Marais wa Tanzania kujengewa Makumbusho Dodoma

Marais wa Tanzania kujengewa Makumbusho Dodoma

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Serikali inakusudia kuanza ujenzi wa Makumbusho ya Marais katika Mji Mkuu wa Taifa letu, Dodoma. Akizungumzia hatua hiyo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Pindi Chana amesema wapo Viongozi wengi walioihudumia Tanzania na Wizara imeona ni wakati mwafaka kuanza ujenzi.

Kwa mujibu wa Waziri Chana, Makumbusho itasaidia kuonesha kwa jamii mchango wa Marais katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi kwa kipindi walichokuwa madarakani.

Swali fikirishi: Wakati kuna changamoto mbalimbali zinazowakumba Wananchi, kuanzia gharama za maisha, utoaji huduma na nyinginezo, ni kweli huu ni wakati "mwafaka" wa Makumbusho?

Kwanini jitihada kubwa sana zinatumika kuonesha "mchango" ilihali ni sehemu ya wajibu wa Viongozi wetu?
 
Makumbusho haitoshi, waruhusu watu waandike vitabu vya kupitia mapito ya viongozi hao kwa uwazi na usahihi siyo kutuonesha sanamu na mapicha au habari za magazeti ya serikali na chama kuwa ndicho chanzo pekee cha kukumbushia legacy za viongozi hawa.


Simulizi za kina mzee Mohamed Said, Mzee Thani n.k pia ziruhusiwe kushapishwa na kuwekwa ktk kumbukumbu za makumbusho





 
Serikali inakusudia kuanza ujenzi wa Makumbusho ya Marais katika Mji Mkuu wa Taifa letu, Dodoma. Akizungumzia hatua hiyo, Waziri wa Maliasili na Utalii,...
Huu Ni ulimbukeni Sana tunatumia nguvu kuuubwa kulazimisha viongozi wetu kukubalika !

Kuna mmoja alitoa amri historia ya Tanzania ifundishwe upya kuanzia chekechea Hadi chuo kikuu ,

Kukaandalia mtaala na vitabu matokeo yake Mungu alipompenda ZAIDI Hilo wazo likafutwa kumbe asilimia 85 ya hiyo historia ilikuwa ya huyo kiongozi eti kwa miaka 6 tu history yake ndiyo ijulikane kwa chekechea Hadi chuo kikuu.

Afrika ninani aliyeturoga?
 
Naona tabia ya kujitwalia utukufu wa mmoja tuu aliye juu ya yote unaendelea.

Hakika kwa mtindo huu, muda si mrefu mwenye wivu na kushare utukufu wake ataonyesha hasira zake tena, iwapo tusipoachana na tabia hiyo.
 
Makumbusho ya kiongozi mmoja itatembelewa Sana kuliko kawaida, Lissu akiwa rais ataifunga( japo hawezi kuwa rais), sijamtaja huyo rais
 
Hii nchi Sasa hivi inaendeshwa ka ma vikoba,huyu Mama anaongea nini!!
 
Huu Ni ulimbukeni Sana tunatumia nguvu kuuubwa kulazimisha viongozi wetu kukubalika !

Kuna mmoja alitoa amri historia ya Tanzania ifundishwe upya kuanzia chekechea Hadi chuo kikuu ,

Kukaandalia mtaala na vitabu matokeo yake Mungu alipompenda ZAIDI Hilo wazo likafutwa kumbe asilimia 85 ya hiyo historia ilikuwa ya huyo kiongozi eti kwa miaka 6 tu history yake ndiyo ijulikane kwa chekechea Hadi chuo kikuu.

Afrika ninani aliyeturoga?
Shenzi! Umesema kweli tupu Aisee!
 
Safi kabisa kumbukumbu mujarab kama hizi zitasheheni hapo makumbusho
IMG_20220713_141753.jpg
 
Serikali inakusudia kuanza ujenzi wa Makumbusho ya Marais katika Mji Mkuu wa Taifa letu, Dodoma. Akizungumzia hatua hiyo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Pindi Chana amesema wapo Viongozi wengi walioihudumia Tanzania na Wizara imeona ni wakati mwafaka kuanza ujenzi.

Kwa mujibu wa Waziri Chana, Makumbusho itasaidia kuonesha kwa jamii mchango wa Marais katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi kwa kipindi walichokuwa madarakani.

Swali fikirishi: Wakati kuna changamoto mbalimbali zinazowakumba Wananchi, kuanzia gharama za maisha, utoaji huduma na nyinginezo, ni kweli huu ni wakati "mwafaka" wa Makumbusho?

