Masasi ya Geofrey Mwambe ni bambam

Masasi ya Geofrey Mwambe ni bambam

Mohamed Ismail

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2014
Posts
224
Reaction score
236
Anaandika Mo Mlimwengu.

Historia hutusaidia kujua tulipotoka, tulipo na tunapoenda. Mh Geofrey Mwambe Mbunge wa Masasi Mjini anazidi kujipambanua kiutendaji namna ambavyo anajitahidi kusukuma maendeleo kwenye jimbo lake.

Binadamu tumeumbwa kusahau na kuna wakati mtu akifanya mazuri tunaona ni kama wajibu wake. Wana Masasi wamezoea kuyaona mazuri yanayofanywa na Mwambe hivyo wanaweza kuyachukulia kawaida na kuona kama ndio wajibu wake. Tukisema ukweli Mwambe anahitaji kupongezwa kutokana na umahiri wake wa kutatua matatizo ndani ya Masasi.

Mwenye masikio atasikia na mwenye macho ataona kwa kasi ambayo anaitumia kwenye kuleta maendeleo. Mwambe kaamua anahakikisha kuboresha ustawi wa jamii wa Masasi . Ni Mwambe huyu huyu ambaye juzi tulishuhudia akigawa magari matatu kwenye shule za sekondari za Marika ,Sululu na Temeke. Lengo mahsusi ni kutoa motisha kwa walimu na hii itasaidia kuleta matokeo chanya kwa wanafunzi.

Jamii ya watu wa kusini kilio kikubwa ni kutokuwa na elimu lakini unaona ambavyo Mwambe kaamua kulivalia njuga suala la elimu. Amekuwa akitumia nafasi yake ya ubunge kushawishi taasisi kusaidia suala la elimu. Tumeona ambavyo amekuwa akivutia taasisi kibao kama NMB, Vodacom kutoa ufadhili kwenye masuala ya elimu na afya.

Kwa Masasi tunaweza kusema Mwambe amekuwa game changer, ni mwanasiasa ambaye siasa zake kazielekeza kwenye utendaji zaidi kuliko kuzungumza tu kama ilivyozoeleka. Leo hii waislamu wa Masasi wanajivunia kuwa na Mwambe kwa kitendo cha kuhakikisha anafanikisha kupata mfadhili wa kuwajengea msikiti ambapo gharama yake ilikuwa milioni 500. Lakini ushawishi wake na moyo wake alifanikisha kumpata Bakhresa kufanya ufadhili huo. Mwambe kaamua kutumia akili na nguvu zake kuwapambania wana Masasi. Leo hii ndani ya Masasi kuna mabadiliko makubwa sasa hivi barabara nyingi zimejengwa kwa kiwango cha lami na huku vijijini barabara zinazidi kuboreshwa. Serikali ya awamu ya sita ya Mh Samia Suluhu Hassan imempata mwakilishi mzuri ndani ya Masasi mjini.

Huduma za kijamii zinazidi kuboreshwa ,zahanati zinajengwa. Hospitali ya Mkomaindo tumeshuhudia ikipokea vifaa tiba vya thamani ya mamilioni ambavyo vinasaidia kutoa huduma kwa ufasaha. Hospitali inaboreshwa na huku huduma ambazo awali zilikuwa hazitolewi zimeanza kutolewa baada ya Mwambe kuchukua jimbo.

Tumeona namna ambavyo amewatua ndoo wakina mama kwenye suala la maji. Kitongoji cha Ipiho Kata ya Marika kwa sasa wana maji ya kutosha ambapo ilikuwa haijawahi kutokea. Ukienda kijiji cha Chakama kata ya Matawale nako umejengwa mradi mkubwa wa maji kwa kushirikiana na Ruwasa ambao utasaidia wananchi kufaidika na maji. Suala la maji kilikuwa ni kilio cha muda mrefu lakini kwa sasa wananchi wananufaika na matunda ya serikali ya awamu yao ya sita.

Mwambe amekuwa tafsiri halisi ya kiongozi ndani ya Masasi. Akiahidi anatekeleza na amekuwa kiongozi mzuri wa kutatua yale ambayo miaka yote yalishindwa kutatuliwa. Na ni kiongozi ambaye anahakikisha kila sekta inafanya kazi vizuri. Amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha wakulima wa mikoa ya kusini wananufaika na zao la Korosho lakini mbali na hilo hata kwenye michezo amekuwa mstari wa mbele. Tuliona namna ambavyo amejitolea kuisaidia timu ya Mkuti Market Fc kwa vifaa vya michezo na gharama nyingine walipochukua ubingwa wa mkoa. Kwa sasa Mh Geofrey Mwambe amekuwa nembo halisi ya wana Masasi kutokana na kazi ambazo anazifanya kwenye jimbo lake.

