Marekani: Aliyetumbuliwa na Rais agoma na kudai ataendelea na kazi Jumatatu, mama Kijakazi ateuliwa kuchukua nafasi yake

Mwasilu

Member
Joined
Feb 2, 2021
Posts
29
Reaction score
30
Mheshimiwa Rais Joseph Biden wa Marekani amemteua Bibi Kilolo Kijakazi kuwa Kaimu Kamishna wa Shirika la Hifadhi ya Jamii, Social Security Administration.

Uteuzi wa Mama Kijakazi unafuatia kufukuzwa kazi kwa aliyekuwa anashikilia nafasi hiyo Bwana Andrew Saul ambae alikataa kujiuzulu mwenyewe alipoombwa afanye hivyo na Rais Biden.

Bwana Saul, ambae aliteuliwa na Rais wa awamu ya 45, Bwana Donald Trump, amepinga vikali kutumbuliwa kwake akidai Rais hana mamlaka ya kumfukuza kazi kwa vile uteuzi wake unalindwa kikatiba , jambo ambalo limepingwa na Rais Biden akirejea uamuzi wa nyuma wa mahakama ya rufaa ya nchi hiyo ambao Rais amedai unampa mamlaka hayo.

Bwana Saul amesema ataripoti kazini kama kawaida Jumatatu asubuhi kwa kujiunga kwenye mtandao wa shirika akiwa nyumbani kwake na kuchapa kazi.

Mama Kilolo Kijakazi ndie aliyewafahamisha wafanyakazi wenzie kwa njia ya barua pepe kwamba ameteuliwa kukaimu uongozi wa taasisi hiyo huku akimshukuru Bwana Saul kwa utumishi wake wa umma.
 
Bongo hata tukipewa Katiba ya Marekani bado kuna matatizo yataendelea kuwepo, matatizo mengine ni kutokana na utamaduni tulionao.

Nakumbuka kipindi cha Magufuli unakuta kiongozi akitajwa jina na Magufuli basi anasimama kabisa hakai hadi aambiwe, hata alipoingia Mama Samia hizo nidhamu za uoga za aina hiyo ziliendelea.
 

Na leo ndio jumatatu
Sauli amefika ofisini? Kijakazi anasemaje😂😂
 
Lakini pamoja na internet accesss zake kukatwa viongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni ya Republicans wamesema sakata bado bichi na kuahidi kwamba Mama Kijakazi atakapoletwa bungeni kuhakikiwa hapiti

Kwa sasa Mama Kijakazi atalazimkka kuongoza taasisi hiyo kwa kukaimu tu mpaka hapo atakapokubalika kaputia mchakato wa bunge wa kuhakiki wateule, confirmation.

Huku kwetu hatuna uhakiki, Rais anaweza kuteua yeyote tu na akapeta


 
Kazi iendelee tuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…