Marvel Cinematic Universe special thread

"You mess with time, it tends to mess back."


Tony Stark, Avenger endgame
 
The thing ni kwamba hao wote watakaokuja kwenye Timeline ya Multiverse of madness wote watakua Variants maana wanetoka kwenye timelines zs dunia yao. Ndio najiuliza je wataweza kubaki forever Kwenye timeline hii su watarudi walipotoka. Lakini pia TVA wataruhu hilo???

Mazee si mnajua Marvel studios wamebadirisha date release Ant-Man 3 itatoka feb na The marvel july. Maana yake hapo kati Kati itatoka Loki S2 na ndio tutapata majibu yote ya mambo yaliyotokea kwenye Multiverse of madness.

Ooooh sasa nimekua excited na series ya Loki kuliko hata muvi zingine 😉

I can't wait I can't wait
Kwani Charles Xavier bado yupo hai??

Keyword = Multverse

"You mess with time, it tends to mess back."


Tony Stark, Avenger endgame
 
Naomba kesho ionyeshwe watupe ile preview(watch before the world)

I cant wait ndg zang naona masaa mawili machache😀
 
Nimeona end credit scenes ya strange


Itakuua hatari


Strange Ana macho matatu


Nadhani DS3 tutakuwa na dormamu
Ndio umegundua leo?? Hukuona viclip vya nyuma walivyokua wanapost Marvel Studios? Mimi nimemuona Charlize theron akiwa kama Clea.
Theories zangu nyingi zimekuja kua kweli

Strange Supreme ndio ana macho matatu as shown in what if..
 
Huku mwishoni sijaelewa yani episode ya 5
Mate, sorry kwa kuchelewa kukujibu nilikua nasubiri Ep6 itoke kwanza. Ila sitakuhadithia from Ep 1


Ipo hivi
Baada ya Marc kupigwa risasi ep4 akadumbukia kwenye maji alijikuta yupo kwenye eneo la kufikirika ambapo yeye inaonekana ni mgonjwa wa hospital. Sasa katika juhudi za kutoroka ndio akagundua kwamba Marc na Steve wapo katika miili tofauti kama mapacha wakakumbatiana baadae akatokea yule kiboko Tawareet Ep 4 ikaisha.

Ep 5 ikagundulika ile hospital walimo ni boat ambayo ipo kuzimu inawasafirisha kwenda kwenye geti la Osrisi ambapo huko wanapimwa mioyo yao kutokana na matendo yao ili kama muzani ukibalnce waende Peponi(Field of Reeds) lakini muzani haubalansi kwakua kuna kumbukumbu kati yao hazipo sawa. Ndio pale tunaona sasa wakiwa wadogo.

Marc akiwa mdogo alikua anateswa na mama yake ajili ya mateso hayo bila kujua akamtengeneza Steve. So steve alikua hateswi na mama yake ili Marc ndio alikua anateswa ndio maana alikua anampigia simu mara nyingi japo alikua kashakufa. (Steve alikua anajua mama yake ni mzuri coz kila mama yake akitaka kumpiga marc alikua anachukua Control ya mwili anapigwa yeye)


So katika harakati za kuingia Peponi Steve anaangukia Kwenye eneo la wafu/kuzimu anabadirika kua mchanga hakafu marc anafanikiwa kuingia Peponi.

Ep6 Steve aliokolewa, well I don't want to spoil it for you. Utatazama. Kama hujaelewa pia uliza
 
Msaada lads, kati ya what if na Loki niangalie ipi? Maana kuna vitu navimiss kabisa mcu kama miendelezo inazidi kutoka hivyo.
 
Y'all I'm sooooooooooo disappointed.
I can't believe, I won't spoil it for you but The whole movie is about Wanda😢😢😢
 
Msaada lads, kati ya what if na Loki niangalie ipi? Maana kuna vitu navimiss kabisa mcu kama miendelezo inazidi kutoka hivyo.
Angalia zote ila anza na LOKI. Series ya Loki itakufungulia uelewa kwenye WHAT IF.
 
Maoni:

Hakuna character yeyote in MCU atapewa heshima kama ilivyopewa character ya Ironman ya RDJ.

Tangu Marvel wamemu-introduce kwa cinema mpaka kui-ua, character imeendeshwa kiprofeshno sana.