Kwa hii miaka miwili ya ubunge wake ndani ya Masasi kashafanya vitu vingi. Kwa kasi hii baada ya miaka mitano tunaiona Masasi kama Dubai kama alivyosema awali wakati anachukua kijiti cha ubunge. Wana Masasi kwa Mwambe walilamba dume na hii itapelelekea Masasi kukimbia zaidi kimaendeleo.

1 NOVEMBER 2022


1667285920765.jpg
1667285890105.jpg
 
Mhe Geoffrey Mwambe Ni Mbunge wa viwango vikubwa sanaa Ana Busara, Hekima, Mzalendo wa kweli, Msomi, Mbobevu katika masuala ya Uwekezaji na uchumi hakika hiii ni Tunu ya taifa letu ni hazina kweli kweli anaifanya Masasi yetu kua Juu na hakika ni fahari yetu[emoji1488][emoji1488]
 
Kweli mahaba ni ukichaa unaweza ita chongo kengeza.

Mwambe huyu huyu ambaye leo hii wana masasi wanalia na bei mbaya ya korosho..zao la korosho linaenda kumfia mikononi wakulima wanaenda kuangukia kwenye janga la umasikini hakuna wakuwasemea.

Barabara zinazojengwa ni barabara za mjini tu nazo ni chache sana..barbara temeke hola..barabra ya mbonde kwenda namkungwi hola na zingine nyingi kama ya nyasa kwenye vijiji vya tukaewote chakama barabara mbovu balaa.

Soko kuu mkuti nalo ni majanga matupu.
Stendi hakuna nalo ni janga..

Hali ya usafi wa mji wa masasi nalo janga mji wote hauna gari za kuzoa takataka kupeleka dampo.

Kuhusu ujenzi wa vituo vya afya na hospitali tunampongeza kwa kuendelea kutia nguvu..ila afahamu bado maeneo mengi ndani ya mji wa masasi na wananchi kwa ujumla yanahitaji kuangaliwa na kusimamiwa vizr kwa maendeleo ya wana masasi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kwa Wana Masasi Mjini, Masasi, Mtwara na Kusini kwa ujumla, Mheshimiwa Geoffrey Idelphonce Mwambe(MB) ni tunu na lulu halisi.

Uzalendo na upendo wake kwa Wana Masasi Mjini ni kiashiria tosha kwamba anawahitaji sana Wana Masasi Mjini wamuunge mkono kutokana na dhamira njema aliyonayo ya kuijenga Masasi Mjini mpya ya maendeleo.

Ameamua kujipambanua kwamba yeye ni kiongozi wa namna gani. Wananchi wamjue kwamba yeye ni mwakilishi wa namna gani. Hii ni njia sahihi ya kuiambia jamii kwamba wewe ni wa aina gani ili wao wakupime kama wamepatia ama hawajapatia

Anaingia kwenye kundi la viongozi wengine wachache wa Kusini ambao waliishi maisha ya uongozi wao kwa sura hii.

Mheshimiwa Geoffrey Idelphonce Mwambe(MB) anaingia kwenye kundi la Hayati Mzee Benjamin William Mkapa, Hayati Mzee Lawi Sijaona Nangwanda, Hayati Dr Alex Halid Mtavala, Marehemu Ng'itu na wengine ambao sikuwataja hapa(nimewataja ambao ninaweza kuwaelezea angalau kwa machache ninayoyajua).

Hii ni fahari kwa Kusini na taifa letu. Jukumu letu ni kumuombea, kumpa ushirikiano na kumuunga mkono katika kila hatua ya utendaji na uwakilishi wake.

Ni wazi kwamba, kwa utendaji wa aina hii, lazima atajitengenezea maadui aidha kwa sababu ya chuki ama kwa sababu ya kuona anawatengenezea mgogoro na wananchi wao. Hili ni la kwetu, ili kila hatua atakayokuwa anaikanyaga awe salama dhidi ya chuki na husda za wanadamu wasiomtakia mema na wasioitakia mema Masasi Mjini na Kusini kwa ujumla.

MwenyeziMungu aendelee kumsimamia na kumuongoza kwenye majukumu yake ya kila siku(ya kwake binafsi na ya umma kama mwakilishi) ili aweze kuwakomboa Wana Masasi Mjini na Wana Kusini wote wanaopenda maendeleo.

Bravo Mheshimiwa Geoffrey Idelphonce Mwambe (MB).
 
Mhe Geoffrey Mwambe Ni Mbunge wa viwango vikubwa sanaa Ana Busara, Hekima, Mzalendo wa kweli, Msomi, Mbobevu katika masuala ya Uwekezaji na uchumi hakika hiii ni Tunu ya taifa letu ni hazina kweli kweli anaifanya Masasi yetu kua Juu na hakika ni fahari yetu[emoji1488][emoji1488]
Ni kweli ila kwenye neno uzalendo inatia ukakasi kweli kweli!
 
