Marekani ipo tayari kuishauri Tanzania kuhusu usalama wa mpaka wake na Msumbiji

Marekani ipo tayari kuishauri Tanzania kuhusu usalama wa mpaka wake na Msumbiji

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Balozi.jpg
Serikali ya Marekani ipo tayari kutoa ujuzi na ushauri kwa Tanzania katika masuala ya kiusalama ili kuimarisha ulinzi kwenye mpaka wake na nchi ya Msumbiji.

Katika mahojiano maalumu na BBC Balozi wa Marekani nchini Tanzania Donald Wright alieleza namna ambavyo Marekani inavyoguswa na tishio la usalama katika baadhi ya mipaka ya Tanzania ikiwemo eneo la mpakani mwa Tanzania na Msumbiji.

Aidha ameelezea athari ya mabadiliko ya tabia nchi lakini pia hatua iliyopigwa na serikali ya Tanzania katika kukuza demokrasia.

Balozi Wright alisema, “Kimsingi Marekani inaguswa na masuala ya kiusalama ya dunia nzima, na hata ukiangalia masuala ya kiusalama katika mipaka ya kusini mwa Tanzania. Kama Balozi natambua na kuweka suala hilo kuwa kipaumbele cha ubalozi wangu…

…tunafikiri kwamba masuala haya yasipoangaliwa kwa umakini yanaweza kuleta madhara, hivyo tumekuwa tukijielekeza katika masuala haya, na tunafurahi kuona Rais Samia Suluhu ameushirikisha umoja wa nchi za kusini mwa SADC ili ziweze kutoa suluhisho na sisi tupo tayari kutoa ushirikiano wetu wa kimawazo pale utakapo hitajika.”

Hali ya Demokrasia Tanzania
Balozi amepongeza jitihada za serikali ya Tanzania ya sasa kutokana na mazungumzo ambayo yamekuwa yakiendelea kati ya serikali, chama tawala na vyama wa upinzani.

Balozi huyo alisema,Rais Samia ameonyesha jitihada kubwa katika suala zima la maridhiano ya kisiasa amekuwa na mikutano kadha kukutama na viongozi wa upinzani ili kupata mariadhiano ya kisiasa na kupata maoni yao hivyo sisi Marekani tunasimama na serikali na kwamba tunaunga mkono kufikiwa kwa maridhiano hayo.

Athari za mabadiliko ya tabia nchi
Hata hivyo Balozi Donald amezungumzia nia ya Marekani kuisadia Tanzania katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Alisema, “Naomba niseme kwamba suala la mabadiliko ya tabia nchi ni janga linazoathiri mataifa mbali mbali duniani, hivyo mabadiliko ya tabia nchi ni eneo muhimu ambalo tunaliangazia pia,na ambalo limekuwa likisababisha ukame,katika ukanda wote wa nchi za jangwa la Sahara,ilikuwa ni mwaka mmoja tu uliopita Kenya ilikumbwa na janga nzige waliodhoofisha uzalishaji katika mashamba ya mawese…

“…kwa hiyo kutaendelea kuwepo na majanga kama hayo hivyo tunataka kushirikiana na serikali ya Tanzania kuhakikisha tunatoa msaada,” alisema Balozi huyo.


Chanzo: BBC
 
Wakae huko huko na ushoga wao maana unamkaribisha sebuleni mwisho unamkuta chumbani kwako na anakutoa nje walahi!
Mabeberu and big NO[emoji2959]
 
Loo! Mimi nilifikiri mpaka uko shwari kwa sasa kumbe kuna kitisho hicho?
 
Hatuna Pesa sisi ya kuweka uzio
Kila mtu anakula kwa kamba yake
 
Serikali iwe makini sana inapofika suala la usalama na urafiki na USA.

Kuna masuala hakuna namna Taifa linahitaji uwekezaji mkubwa hasa kwenye maarifa na technolojia.
Usalama unahitaji watu wenye akili na vifaa vya kisasa, ninaposema watu wenye akili namaanisha.
Tuna tatizo la kutokuwa serious na kujali watu wenye akili na vichwa timamu.
 
Wameanzaaa, Wanataka kuchonganisha tupigane watuuzie Mizinga[emoji849]
 
September 11 walikuwa wapi kufanya hivyo nchini kwao?
 
Kwa hiyo yupo concerned na usalama wa Watanzania Ila wa wakwao hata wakifa poa. Wamalize kwanza matatizo Yao ndipo waje kwetu. Waache unafiki.
Screenshot_20220708-142525.jpg
 
Back
Top Bottom