Mapishi ya Firigisi za foil

Mapishi ya Firigisi za foil

MBITIYAZA

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2017
Posts
14,947
Reaction score
26,074
Nipende kuwatakieni heri ya Christmas na mwaka mpya wanajf wote!

Imezoeleka kupika vyakula vile vile kwenye sikukuu kubwa kubwa !

Leo tugeukie upande wa pili wa nyama !
Firigisi ni nyama tamu sana; hebu leo tengeneza firigisi za foil kwa familia yako

Maandalizi:

Andaa firigisi zako, zioshe vizuri

Weka viungo uvipendavyo (swaumu, tangawizi, pilipili manga, karoti, hoho, vitunguu vingi(hivi viweke kwa uwingi kuliko kiungo chochote yaani kata hata vitunguu vitatu in cubes))

Changanya hivyo viungo na hizo firigisi zako kisha ziache kwa muda kiasi kwenye friji ziingie viungo

Weka katika foil na ufunge vizuri

Weka kwenye oven(hata mkaa inawezekana) ila hakikisha unaweka kwenye moto mdogo ili ziive vizuri

Muhimu: Weka hata saa moja hivi kama watumia mkaa na uwe unageuza lile foil ili kupata moto kote!

Hakikisha kuna kasupu kamebakia huwa kana ladha mujarabu

Angalia kama zimeiva fresh

Chakula hiki waweza kula na ugali au pilau au wali pemben na juice baridii!

[HASHTAG]#mbiti[/HASHTAG]
 
chunga: foil ikiyeyuka hata kidogo na kupinga kwenye chakula ni hatari kwa afya yako. Kila anayekula vya foil ni mhanga wa magonjwa yasiyojulikana. Kama vile vile anayekula vilivyopikwa kwa sufuria za aluminium. Maendeleo na changa moto!!!!!!!!!
Turudie kwenye vyungu na majani ya migomba ndugu zangu.
 
chunga: foil ikiyeyuka hata kidogo na kupinga kwenye chakula ni hatari kwa afya yako. Kila anayekula vya foil ni mhanga wa magonjwa yasiyojulikana. Kama vile vile anayekula vilivyopikwa kwa sufuria za aluminium. Maendeleo na changa moto!!!!!!!!!
Turudie kwenye vyungu na majani ya migomba ndugu zangu.
sawa sawa mkuu !bas toa foil weka kwenye majan ya migomba vndika kwenye majivu !easy
 
[emoji39] [emoji39] [emoji39] [emoji39]
 
Sikusoma yote unatengeneza sumu yakulisha watu wako bila kujua foil sumu
 
Hivi kwa nini wengine tunapenda kula vizuri lakini habari za mapishi zinatuchefua?

Ni ugumegume au nini?
 
Back
Top Bottom