Kwanini jitihada kubwa sana zinatumika kuonesha "mchango" ilihali ni sehemu ya wajibu wa Viongozi wetu?
Ndio tumekopa kwasababu hiyo?hatari wasisahau kuweka na kumbukumbu ya wavuvi kuchomewa nyavu halali bilakusahau risasi 16
 
Serikali inakusudia kuanza ujenzi wa Makumbusho ya Marais katika Mji Mkuu wa Taifa letu, Dodoma. Akizungumzia hatua hiyo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Pindi Chana amesema wapo Viongozi wengi walioihudumia Tanzania na Wizara imeona ni wakati mwafaka kuanza ujenzi.

Kwa mujibu wa Waziri Chana, Makumbusho itasaidia kuonesha kwa jamii mchango wa Marais katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi kwa kipindi walichokuwa madarakani.

Swali fikirishi: Wakati kuna changamoto mbalimbali zinazowakumba Wananchi, kuanzia gharama za maisha, utoaji huduma na nyinginezo, ni kweli huu ni wakati "mwafaka" wa Makumbusho?

Kwanini jitihada kubwa sana zinatumika kuonesha "mchango" ilihali ni sehemu ya wajibu wa Viongozi wetu?
Ndio vipaumbele vya ccm[emoji25]
 
27 July 2022
Nairobi, Kenya

Rais Uhuru Kenyatta afungua kituo cha historia ya taifa la Kenya


Kituo hicho kilichopo ktk eneo la Bustani ya Uhuru / Uhuru Park jijini Nairobi limekusanya kumbukumbu mbalimbali zilizo ktk maandishi, picha, vifaa, mavazi, wanyama, sehemu tajwa tengefu, Simba wa Tsavo, Ujenzi wa reli enzi ya mkoloni, kumbukumbu ya hali ya hatari wakati wa MauMau, mashujaa wa kupigania uhuru wa Kenya, idadi ya makabila, siasa, wapigania uhuru na pia viongozi wakuu wa Kenya kiasi kwamba mgeni kutoka nje au raia wa Kenya anaweza kutembele kituo hicho kwa masaa kadhaa na kupata picha halisi ya historia nzima ya taifa la Kenya na tunu zake za asili.
Source : KTN News Kenya
 
Makumbusho haitoshi, waruhusu watu waandike vitabu vya kupitia mapito ya viongozi hao kwa uwazi na usahihi siyo kutuonesha sanamu na mapicha au habari za magazeti ya serikali na chama kuwa ndicho chanzo pekee cha kukumbushia legacy za viongozi hawa.


Simulizi za kina mzee Mohamed Said, Mzee Thani n.k pia ziruhusiwe kushapishwa na kuwekwa ktk kumbukumbu za makumbusho





Mzee Mohamed Said ni mpotoshaji mkubwa hafai hata kusikilizwa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mzee Mohamed Said ni mpotoshaji mkubwa hafai hata kusikilizwa.

#MaendeleoHayanaChama

Pia kazi hii kutunza kumbukumbu ya historia ya mataifa la Tanganyika na Zanzibar yanayounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haitakiwi isimamiwe na chama tawala pekee maana itapotosha ukweli.


Kazi hii ya anzisha kituo cha kuhifadhi kumbukumbu, hadithi na historia ya jamii zote kuanzia utamaduni, shughuli za kijamii, siasa, mapambano ya kuleta maendeleo ya watu, maendeleo ya vitu n.k inapaswa kuondokana na ukiritimba wa chama cha Mapinduzi ili kumbukumbu zote za nyanja mbalimbali zisipotee na kubaki historia ya CCM tu.

Soma zaidi : source : Kwanini Tanzania hatuna majengo ya kifahari, minara, na makumbusho zinazotambulika duniani?
 
Kila rais ajengewe jumba lake la makumbusho.
Kuna marais jumba lao litaota nyasi
 
Mji wa Bagamoyo iliopo ktk pwani iwe ndiyo eneo la kuhifadhi historia yote ya taifa la Tanzania.


Maana tayari kuna majengo ya kale yanayohitaji kuhifadhiwa na pia hilo Jumba la Historia ya Taifa lijengwe Bagamoyo badala ya Dodoma kutokana na kuwa mji huu mdogo wa Bagamoyo unaweza kuwa eneo mahususi la kumbukumbu na utalii endelevu wa kihistoria kwa Tanganyika yote.

Bagamoyo eneo lenye urithi, mali-kale, lililohifadhi siri nyingi



Source : NIANIMAARIFA
 
Sijui kwanini nimekumbuka Lincoln Memorial and other things along the National Mall in DC

Anyways
Vijengwe vitu vizuri
Like a Museum hivi
Gharama yaweza kuwa nafuu ila pavutie
 
Back
Top Bottom