Marekani yamfukuza mhusika wa Mauaji ya Kimbari ya Rwanda, aliyemaliza kifungo jela kwa unyanyasaji wa kijinsia Marekani

Marekani yamfukuza mhusika wa Mauaji ya Kimbari ya Rwanda, aliyemaliza kifungo jela kwa unyanyasaji wa kijinsia Marekani

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
04 March 2025
Kigali, Rwanda


Marekani yamfukuza mfungwa wa Mauaji ya Kimbari ya Rwanda Ahmed Napoleon Mbonyunkiza​

2025-03-04

Mamlaka ya Kitaifa ya Mashtaka ya Umma (NPPA) nchini Rwanda mnamo Jumanne, Machi 4, 2025 ilithibitisha kufukuzwa kwa Ahmed Napoleon Mbonyunkiza kutoka Marekani.

Mbonyunkiza, 57, alifukuzwa baada ya kutumikia kifungo cha miaka 15 jela nchini Marekani kwa makosa yanayohusiana na unyanyasaji wa kingono.


View: https://m.youtube.com/watch?v=Y-W52uScpmo
Video : Kigali International Airport March 4,2025 Ahmed Mbonyunkiza akiwasili toka Marekani chini ya escort ya askari


Mnamo 2007, alihukumiwa bila kuwepo mahakamani nchini Rwanda, na Mahakama ya Nyakabanda Gacaca kwa uhusika wake katika Mauaji ya Kimbari ya 1994 dhidi ya Watutsi.


Katika taarifa, NPPA ilipongeza mamlaka za mahakama za Marekani kwa ushirikiano wao katika kuwafukuza wakimbizi waliokimbia mauaji ya halaiki na kujificha nje ya Rwanda.

"NPPA inaipongeza Marekani kwa mchango wao katika mapambano dhidi ya wanaokwepa mkono wa sheria kwa kutoroka Rwanda," ilisema taarifa hiyo.

Kufukuzwa kwa Mbonyunkiza ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za kimataifa za kuwafikisha mbele ya sheria wahusika wote wa mauaji ya kimbari.

1741145650971.jpeg

Kushoto : Napoleon Ahmed Mbonyunkiza

TOKA MAKTABA:
Iowa Sex Offender Registry (.gov)
https://www.iowasexoffender.gov
NAPOLEON MBONYUNKIZA - Iowa Sex Offender Registry

Napoleon Ahmed Mbonyunkiza is a convicted sex offender. Napoleon resides at Polk Co Jail, Ice Hold, Des Moines, Iowa, 50313.
 
Kufukuzwa kwa Mbonyunkiza ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za kimataifa za kuwafikisha mbele ya sheria wahusika wote wa mauaji ya kimbari.
Sir Slim vipi hatajwi?
 
Mbonyunkiza, 57, alifukuzwa baada ya kutumikia kifungo cha miaka 15 jela nchini Marekani kwa makosa yanayohusiana na unyanyasaji wa kingono.
Jela Marekani maisha mserereko kuliko Africa
 
Mwandishi wa hii Habari ni Nani? Imeandikwa hovyo haswa, Inabidi pascal aanzishe chuo kufundisha waandishi kuandika!
Yote tisa.

Itoshe, Pascal ana sakamwa, ana nyanyaswa, ana zodolewa na kudhihakiwa yaani ana pakwa matope yote na maneno mengine mengi-ili aonekane si mwandishi wa kuaminiwa na Umma wa Watanzania.

Hiyo inaogopesha. Na sio hivo tu, ni hatari kwa usalama wa taifa letu.

Hata hivyo, huyo muuaji got what he deserve. Yaani ameua kwao na amebaka Marekani.

.....
 
Yote tisa.

Itoshe, Pascal ana sakamwa, ana nyanyaswa, ana zodolewa na kudhihakiwa yaani ana pakwa matope yote na maneno mengine mengi-ili aonekane si mwandishi wa kuaminiwa na Umma wa Watanzania.

Hiyo inaogopesha. Na sio hivo tu, ni hatari kwa usalama wa taifa letu.

Hata hivyo, huyo muuaji got what he deserve. Yaani ameua kwao na amebaka Marekani.

.....

Pascal ni rafiki yangu na ninamjua kuliko wewe, ana uwezo mkubwa na akili sana, ila kinachouma ameamua kuweka akili pembeni na kussupport ujinga wa Ccm regardless the cost!
 
Pascal ni rafiki yangu na ninamjua kuliko wewe, ana uwezo mkubwa na akili sana, ila kinachouma ameamua kuweka akili pembeni na kussupport ujinga wa Ccm regardless the cost!
Aha. Kwahiyo swali na nasaha yako ilikuwa ni ya kinafiki, yani ulikuwa unakejeli?

Ok.🤭 Nimekuelewa.
 
Duh; unatoka kutumikia miaka 15 jela Marekani; unafukuzwa mara baada ya kifungo chini ya ulinzi mkali hadi Rwanda; unapokelewa na polisi pingu mkononi moja kwa moja Central ndani gari maalumu then mahabusu ukisubiri kupelekwa mahakamani. Balaa hili!
 
Back
Top Bottom