pangakali 2
JF-Expert Member
- Aug 9, 2019
- 239
- 221
Habarini za asubuh wakuu.
Tukumbuke nyuma kidogo. Nakumbuka mara yangu ya kwanza kumiliki simu ilikua mwaka 1999 nilikua mwanza nikiwa kwenye daladala mara pap naona simu kwenye siti tulivyofika nyakato nikawa wa mwisho kushuka jasho linanitoka balaa. Nikawaza kuitangaza nikaona itakua halali ya Kondatka. Nikajipa moyo kuwa sijaiba atakaye jitokeza nitampatia.
Nimekaa nayo mwaka mzima ndani bila kuitumia. Matokeo ya darasa la saba yalivyotoka nikaenda kuanza form one Wilaya fulani Mkoa wa Kigoma. Kwa kipindi iko matumizi ya simu za mkononi yalikua bado hayajafika. Tukiwa form two Voda wakazindua mawasiliano. Hapo ndio nilianza kuitumia rasmi kwa mara ya kwanza. Kwa kweli ilinisaidia sana kupata pata vijisent kwa ajili ya kujikimu. Kwa waliokuwa wanahitaji kubip nilikua nawatoza sh 50, kutuma ujumbe 100.
Je? Ewe mwana JF mwenzangu ulimiliki simu yako kwa mara ya kwanza mwaka gani na uliipataje?
Tukumbuke nyuma kidogo. Nakumbuka mara yangu ya kwanza kumiliki simu ilikua mwaka 1999 nilikua mwanza nikiwa kwenye daladala mara pap naona simu kwenye siti tulivyofika nyakato nikawa wa mwisho kushuka jasho linanitoka balaa. Nikawaza kuitangaza nikaona itakua halali ya Kondatka. Nikajipa moyo kuwa sijaiba atakaye jitokeza nitampatia.
Nimekaa nayo mwaka mzima ndani bila kuitumia. Matokeo ya darasa la saba yalivyotoka nikaenda kuanza form one Wilaya fulani Mkoa wa Kigoma. Kwa kipindi iko matumizi ya simu za mkononi yalikua bado hayajafika. Tukiwa form two Voda wakazindua mawasiliano. Hapo ndio nilianza kuitumia rasmi kwa mara ya kwanza. Kwa kweli ilinisaidia sana kupata pata vijisent kwa ajili ya kujikimu. Kwa waliokuwa wanahitaji kubip nilikua nawatoza sh 50, kutuma ujumbe 100.
Je? Ewe mwana JF mwenzangu ulimiliki simu yako kwa mara ya kwanza mwaka gani na uliipataje?