Mara ya mwisho Arsenal kutwaa Ubinhwa wa EPL

Christopher Wallace

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2015
Posts
1,479
Reaction score
3,788
Miaka 13 sasa toka Arsenal atwae ubingwa wake wa mwisho EPL, mambo mengi yametokea na hata kupita, tujikumbushe baadhi ya mambo hayo;

1. Kikwete ameingia madarakani ametawala miaka 10 na sasa amestafu.

2. Rais wa Marekani alikuwa ni George Bush.

3. Messi bado alikuwa nyumbani kwao Argentina.

4. Mtandao wa Tigo ulikuwa unaitwa Buzz.

5. JamiiForums ilikuwa bado haijaanzishwa.

6. Chama Kikuu cha Upinzani kilikuwa ni CUF

7. Boko na Bunju kulikuwa ni mapori watu wanaenda kuwinda.

Endelea na wewe...
 
Chelsea ilikuwa haina kombe ila sasa wana vi5 plus uefa and europa
 
Guadiola alikuwa bado ni mchezaji.

Mtandao wa Twitter ulikuwa bado haujaanzishwa.

Tanzania tulikuwa na majiji mawili tu(Dar na Mwanza).

Lakini pia tusisahau tangu Arsenal achukue ubingwa wa EPL hakuna tena timu nyingine iliyochukua ubingwa ule wa kihistoria kama alivyofanya Arsenal.

Tunafahamu kuwa Arsenal alichukua ubingwa bila kupoteza mechi hata moja msimu mzima tena kwa kikosi cha gharama nafuu kabisa kisichozidi £31m.

Na alivunja record iliyokuwa imedumu kwa muda wa miaka 115 kwenye EPL ambapo awali ilikuwa inashikiliwa na Preston.
 
Wewe mtoa post ni limbukeni ktk kushabikia timu za ulaya. Zipo rekodi nzuri na bora zimewekwa na timu ya arsenal pale uingereza na hazijavunjwa ni timu yoyote hadi sasa.
Ni arsenal hawa waliotwaa ubingwa wa epl pasipo kupoteza mechi hata moja licha ya ugumu wa ile ligi ni 2003/2004.
Ndiyo timu pekee iliyotwaa kombe la heshima uingereza mara bingo la FA kuliko timu nyingine yoyote pale kwa malikia.
Ndiyo timu iliyoshiriki mashindano ya uefa mara nyingi kuliko timu yoyote pale uingereza na kupata mafanikio kiuchumi kupitia ushiriki huo.
Imefika fainali ya uefa mara ya mwisho 2006 na kutolewa na Barcelona mara baada ya mchezaji wake golikipa kupewa red card hivyo kulazimika kupunguza mchezaji mmoja ndani ili kuruhusu kuingia golikipa mpya. Bado walitoka 2-1 magoli yote yakipatikana baada ya kucheza pungufu.
Mafanikio ni mengi, kila timu Klabu ina la kujivunia. Timu kama Chelsea, mancity, totenham hazikujulikana kabisa ktk medal ya soka na mashabiki wake mlio wengi ni wale mmetoka majuzi kijijini mmekuja mjini mkajua kuna supersport .
Washabiki halisi wa mpira utawakuta man u, Liverpool, arsenal, everton, newcastle na Aston Villa.
Sasa nyie wa kuja msitusumbue na ujinga wenu wa kuiponda arsenal utadhani ushabiki ni sare mburula nyie hadi tushabikie timu moja.
Nyinyi wengine ni mashankupe tu mnaohama timu kila kukicha na kushinda mitandaoni kutukana mashabiki wa timu nyingine.
Ungejua hakuna mwaka arsenal haijapata kuvuka bila kupata kombe lolote sasa sijui mnataka nini.
Njoo na povu uwezavyo ila najua arsenal ikirudi njia zake vizuri wewe utakuwa shabiki wake mkuu kwa uhamiaji wako haramu ulionao. Tuheshimiane tena tuheshimiane mno.
Arsenal ndiyo chama langu tangu 1994 wewe sijui ulikuwa wapi nisisonge mbele sana juu yako bann isije ikanihusu.
 
Hivi kumbe kufungwa Fainali na Barca ni mafanikio? Ningekuwa mimi ndio mtoa mada ningekununulia Pepsi baridiiiii
 
Hivi kumbe kufungwa Fainali na Barca ni mafanikio? Ningekuwa mimi ndio mtoa mada ningekununulia Pepsi baridiiiii
Yaani timu haijawahi fika hata fainali achilia mambo ya kombe na nyingine inaishia makundi bado wewe unaona ni sawa.
Akili yako unawaza hiyo pepsi tu.
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…