Marekani: Miili zaidi yapatikana katika jengo lililoporomoka Florida

Marekani: Miili zaidi yapatikana katika jengo lililoporomoka Florida

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Wakati shughuli za uokoaji zikiendelea katika jengo la ghorofa 12 lililoporomoka siku ya Ijumaa nje kidogo ya mji wa Miami, Florida nchini Marekani, miili zaidi imetolewa katika kifusi cha jengo hilo.

Watu 9 waliripotiwa kufariki kufikia siku ya Jumapili, akiwamo mtu mmoja aliyefariki akiwa hospitalini, huku wengine zaidi ya 150 wakiwa hawajulikani walipo. Wengine 8 wameokolewa na wapo salama.

Marekani imeomba msaada wa wataalamu wa uokoaji kutoka Israel na Mexico baada ya shughuli za uokoaji kutatizwa na moto uliokuwa ukiwaka katikati ya kifusi siku ya Jumamosi.

Kitendawili cha jengo hilo kuporomoka bado hakijatenduliwa. Vyombo vya habari vya Marekani viliripoti kuwa mwaka 2018, wahandisi walionya nyufa katika msingi wa jengo hilo na kuwa lilihitaji ukarabati mkubwa. Ripoti hiyo ilionesha pia uwepo wa nyufa katika nguzo na kuta za eneo la kupaki magari katika jengo hilo.

Zikiwa zimepita zaidi ya saa 80 tangu kuporomoka kwa jengo hulo, waokoaji wanasema bado kuna matumaini ya kuwapata wahanga wakiwa hai. Wakati huo, familia na marafiki wa wakazi wa jengo hilo wanasubiri kwa hamu taarifa zozote kutoka kwa timu za waokoaji. Baadhi yao wametoa sampuli za vinasaba (DNA) ili kuwatambua kwa urahisi watakaookolewa.

Mmiliki wa jengo hilo, Erick de Moursa anasema alipaswa kuwepo nyumbani wakati jengo hilo lilipoporomoka, lakini alishawishiwa na mpenzi wake kubaki naye usiku, umbali wa takriban kilomita 3 kutoka eneo jengo lililoporomoka, na kuyaokoa maisha yake.

“Ni Mungu tu. Kwangu mimi huu ni muujiza,” raia huyo wa Brazil aliliambia Shirika la Habari la Reuters.

Chanzo: Al Jazeera

1624813677997.png

Mwanamke akisali katika ufukwe wa Miami, Florida wakati waokoaji wakiendelea kutafuta miili katika kifusi cha jengo hilo | Picha: Reuters
 
June 24/2021

A massive rescue operation is underway after an apartment building close to Miami Beach collapsed in the early hours of this morning.
The ocean-front building, a twelve-story apartment complex called Champlain Towers South, has partially collapsed, fire rescue services have confirmed.
Neighbours say the building was mostly occupied but it is not known what caused the tower which was built in 1981 near 88th street and Collins Avenue in Surfside, Florida, to collapse.
There are fears that many people may be dead or remain trapped beneath the rubble at Champlain Towers South as a search-and-rescue operation by local authorities got underway.
One witness, who was staying in the south Florida island city with his family, was in a neighbouring building at the time and said the collapse sounded and felt like a tornado or earthquake, Fox News reported.
The witness claimed that much of the building was occupied at the time of the collapse, which he estimated to have occurred at around 1.20am.
He told the publication: 'It was the craziest thing I ever heard in my life.'
Shocking video footage showed a boy being pulled from the wreckage by firefighters as the huge search-and-rescue operation continued, according to NBC6.
13754823_446176879720381imagea251624527818284_jpeg2dfaf17ce961f95806d5f1c3d0e1f240.jpeg

13755064_screenshot20210624113417newsbreak_jpegb88afce135043212d91ad5e2f45a4818.jpeg

13755724_2_jpegea571676ce9b75b0730a5d56350ae93e.jpeg

13755725_3_jpeg182845aceb39c9e413e28fd549058cf8.jpeg

Some of these people(down pic) were rescued from the Surfside condo building that’s partially collapsed.
13753175_img20210624112744_jpeg833a7755c278d1796c13b3d0e4b7df16.jpeg


Possible Failure Point Emerges in Miami Building Collapse.
Some engineers looking at the failure of a 13-story condo tower in Florida said the collapse appeared to have begun somewhere near the bottom of the building.

It's in Miami, Florida too, where in 2018, a pedestrian bridge stretching across a street on the Florida International University campus in Miami collapsed on a Thursday afternoon, killing multiple people. 👇
6834855_screenshot20180315210731_jpegde32ca0aeee82497b8a2d39d15d6130b.jpeg
 
Bado kunachunguzwa, hawajapeana final findings to what happened, but according to residents, the building had some cracks I think, and they had already informed the manager. We'll know more soon.
mzee umeripoti vizuri sana
 
Back
Top Bottom