Marekani yakwama kupata sampuli za Mwezi kutokana na Kifungu cha Wolf

Marekani yakwama kupata sampuli za Mwezi kutokana na Kifungu cha Wolf

Yoyo Zhou

Senior Member
Joined
Jun 16, 2020
Posts
126
Reaction score
215
VCG111499936374.png
Hivi karibuni Chombo cha Chang'e No. 6 cha China kilifanikiwa kumaliza kazi yake ya kuchunguza Mwezi na kurejea duniani, na kuleta sampuli ya kwanza duniani ya udongo na mawe kutoka kwenye upande wa mbali wa Mwezi. Baada ya China kutangaza kuwa itashirikiana na jamii ya kimataifa kutafiti sampuli hiyo, Mkuu wa Shirika la Anga za Juu la Marekani (NASA) Bill Nelson alisema wanasayansi wa Marekani wataruhusiwa kuomba kutafiti sampuli hizo, lakini wanatakiwa kuhakikisha kuwa hawakiuki kifungu cha Wolf cha sheria ya nchi hiyo.

Awali, msemaji wa NASA Faith Marco alilalamika kwamba China inashirikiana na Ufaransa, Italia, Pakistani na Shirika la Anga za juu la Ulaya kutekeleza mradi wa kukusanya sampuli kutoka upande wa mbali wa Mwezi, lakini haikuialika NASA kufanya hivyo, na hata sasa haiko tayari kushirikiana na Marekani kutafiti sampuli ya Mwezi.

Kuhusu suala hilo, jibu la Wizara ya Mambo ya Nje ya China limekuwa rahisi na la wazi, China siku zote inapenda kushirikiana na Marekani katika utafiti wa anga za juu, lakini labda Marekani imesahau kifungu chake cha Wolf, ambacho kinapiga marufuku mashirika yoyote ya nchi hiyo kushirikiana na China katika utafiti wa anga za juu. Naye naibu mkuu wa Shirika la Anga za Juu la China Bian Zhigang pia amesema kizuizi kikuu dhidi ya ushirikiano wa China na Marekani katika utafiti wa anga za juu ni Kifungu cha Wolf, kama Marekani ikitaka kushirikiana na China, ni lazima iondoke kizuizi hicho.

Mwaka 1999, Marekani ilitoa ripoti ya Cox, ikidai China “kuiba” teknolojia ya anga za juu ya Marekani, na kuyataka mashirika yake na hata ya nchi nyingine kutoiruhusu China kurusha roketi zao, ili kuzuia maendeleo ya teknolojia ya anga za juu ya China. Baadaye, iliona kwamba hatua hiyo haitoshi, na kuanza kutekeleza Kifungu cha Wolf mwaka 2011, ambacho kilikataza kabisa NASA kufanya mawasiliano na ushirikiano wa aina yoyote na China.

Hata hivyo, hatua hizo ilishindwa kuzuia maendeleo ya sayansi na teknolojia ya anga za juu ya China. Tangu Marekani ianzishe Kifungu cha Wolf, China imetekeleza kwa mafanikio miradi mikubwa mbalimbali ya anga za juu kama vile kujenga kituo cha anga za juu na kuchunguza sayari za Mwezi na Mars. Hivi karibuni chombo cha Chang'e No. 6 kilifika upande mbali wa Mwezi, na kurudi ikichukua sampuli ya huko. Hii ni kazi ya upainia katika historia ya binadamu. Kama ripoti ya CNN ilivyosema, China sasa ina kitu ambacho hakuna mtu mwingine aliyewahi kuwa nacho, yaani sampuli ya mawe na udongo kutoka upande mbali wa Mwezi. Ikilinganishwa na sampuli zilizopatikana zamani kwenye upande wa mbele wa Mwezi, sampuli hiyo ni muhimu kwa binadamu kuelewa muundo wa Mwezi mzima, na hata historia ya mabadiliko ya mfumo wa jua. Bila shaka Marekani inatamani sana sampuli hiyo, lakini inakwamishwa na Kifungu cha Wolf.

Katika miaka ya hivi karibuni, Marekani imezidi kujaribu kuzuia maendeleo ya teknolojia za juu za China, na kuweka vikwazo mbalimbali. Lakini kama teknolojia ya anga za juu, kitendo hicho hakiwezi kuzuia maendeleo ya China hata kidogo, kinyume chake, mara kwa mara Marekani inajidhuru mwenyewe. Ushirikiano huleta mafanikio ya pamoja, huku ubinafsi ukileta hasara. Huu ni ukweli.
 
Kwahio Marekani hakwenda mwezini mwaka 1961 enzi za Armstrong?

udongo hawakuchukua toka enzi hizo?
Marekani wana sample lakini ni za kutoka moon's near side

Ila China ndio limekuwa taifa la kwanza duniani kukusanya sample kutoka moon's far side (eneo la mbali zaidi la mwezi)

Ni eneo ambalo hakuna chombo chochote cha angani kimewahi kufika. Kwa hiyo hakukuwahi kuwa na taarifa zozote za kitafiti kuhusu eneo hilo la mwezi mpaka Chang'e 6 ilipoleta hizo sample ni historic mission

Astronauts huliita eneo hilo mysterious region
 
Kwahio Marekani hakwenda mwezini mwaka 1961 enzi za Armstrong?

udongo hawakuchukua toka enzi hizo?
Kwanza usiwe mvivu wa kujisomea, ungesoma post namba moja yote ungeelewa kilichoandikwa, usiwe mvivu wa kusoma.

Ni mwaka 1969 na Armstrong na wenzake walichukuwa sampuli za mwezini, walichukuwa upande wa mbele wa mwezi, ambao ni upande huu tunaouona tukiwa duniani. Wachina chombo chao kimekwenda kuchukuwa sampuli upande wa nyuma, usioonekana kutokea duniani.

Umeelewa?
 
Back
Top Bottom