#COVID19 Marekani: Wananchi wadaiwa kununua Kadi bandia za Chanjo zilizopo mtandaoni

#COVID19 Marekani: Wananchi wadaiwa kununua Kadi bandia za Chanjo zilizopo mtandaoni

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Kiongozi wa Wademocrat katika Baraza la Seneti nchini Marekani Chuck Schumer leo ametoa wito kwa mamlaka za nchi hiyo kukomesha mauzo ya vitambulisho bandia vya chanjo ya Covid-19 vinavyouzwa mtandaoni.

Wito wa Schumer unafuatia ripoti za shirika la habari la Associated Press zilizofichua jinsi watu wananunua kadi za chanjo mtandaoni.

Hali hiyo imezua wasiwasi mkubwa miongoni mwa maafisa wa shule na vyuo vikuu nchini Marekani vinavyohitaji uthibitisho wa mtu kuchanjwa dhidi ya Covid-19 kabla ya kuruhusiwa kuhudhuria masomo darasani.

Schumer amezitaka idara za ulinzi wa mipaka, shirika la upelelezi la FBI kwa kushirikiana na wizara ya afya kufanya operesheni ya pamoja kukomesha kadi bandia. Amezitaka pia mamlaka za serikali kuu kuendesha kampeni ya kuwakumbusha raia kwamba kugushi kadi za chanjo kunaweza kupeleka gerezani.
 
Wanajipa hasara bure kuigundua kua ni feki ni kitendo cha dakika 1 tu kusearch serial number kwenye mtandao.
Kwa Tanzania, kabla hujachanja inabidi ufanye booking kupitia Chanjocovid.moh.go.tz na ukishafanya tu unapokea serial number kwenye simu yako.

Na kwenye documents zako kuna hadi batch Number ambayo inapatikana kwenye kichupa cha chanjo uliyochanja.
 
Kwa Tanzania, kabla hujachanja inabidi ufanye booking kupitia Chanjocovid.moh.go.tz na ukishafanya tu unapokea serial number kwenye simu yako.

Na kwenye documents zako kuna hadi batch Number ambayo inapatikana kwenye kichupa cha chanjo uliyochanja.

Sasa hapo si ndio patam, nna mpanga mchomaji asinichome baada ya hizo taratibu zote. Batch namba atakayoitumia kuniandikishia namwamia aimwage isitumike tena.
 
Chamsingi watu tukachange. Mtu akiamua kitu kukwepa, atakwepa tu.

Nnachosisitiza, watu wapewe elimu ya kutosha. Wenyewe wataenda kuchanja na kuchukua tahadhari.

Wakianza kuweka nguvu kubwa namna hii itaonekana tuna taarifa za wengi kuchanjwa lakini maambukizi yanaongezeka.
 
Kwa Tanzania, kabla hujachanja inabidi ufanye booking kupitia Chanjocovid.moh.go.tz na ukishafanya tu unapokea serial number kwenye simu yako.

Na kwenye documents zako kuna hadi batch Number ambayo inapatikana kwenye kichupa cha chanjo uliyochanja.
Yaani mfumo wa TZ uwe smart kuliko wa Amerika?

TZ hawahangaiki na kadi feki,wao hata alifanya hiyo booking.
Kwenye kuchomwa anahonga achomwe water for injection,hizo serial no.zinabaki Kama ilivyo kawaida.
 
Yaani mfumo wa TZ uwe smart kuliko wa Amerika?

TZ hawahangaiki na kadi feki,wao hata alifanya hiyo booking.
Kwenye kuchomwa anahonga achomwe water for injection,hizo serial no.zinabaki Kama ilivyo kawaida.
Sishani hata kama umeelewa. Nano kasema Marekani wametumia system ?
 
Back
Top Bottom