Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Wakati huo huo, Rais wa Marekani, Donald Trump amewataka maafisa wa afya kupunguza kasi ya kuwapima watu virusi vya corona. Akizungumza katika wa kuzinduliwa kwa kampeni yake kuwania kuchaguliwa tena kwenye uchaguzi wa Novemba, Trump amesema maafisa wa afya waachane na mpango huo kwani unasababisha kuongezeka kwa idadi kubwa ya visa vya maambukizi.
''Unapowapima watu kwa wingi, utabaini watu wengi zaidi wameambukizwa. Hivyo nawaambia watu wangu, tafadhali punguzeni kasi ya upimaji wa COVID-19. nyie mnapima nakupima tu,'' alisema Trump. Aidha, Trump ameongeza kusema kuwa Marekani imewapima watu milioni 25 virusi vya corona.
Nako nchini Iran, shirika la habari la Iran, Isna limeripoti kuwa Waziri wa Afya Saeed Namaki amesema mripuko wa virusi vya corona utaendelea hdi 2022. Namaki amesema kulingana na makadirio rasmi, wananchi wa Iran itabidi waishi na virusi vya corona kwa miaka mingine miwili.
Iran inakabiliwa na mripuko mbaya wa COVID-19 katika eneo la Mashariki ya Kati, huku kukiwa na uvumi kuhusu takwimu rasmi za waathirika pamoja na maafisa wa ngazi ya juu wa serikali ambao wanaugua na kufariki kutokana na virusi hivyo.
DW Swahili
''Unapowapima watu kwa wingi, utabaini watu wengi zaidi wameambukizwa. Hivyo nawaambia watu wangu, tafadhali punguzeni kasi ya upimaji wa COVID-19. nyie mnapima nakupima tu,'' alisema Trump. Aidha, Trump ameongeza kusema kuwa Marekani imewapima watu milioni 25 virusi vya corona.
Nako nchini Iran, shirika la habari la Iran, Isna limeripoti kuwa Waziri wa Afya Saeed Namaki amesema mripuko wa virusi vya corona utaendelea hdi 2022. Namaki amesema kulingana na makadirio rasmi, wananchi wa Iran itabidi waishi na virusi vya corona kwa miaka mingine miwili.
Iran inakabiliwa na mripuko mbaya wa COVID-19 katika eneo la Mashariki ya Kati, huku kukiwa na uvumi kuhusu takwimu rasmi za waathirika pamoja na maafisa wa ngazi ya juu wa serikali ambao wanaugua na kufariki kutokana na virusi hivyo.
DW Swahili