Marekani yatakiwa kupunguza upimaji COVID19

Marekani yatakiwa kupunguza upimaji COVID19

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Wakati huo huo, Rais wa Marekani, Donald Trump amewataka maafisa wa afya kupunguza kasi ya kuwapima watu virusi vya corona. Akizungumza katika wa kuzinduliwa kwa kampeni yake kuwania kuchaguliwa tena kwenye uchaguzi wa Novemba, Trump amesema maafisa wa afya waachane na mpango huo kwani unasababisha kuongezeka kwa idadi kubwa ya visa vya maambukizi.

''Unapowapima watu kwa wingi, utabaini watu wengi zaidi wameambukizwa. Hivyo nawaambia watu wangu, tafadhali punguzeni kasi ya upimaji wa COVID-19. nyie mnapima nakupima tu,'' alisema Trump. Aidha, Trump ameongeza kusema kuwa Marekani imewapima watu milioni 25 virusi vya corona.

Nako nchini Iran, shirika la habari la Iran, Isna limeripoti kuwa Waziri wa Afya Saeed Namaki amesema mripuko wa virusi vya corona utaendelea hdi 2022. Namaki amesema kulingana na makadirio rasmi, wananchi wa Iran itabidi waishi na virusi vya corona kwa miaka mingine miwili.

Iran inakabiliwa na mripuko mbaya wa COVID-19 katika eneo la Mashariki ya Kati, huku kukiwa na uvumi kuhusu takwimu rasmi za waathirika pamoja na maafisa wa ngazi ya juu wa serikali ambao wanaugua na kufariki kutokana na virusi hivyo.


DW Swahili
 
Huyu Trump ni chizi hana tafauti kubwa na chizi mgine.......kwani kama hataki wapime kwanini amenunua testing kites 100m
 
Anachoongea ndio ukweli wenyewe mnapima tu mnapima tu halafu hakuna tiba nini maana yake zaidi ya kujengana hofu tu.
 
Hapo wanashindwa tuu kusema waz kwamba hebu tuungane na komando Magufuli...manake naona yoote wanayoyafanya kwa sasa ni yale watu walikuwa wanambeza Magufuli
 
Huyu Trump ni chizi hana tafauti kubwa na chizi mgine.......kwani kama hataki wapime kwanini amenunua testing kites 100m

Aliyetoa hela ni wewe au yeye fikiria halafu utajua yupi chizi kati yenu[emoji23]
 
Unapima na baada ya kupima unawaambiaje?
Ukimwi tunapimwa kwa sababu tunashauriwa kuishi na matumaini, halafu na matumizi sahihi ya dawa za kufubaza. Korona ukipima na kukutwa nayo watakushauri nini?
Magufuri anachofanya ni sahihi, anajaribu kuwajenga kisaikolojia, kwamba hatuwezi kujifungia ndani, lazima maisha yaendelee. Lakini lililokubwa zaidi ni kuchukua tahadhari. Katika tahadhari, la msingi ni kuimarisha kinga ya mtu mmoja mmoja.
 
Back
Top Bottom