANAYACHAMBUA MAPINDUZI NA MAANA YAKE

Ayatollah Mohammed Said: Radio Uhai FM

SWALI:
Sherehe za mapinduzi kadri tunavyoendelea kuziadhimisha vizazi vinavyokuja vinajifunza kitu gani?

JIBU
Kwanza ni kuwa watu wengi washajua ukweli wa mapinduzi. Na hayana nguvu au umuhimu kama viongozi wetu wanavyodhani. Watu wanataka maendeleo na utangamano, wamepiga kura hapa ya serikali ya umoja wa kitaifa, umeona matokeo yake, watu wengi wamepiga kura kutaka serikali ya umoja wa kitaifa.

Sasa yale mambo ya mapinduzi, ya sijui tulikuwa tukifanywa hivi na vile, hakuna mtu sasa anayetaka kusikia hivyo. Mambo hayo yanepita. Watu wanataka kutizama mbele. Na kuona nchi inatoka kwenye umasikini inakwenda kwenye maendeleo. Kadri tunavyokwenda ndio hawa wana mapinduzi wanavyozidi kupoteza nguvu.

Kama nilivyokuambia mwanzo kama kweli haya mapinduzi yana nguvu hivyo mbona wanashindwa kushinda uchaguzi huru na haki??

SWALI:
Uligusia pale mwanzo sheikh Mohammed kwamba kuna swala moja kubwa sana kila unapotazama historia ya kweli kabisa iliyoandikwa kuhusu mapinduzi yanazungumzwa masuala ya mauaji makubwa sana ambayo yalitokea. Hiyo inabaki kuwa ni kumbukumbu kubwa sana. Haya mauwaji yalitokana na msigano wankitu gani. Nini sababu hasa?

JIBU:
Ndio, Profesa Ibrahim Noor akaandika kitabu kile "Propaganda na udini Tanzania", akaonesha tarekh yake. Zile propaganda za kuwa Waarabu walikuja kukamata watumwa. Utumwa umefanywa na mataifa mengi. Hakuna utumwa mbaya kama ule wa Trans Atlantic Slave Trade - unaotoka Afrika magharibi na kuvuka bahari kwenda Marekani. Ule ndio unyama mkubwa. Hakuna utumwa mbaya kama wa Ubelgiji Kongo. Hawayasemi hayo. Wao kila siku wanawasingizia Waarabu tu. Na ukiwapeleka huko huwa hawana la kusema, wananyamaza kimya. Hizi propaganda ndizo zilizosababisha mauaji makubwa sana kutokea baada ya miaka zaidi ya 150 kuondolewa kwa biashara ya utumwa.

Miaka kama 20 iliyopita tusingeweza kufanya kitu kama hiki watu wakatusikiliza. Leo hivi tunazungumza bila ya matatizo. Na vijana wetu wanatakiwa waelezwe ukweli wa historia. Kuwa hii ni historia. Na usemwe ule ukweli. Watu wanaelewa. Na ndio maana kwa kuelewa kwao huko wanamapinduzi wanashindwa kushinda chaguzi huru.

SWALI:
Hebu nisaidie kunifumbua kidogo hata kwa jinsi ulivyosoma tu. Turudi nyuma zaidi ya 1964 kwanzia miaka ta 1952 uliozaliwa wewe kwenda nyuma, je maisha ya Zanzibar yalikuwa ni ya namna gani?

JIBU:
Nitakwambia kitu kimoja. Kulikuwa na watu wana nafasi zao katika jamii ya Waarabu hili huwezi kuliepuka. Haya yote ni katika madhara ya ukoloni. Na Sultan alikuwa hana nguvu hivyo. Nguvu zote alikuwa anazo Muingereza.

Kulikuwa na Waarabu masikini wakifanya kazi za vinyozi, wakilima, wakiuza kahawa mitaani, na wengine wakifanya kazi za utopasi zile za kutapisha choo, zamani vile vyoo vya shimo wanakuja kupakuwa na wakibeba kwa mapipa kwenda kumwaga. Si kama Waarabu wote walikuwa katika hali ya juu. Walikuwepo masikini. Wakitumikishwa kazi kama anavyotumikishwa Muafrika. Ukisoma kitabu cha Profesa Ibrahim Noor utayakuta haya yote. Na hizi chuki wanazosema ni za kupandikiza. Sultan aliondoka Zank

pDr zibar bila ya kuuwa raia wake, aliondoka mikono misafi haina damu ya mtu yeyote. Damu imeanza kumwagika baada ya hao wanaoitwa wanamapinduzi kushika serikali. Ndio wakaanza kuuwa watu na kuwaweka kwenye jela za mateso. Nadhani nimelijibu suali lako.

#Pray4Zanzibar

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizo ndugu yangu ni ndoto za mchana. Kwa miaka yote mmejaribu kila namna na mmeshindwa nangoja nione kwani kila enzi ina mambo yake na ile enzi hairudi tena.
 
Nawasalimu katika jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwatumia salaam zangu za kuadhimisha kumbukumbu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, tutayalinda kwa gharama yoyote.

Nawatakia maadhimisho mema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Kazi Iendelee!.

Paskali
 

Njaa
 
Mzee Mohamed upo?...
 
Mkuu JokaKuu kwanza hongera kwa bandiko zuri .
.
Niko Interested kujua ukweli juu ya mapinduzi ya Zanzibar na maisha ya John Okello baada ya mapinduzi.
Karibu mitaa hii Mapinduzi ya Zanzibar: Mchango wa John Okello (Che Guevara wa Afrika Mashariki) umefutwaje?
P
 
Nawasalimu katika jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwatumia salaam zangu za kuadhimisha kumbukumbu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, tutayalinda kwa gharama yoyote.

Nawatakia maadhimisho mema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Japo sasa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yanaelekea miaka 60, Miaka 50 Ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Bado Kuna Maswali Bila Majibu -1

Kazi Iendelee!.

Paskali
 
Mapinduzi ya Zanzibar yana upotoshaji mtupu historia imepindishwa kwa hali ya juu sana.

Wanamapinduzi halisi hawatajwi wanatajwa wale waliojifungia ndani siku ya tukio.

Kwangu sioni umuhimu wa kuadhimisha uongo .
 
Kama baada ya miaka takriban 60 Mapinduzi yanahitaji kulindwa kwa nguvu zote kuna walakini pahali.
Najiuliza mapinduzi ya Marekani na Ufaransa bado yanalindwa kwa nguvu?
 
It was genocide, Mauaji ya kimbari yaliyodhaminiwa na Uingereza, yaliyoongozwa na Nyerere pamoja na Waisrel ili kuuondoa Uislam katika upande huu wa Afrika

Cha kushangaa Uislam umezidi kupamba moto Zanzibari,


Mapinduzi ya Zanzibar sio kitu cha kujivunia, Wazanzibari wengi sana, wasio kuwa na hatia, walipoteza maisha siku ile

May God cursed that day..
 
Mwana JF, Paskali, anakutakia wewe na familia yako HERI YA SIKUKUU YA MAPINDUZI MATUKUFU
YA ZANZIBAR!
Paskali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…