#TEAMMARVEL
 
Nieleweshe hapo kwenye Marc alimtengeneza vipi Steve??? Na ikawaje huyu akawa M british anaendesha maisha yake mbali na mwingie M Marekani anaendesha maisha yake kwingine kama walikua ni mwili mmoja???

Hapo kiukweli wamenichanganya sana tho nimeangalia episodes zote
 
Kwl mm mwenyw apa nashindwa kuelewa
 
Duuuh ntajitahidi siku moja niende hapo Aura nikajionee mwenyewe mmepamwagia misifa Duuuh maana me chaka langu ni MC.
 
N
Movie ishakuwa spoiled kitambo nikiingia YouTube nakutana na cutscenes mbalimbali
Ndio maana nimekataa kutumia YouTube hii week hata nikikuta final trailer siangaliii maana hizo final trailers haziishi.

Movie ikiwa mbaya Marvel watakuwa wamenivunja moyo degree ya kuvunjwa moyo kimapenzi
 
Marc anaugonjwa wa akili, unaitwa dissociative identity disorder. Ilikuwaje akawa nao,

*kutokana na kifo cha mdogo wake, mama yake marc akawa anamlaumu marc kwamba ndio sababu ya mdogo wake kufa. Mama'ke akapunguza mapenzi kwake na akawa anampiga piga kwa sababu ndogo sana.

*Kiafya/tiba zaidi, inafahamika kwamba ubongo wetu unaweza ku-process matukio tofauti sana, ikiwamo ikihitaji kukulinda wewe muhusika mwenyewe, unaweza kupoteza kumbukumbu muhimu sana, au ukatengeneza kumbukumbu mpya ambazo haujawahi kuzipitia kabisa, lakini ubongo wako ukakutaarifu kuwa hizo kumbukumbu mpya ndio uhalisia wenyewe.

*kuna scene inamuonesha marc alikimbilia chumbani baada ya mama yake kuanza kuwa mkali bila sababu, pale chumbani ukutani kulikuwa na jariba limebandikwa, jarida lile ukiliangalia lina picha ya mtu , the jina la huyo mtu ni "Steven Grant", mtu mashuhuri wa kuvumbua mambo ya kale, hasa hasa ya watu wa misri(yaani explorer).

Sasa, ubongo wa marc ukataka kumlinda "mtoto marc" kutokana na manyanyaso aliyokuwa anayapitia kutoka kwa mama yake, ndio hapo ukaunda kumbukumbu mtu (tuseme personality) mpya kabisa ambayo ndio hiyo "steven grant". Bila shaka huyo steven grant(wa kwenye jarida, alikuwa anatokea uingereza na kuongea lafudhi ya uingereza, wakati marc anaongea lafudhi ya kimarekani).
Pia sababu steven grant wa kwenye jarida ni "explorer" wa mambo ya zamani hasa hasa ya watu wa misri, ndo hiyo inamfanya alter ego ya marc spencer(yaani steven grant wa marc spencer) kuwa mjuaji sana wa mambo ya wamisri na hadithi zao za kale..

Kwa hivyo basi, sio kwamba yeye Marc Spencer ndo alimtengeneza Steven Grant kwa hiari yake, hapana, ni ubongo wake katika jitihada za kumuokoa kutokana na kile alichokuwa anapitia kutoka kwa mama yake wakati wa utoto.
 
Nilitaka nianze kueleza naona kuna mtu kanisadia but mm nitaelezea upande wa reality

Dissociative Identity Disorder au Multiple Personality Disorder ni ugonjwa wa akili ambao mgonjwa ana personality zaidi ya moja. Mara nyingi mtu mwenye tatizo hili hua anasumbulia na upotezaji wa kumbukumbu. Mtu anaweza kua na jina na characteristics fulani lakini pia Identity yake nyingine inakua na jina na sifa zake. So kama personality fulani ikiwa On basi ile nyingine inapoteza kumbukumbu. Ikirudi inashangaa imefika vipi hapa alipo.

Tafiti zinasema kua karibia 2% ya wagonjwa wa akili wanakua wana tatizo hili na halina tiba. Mara nyingi humtokea mtu aliyekua abused utotoni

Kwa kuelewa zaidi Tafuta muvi inaitwa Glass ya 2019 kacheza James Mcavoy utajifunza zaidi
Sawa nimekuelewa pia hii kwa kibinadamu inawezekana au ni movie tu, mfano hivyo alivyokuwa anajibadirisha mara kuwa marc mara steve


Kwl mm mwenyw apa nashindwa kuelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…