Marekani yadai ina habari ya orodha wanaopaswa "kuuawa au kupelekwa kambini" Ukraine

Marekani yadai ina habari ya orodha wanaopaswa "kuuawa au kupelekwa kambini" Ukraine

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
1645453064892.png

Marekani imeuonya Umoja wa Mataifa kuwa ina habari kwamba Urusi ina orodha ya raia wa Ukraine wanaopaswa kuuawa ama kuweka kwenye kambi za mateso iwapo uvamizi dhidi ya Ukraine utatokea.

Haya ni kwa mujibu wa barua iliyotumwa kwa Mkuu wa Haki za Binaadamu wa Umoja wa Mataifa, Michelle Bachelet, na nakala yake kupatikana na shirika la habari la AFP. Barua hiyo imesema kwamba Marekani ina taarifa za kuaminika zinazoonyesha kwamba vikosi vya Urusi vinandaa orodha hiyo na wana taarifa pia kuwa vikosi vya Urusi vinaweza kuchukuwa hatua za hatari kutawanya maandamano ya amani au upinzani unaojulikana kutoka kwa raia.

Waraka huo, uliotiwa saini na Bathsheba Nell Crocker, balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa mjini Geneva, unaonya kuwa uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine unaweza kuleta dhuluma kama vile utekaji nyara au mateso, na unaweza kuwalenga wapinzani wa kisiasa na watu wa dini na makabila ya wachache, miongoni mwa mengine. Moscow inakanusha kuwa ina mpango wa kushambulia Ukraine lakini inatafuta hakikisho kwamba Ukraine haitajiunga na NATO.

DW Swahili
 
Kama vipi hivi vita wavibebe waende wakapiganie pale Texas au Wisconsin....

Ni rahisi sana kushabikia vita iwapo vinapiganwa maili za kotosha kutoka kwako na wewe if anything you are bound to profit.....
 
Du! hapo kama ni raia wa Ukraine alafu unakubalika na Warusi, kiwepesi tu unaweza ukalamba uteuzi wa Uraisi maan wakishaichukua nchi lazima wamuweke kibalaka wao
 
Marekani anazidi kumchokonoa Putin; atapata anachotafuta huyo JB
 
Marekani anazidi kumchokonoa Putin; atapata anachotafuta huyo JB

Us sio wakuwakurupukia kindezi mkuu,wejiulize kwanini wao wanaweza kusogelea nchi yoyote na wakaweka kambi karibu na wanaemdhania kuwa aduiyao.
Lakini hakuna nchi hata moja ambayo imejaribu kuweka vikosi vya jeshi karibu na mpaka wa US hata kupitia nchi jirani.

Putin anaujua mziki wa hao jamaa, kinacho mtia hofu kuivamia Ukraine ni marekani tu, hakuna kingine.

Us ana kambi kubwa za jeshi na silaha kali Romania na Poland, sasa Putin ndio maana anaamua kutaka kujitoa muhanga ili kudhibiti hatari mapema, ili Us wasije kuweka kambi na silaha Ukraine na kuwafanya wasilale usingizi.
 
Us sio wakuwakurupukia kindezi mkuu,wejiulize kwanini wao wanaweza kusogelea nchi yoyote na wakaweka kambi karibu na wanaemdhania kuwa aduiyao.
Lakini hakuna nchi hata moja ambayo imejaribu kuweka vikosi vya jeshi karibu na mpaka wa US hata kupitia nchi jirani.

Putin anaujua mziki wa hao jamaa, kinacho mtia hofu kuivamia Ukraine ni marekani tu, hakuna kingine.

Us ana kambi kubwa za jeshi na silaha kali Romania na Poland, sasa Putin ndio maana anaamua kutaka kujitoa muhanga ili kudhibiti hatari mapema, ili Us wasije kuweka kambi na silaha Ukraine na kuwafanya wasilale usingizi.
Lakini Russia iko karibu Sana na Marekani
 
Lakini Russia iko karibu Sana na Marekani

Kutokea wapi.

Kutoka Moscow kuitafuta Alaska sio mchezo,Putin kama anataka kumtia joto babu Bid, labda aweke base Canada na Mexico kitu ambacho hakiwezekani kirahisi.
 
Us sio wakuwakurupukia kindezi mkuu,wejiulize kwanini wao wanaweza kusogelea nchi yoyote na wakaweka kambi karibu na wanaemdhania kuwa aduiyao.
Lakini hakuna nchi hata moja ambayo imejaribu kuweka vikosi vya jeshi karibu na mpaka wa US hata kupitia nchi jirani.

Putin anaujua mziki wa hao jamaa, kinacho mtia hofu kuivamia Ukraine ni marekani tu, hakuna kingine.

Us ana kambi kubwa za jeshi na silaha kali Romania na Poland, sasa Putin ndio maana anaamua kutaka kujitoa muhanga ili kudhibiti hatari mapema, ili Us wasije kuweka kambi na silaha Ukraine na kuwafanya wasilale usingizi.

Don't forget how promptly & severely tiny Fidel Castro's Cuba ^beated^ the uncalled-for infiltration of JFK and his crooked CIA, and Mafia mobs! Bay of Pigs--sounds familiar?
 
Tuone she utu kwa kuyapata hifadhi, tuombe unhcr watupe fedha za kuwakimu
 
Back
Top Bottom