Marekani yatangaza vikwazo vya viza dhidi ya Maofisa wa Somalia

Marekani yatangaza vikwazo vya viza dhidi ya Maofisa wa Somalia

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Marekani imetangaza vikwazo vya viza dhidi ya maafisa wa sasa au wa zamani wa Somalia wanaotuhumiwa kuhujumu michakato ya kidemokrasia.

Hatua hiyo inakuja wakati ambapo Marekani inasukuma kufanyika kwa uchaguzi wa kuaminika nchini Somalia - ambao umechelewa kwa muda mrefu.

Katika taarifa, Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken alisema vizuizi vya visa vinatumika kwa watu “ambao wameshindwa kutekeleza majukumu yao ya kutekeleza uchaguzi kwa wakati na wazi“.

Pia vinalenga maafisa ambao “wamewalenga waandishi wa habari na wanachama wa vyama vya upinzani kwa unyanyasaji, vitisho, kukamatwa na vurugu“.

Somalia imeahirisha uchaguzi tangu mamlaka ya Rais Mohamed Abdullahi Farmajo yalipokamilika Februari mwaka jana.


Chanzo: Star TV
 
ndio njia pekeee alobakia nayo paper tiger maskini[emoji16][emoji23][emoji2]
 
Back
Top Bottom