Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,681
- 8,887
Pastor Masanja akiwa kwenye kipindi kwenye redio ya EFM ameipongeza TRA kuongeza makusanyo kwa 14.5% kufikia trilioni 27.64 kwa mwaka wa fedha 2023/24 lakini amesikitishwa na uamuzi wa Serikali kupunguza faini ya kutotoa risiti ya EFD kwa wafanyabiashara kutoka milioni 15 mpaka milioni 4.
Masanja amesema Serikali haitaki wafanyabiashara walipe faini, amewasihi kufanya biashara kihalali wasikutane na faini.
Masanja amesema wanapolalamika faini kubwa na kutaka faini ndogo inamaanisha wanataka kuendelea kufanya makosa.
Masanja amehoji kwanini mtu apunguziwe adhabu ya kosa ambalo bado hajafanya.
Masanja amesema Serikali haitaki wafanyabiashara walipe faini, amewasihi kufanya biashara kihalali wasikutane na faini.
Masanja amesema wanapolalamika faini kubwa na kutaka faini ndogo inamaanisha wanataka kuendelea kufanya makosa.
Masanja amehoji kwanini mtu apunguziwe adhabu ya kosa ambalo bado hajafanya.