Marehemu Nyaulawa, kuugua mpaka kufa kwake

RIP Nyaulawa

Kuhusu wabunge watatu wa jimbo hilo kufa kabla ya kumaliza muda wao nafikiri waombaji waende kulishughulikia hilo jambo.
 
Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi. Amin
 
Mwenyezi Mungu aiweke Roho ya Marehemu Nyaulawa mahali pema Peponi!! Amin
 
RIP Richard Nyaulawa, Mwenyenzi Mungu iongoze familia pamoja na ndugu na marafiki katika kipindi hiki kigumu
 
RIP Nyaulawa. Poleni wafiwa.

Hii habari ya wabunge watatu wa jimbo hilo kufariki kabla ya kumaliza muda wao, inaweza kuzua maswali.

Inaweza kuzua maswali hapa Jf ama huko Mbeya?
 
R.I.P Richard
Mungu ampe faraja mjane,watoto pamoja na familia ya Nyaulawa
Ulitoka mavumbini na mavumbini umerudi
 
RIP Nyaulawa,

Nadiriki kusema kuwa yeye ndiye muasisi (indirectly) wa JF. Nadhani JF ni matokeo ya kufa kwa BCS baada ya discussions kule kuwa moto mno na hivyo kufungwa.
 
Poleni sana familia na wana Mbeya Vijijini. Hakushiriki pia kuanzisha ACB?+Bussiness Care nk? Nani kumrithi kupitia CCM yetu? Najua pale CHADEMA hawana chao, sio kama Tarime

.....ndiyohiyo

Acha siasa hapa. Mambo ya Tarime na haya ni tofauti sana. Kama unataka kumrithi subiri tumalize kuomboleza. Ah! watu wengine bwana, wanakera!!!!!!!!!!!!!
 
Poleni sana wafiwa. Naomba kuuliza kidogo; hivi wagombea UBUNGE na URAIS wa nchi wanalazimika kupima AFYA zao kabla ya kuruhusiwa rasmi kugombea?
 
Ndugu,


Richard Nyaulawa. Upate raha ya milele, na mwanga wa milele ukuangazie. P.K.A

Wasalaam,

JJ
 
RIP Richard...vijana wa majira tutakukumbuka kwa mengi na hasa kwa kutoa nafasi na ajira kwa vijana...
 
Kwa wale watakopenda kushiriki katika safari ya mwisho ya kumsindikiza Mbunge wetu,

Mwili wa Marehemu utawasili nyumbani kwake Mtaa wa Mzimuni, Kawe Majumba Sita, Barabara mpya ya kuelekea Bahari Beach siku ya Jumatano Saa Nne Kamili Asubuhi, na Kufuatiwa na Ibada ya Kuuaga Mwili wa Marehemu na Buriani Katika Kanisa Katoliki alilokuwa anasali la Mtakatifu Martha - Mikocheni (Kwa warioba). Ibada kanisani hapo itaanza saa Saba Mchana. Kwa yeyote yule na kwa imani zetu tofauti, tuungane kumuombea apumzike kwa Amani......

Raha ya Milele Ampe ee Bwana, Na Mwanga wa Milele Amuangazie,
Marehemu Apumzike kwa Amani. Amina.
 

RIP Mh. Nyaulawa wote ndio njia.Poleni wafiwa wote na wana Mbeya.
Mungu naye anapenda watu wazuri ndio maana wanatangulia wanaachwa waovu!!
Bwana alitoa na Bwana ametwa, jina lake lihimidiwe!!
Amen
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…