Mapishi ya Chapati: Jikoni kwa Evelyn Salt & Mentor

Hongera sana kwa mapishi. Hapo kwenye namba 15, binafsi huwa navuta gently hiyo chapati kwa kutumia finger tips. Napata mdabwada mwembambaa halafu nakunja duara kuanzia ncha ya juu. Hapo unapata thin layers kweli.

Kuokoa muda huwa ziachi kikando kwa nusu saa kabla ya kupakaa mafuta. Naacha baada ya kupakaa mafuta.

Niwe mkweli, sijapika chapati siku nyingi. Nna excuses kama 10[emoji4]
 
Itakua hupendelei vitu vya mafuta ndio mana au samli inakukinaisha

Vitu vya mafuta nakula sana aisee.

Thank goodness nina fast metabolism na ni gym rat la sivyo ningekuwa kama Le Mutuz😀.

Huwa napenda sana kukaanga samaki [Tillapia] na kuku kwenye deep fryer na huwa natumia olive oil.

Nadhani itakuwa ni ngano inayonipa hiyo 'replete feeling'.

Ila ingekuwa ni ngano basi maandazi nayo yangekuwa yananipa hiyo feeling lakini nikiyala huwa sijisikii kama vile ambavyo huwa najisikia nikila chapati.
 

Ni samli kaka Nyani Ngabu ndio inakufanya ujiskie ivo
 
Kuna uzi niliwahi kusoma hapa ulisema maji ya kukandia yawe ya baridi kiasi ndio chapati zinakuwa laini... hongera kwa mapishi
Hakuna chapati laini vizuri kama inayomixiwa na maboga...niliwahi kula mahali flani kiukweli ni nzuri.

Nilielekezwa namna ya kupika kuwa ni hivi:-

-Unapika maboga kawaida kisha yakiiva unablend na maji ya uvuguvugu itakuwa kama siagi, baada ya muda mfupi unachanganya kwenye unga wa chapati kisha banika chapati zako.

Wallah...ni tamu na laini kwelikweli.
 
Olive oil....like Bertoli, that's best cooking oil with no colestral at all

Mkuu unajua kula vya afya haswaa, ila ya gharama hayo mazee...sisi tunakomaa na sunola tu yakhee.
 
Pompeian ndo fav brand yangu.

Inanogesha sana ladha. Hususan ile first cold press...

So good, at times we use bertoli at home,

Hayo ukikaangia samaki...then veggies juu, daah utafill ladha safi sana.
 
Natumia maji barid au ya kawaida nadhan maji moto yanafanya ile nyama inawiva, tofaut kwenye maandazi inasaidia kuumua sabab ya hamira. Ila ile PPF hata ukandie nin itatoka bila kukanda muda mrefu
 
Whaaat!
Naanza kumkazia apike chapati


Chunga tu usije kumfukuza shemeji!




asante Nifah.

Aisee umenikumbusha swedish pancakes..dah! nitajaribu siku moja. Sema sasa likizo zimeisha na mai-waifu a.k.a wifi yako Evelyn Salt akishaanza kushika chaki anakuwa bize. Ila tutajitahidi anifundishemo mapishi mapya mara moja moja.


Nice chapati kaka Mentor hongera wifi Evelyn Salt

Binadamu kama nyie ndo mnahitajika duniani.

I know it is not perfect lakini hiyo ndiyo chapati yangu YA KWANZA EVER kupika...!

Hahahaha lol umenikumbusha me nliambiwa mkono wangu wa mzungu ulitokeza kwenye upishi wa vitumbua lol

Ahahah atakuwa alikuwa huyuhuyu KakaJambazi !???
 
Mhhhhhh hii ni kweli jamani?
Maboga kwenye chapatti?
Ngoja nitacheki na chef wangu nimuulize...nataka kujua mapishi mbalimbali na kwa ufasaha ili hubbie to be afurahie mapishi yangu always [emoji12]
 
Mhhhhhh hii ni kweli jamani?
Maboga kwenye chapatti?
Ngoja nitacheki na chef wangu nimuulize...nataka kujua mapishi mbalimbali na kwa ufasaha ili hubbie to be afurahie mapishi yangu always [emoji12]
Ni kweli kabisa, sisi tulishapikiwa na binti mmoja wa kikamba na ni laini haswa.

Jaribu uone, kisha ulete mrejesho.
 

Heri ya mwaka mpya kwako.

Naam na mimi nitajaribu hiyo kutengeneza layers nyembamba next time..sijui itakuwa lini lol!

Halafu je, kuchemsha mafuta kabla ya kuyachanganya na unga nayo una manufaa gani? au nayo ni mazoea tu?



Usije ukapikiwa chapati ngumu kuliko maisha yako

Ahahah naona anatafuta recipe for divorce!
 
Mi chapati huwa zinanijaza tumbo [zinanifanya nijisikie nimeshiba mno] sana.

Hivi mpo mlio kama mimi?

Na kwa sababu hiyo huwa sizili mara kwa mara.
Hata mimi aiseee!! Na huwa siwezi kula zaidi ya moja na ninashiba kweli, hapo kula tena ni hadi saa tisa au kumi alafu ndio basi.
 
Chapati zina kazi, yaani wanangu wakisema "mamdogo tunataka chapati" najikuta nimechoka ghafla.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…