Marais waliowahi kuongoza wakitumia wheelchairs

Marais waliowahi kuongoza wakitumia wheelchairs

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
2,428
Reaction score
3,937
Kuna kitu nimesikia hivi karibuni kuna watu wanasema 'hatuwezi kujibizana na mgonjwa'. Mimi nimeichukulia kauli hiyo kama tu kucheza na fikra za watu wengi (hasa huku kwetu wengi bado wanawachukulia walemavu kama robo-watu) kuwa mlemavu hajakamilika na kwamba hana uwezo wa kuongoza.

Nimetafakari jinsi maraisi wengi wa nchi kama Marekani wanapopata nafasi ya kuongoza, wanatumia changamoto mbalimbali walizopitia au wanazopitia kubadilisha maisha ya wengine wenye matatizo hayo hayo.

Nikamkumbuka Franklin Delano Roosevelt (maarufu kama FDR), mmoja wa maraisi ambao Wamarekani wanamchukulia ni bora zaidi kutokea nchini kwao na duniani kiujumla. Huyu ni Raisi PEKEE wa Marekani aliyeshinda kwa miula 4 katika historia ya Marekani (na hakufanya hivyo kwa kuchakachua katiba). Kilichofanya nimkumbuke ni kwamba karibu miaka 10 kabla ya kushinda uraisi alipata ugonjwa (kuna wanaosema ni polio) uliomlazimisha kutumia gongo, leg braces na wheelchair. Alitawala kipindi chote cha uraisi (miaka 12) akitumia hivo vitu.

Kwenye biography aliyoandika mke wake, anasema experience hiyo ilimfanya FDR kuyaangalia maisha katika jicho tofauti, kujenga uvumilivu na kutokata tamaa. Zote hizi zilikuwa ni sifa zilizomsaidia sana katika kuongoza.

Ni muhimu nikipoint kuwa kipindi kile wasaidizi wa FDR walijitahidi sana asipigwe picha akiwa kwenye wheelchair. Bado kipindi kile hata wao walikuwa na ‘stigma’ ya uwezo wa mtu mwenye ulemavu.

Ningeomba mtakaosoma uzi huu mgoogle historia nzima ya FDR na utendaji wake kama Raisi na discussion nzima ya ugonjwa wake. Kuna mengi ya kujifunza.



FDR - fransklin roosevelt - 1941.jpg


FDR - fransklin roosevelt - 1924.jpg
 
Mwisho wa siku ni lazima tukumbuke kwamba mbali na haya yote yanayotokea sasa sisi ni Watanzania na ndugu.

Hizi kauli baina ya CHADEMA na CCM tunaweza tukazifurahia kwa kipindi hiki kwasababu hatuoni madhara yake kwa huu muda mfupi.

Lakini siku Lissu au Magufuli wanakuwa hawapo ndipo tutajua kwamba kuna umuhimu wa kuwafunga lijamu hawa wanasiasa kwasababu nyufa wanazozijenga CCM na UKAWA kwa kipindi hiki zitakuja kuligharimu taifa huko mbeleni.
 
Ni kweli FDR aliugua polio. Wakati huo haikuwepo chanjo ya polio. Chanjo ya polio iligundulika miaka ya 50 na kitu tu.
 
Amewagonga ambapo hawakutegemea wajinga Lumumba

Ndio maana wanahangaika na ujinga kuliko ujinga wenyewe


Unamtoa seya unamkaribisha ikulu unamtafutia studio ili uonekane nani ?



Akili za kijinga ziko mbele yetu
 
So unataka kuharibu kabisa matumaini yetu kuwa jembe halitaingia tena kwenye mpini!!Lisu atatembea na atawakomesha wote waliomdhulumu(kama na yeye hajadhulumu lakini) Inch'Allah!
 
So unataka kuharibu kabisa matumaini yetu kuwa jembe halitaingia tena kwenye mpini!!Lisu atatembea na atawakomesha wote waliomdhulumu(kama na yeye hajadhulumu lakini) Inch'Allah!

Hamna, haikuwa nia yangu hiyo. Lissu ni mtu muhimu sana kwa taifa hili, kwanza nadhani watanzania kwa ujumla wetu tayari tumemuangusha. Tumeshindwa kusimama naye kumtetea. Naamini tungepiga kelele kwa umoja wetu, wasingeendelea na michezo hii wanayofanya ya kutelekeza uchunguzi na kupiga danadana malipo ya matibabu. Mwisho wa siku wanaanza kumuita ‘mgonjwa’ kwa kejeli.
 
Back
Top Bottom