Kweli mahaba ni ukichaa unaweza ita chongo kengeza.

Mwambe huyu huyu ambaye leo hii wana masasi wanalia na bei mbaya ya korosho..zao la korosho linaenda kumfia mikononi wakulima wanaenda kuangukia kwenye janga la umasikini hakuna wakuwasemea.

Barabara zinazojengwa ni barabara za mjini tu nazo ni chache sana..barbara temeke hola..barabra ya mbonde kwenda namkungwi hola na zingine nyingi kama ya nyasa kwenye vijiji vya tukaewote chakama barabara mbovu balaa.

Soko kuu mkuti nalo ni majanga matupu.
Stendi hakuna nalo ni janga..

Hali ya usafi wa mji wa masasi nalo janga mji wote hauna gari za kuzoa takataka kupeleka dampo.

Kuhusu ujenzi wa vituo vya afya na hospitali tunampongeza kwa kuendelea kutia nguvu..ila afahamu bado maeneo mengi ndani ya mji wa masasi na wananchi kwa ujumla yanahitaji kuangaliwa na kusimamiwa vizr kwa maendeleo ya wana masasi.

#MaendeleoHayanaChama
nanukuu maneno ya mwisho kabisa " #maendeleoHayanaChama"
 
niliwahi kutana nae akiwa mtumishi wa BOT na Baadae wizara ya afrika mashariki alikuwa vizuri sana kwenye kujenga hoja... Sijui nani alimdanganya aingie kwenye siasa..... kwa CCM hii ya sasa hatoboi ,ni mmoja ya vijana watiifu wa mwenda zake
 
niliwahi kutana nae akiwa mtumishi wa BOT na Baadae wizara ya afrika mashariki alikuwa vizuri sana kwenye kujenga hoja... Sijui nani alimdanganya aingie kwenye siasa..... kwa CCM hii ya sasa hatoboi ,ni mmoja ya vijana watiifu wa mwenda zake
Hilo Ni jembe kweli kweli na sio kudanganywa kuna wakati unatakiwa kupata wasaa wa kuwahudumia na wengine katika eneo lako ndicho alichofanya kaenda kusaidia nyumbani na kazi zinakwenda vizuri sanaa huku wananchii wa jimbo la masasi wakiona kama alichelewa kua mbunge wao , Kongele Mzee Geoffrey Mwambe kwa kuamua kurudi nyumbani na kua Mtumishi wetu[emoji1488][emoji1488][emoji1488]
 
Kweli mahaba ni ukichaa unaweza ita chongo kengeza.

Mwambe huyu huyu ambaye leo hii wana masasi wanalia na bei mbaya ya korosho..zao la korosho linaenda kumfia mikononi wakulima wanaenda kuangukia kwenye janga la umasikini hakuna wakuwasemea.

Barabara zinazojengwa ni barabara za mjini tu nazo ni chache sana..barbara temeke hola..barabra ya mbonde kwenda namkungwi hola na zingine nyingi kama ya nyasa kwenye vijiji vya tukaewote chakama barabara mbovu balaa.

Soko kuu mkuti nalo ni majanga matupu.
Stendi hakuna nalo ni janga..

Hali ya usafi wa mji wa masasi nalo janga mji wote hauna gari za kuzoa takataka kupeleka dampo.
Huko kwenu Masasi hakuna wakurugenzi wa halmashauri kila kitu anafanya mbunge?

Musimuangushie majukumu ambayo hata siyo yake, yeye atasaidia kusukuma gurudumu na wengine watekeleze majukumu yao.
 
Anaandika Mo Mlimwengu.

Historia hutusaidia kujua tulipotoka, tulipo na tunapoenda. Mh Geofrey Mwambe Mbunge wa Masasi Mjini anazidi kujipambanua kiutendaji namna ambavyo anajitahidi kusukuma maendeleo kwenye jimbo lake.

Binadamu tumeumbwa kusahau na kuna wakati mtu akifanya mazuri tunaona ni kama wajibu wake. Wana Masasi wamezoea kuyaona mazuri yanayofanywa na Mwambe hivyo wanaweza kuyachukulia kawaida na kuona kama ndio wajibu wake. Tukisema ukweli Mwambe anahitaji kupongezwa kutokana na umahiri wake wa kutatua matatizo ndani ya Masasi.

Mwenye masikio atasikia na mwenye macho ataona kwa kasi ambayo anaitumia kwenye kuleta maendeleo. Mwambe kaamua anahakikisha kuboresha ustawi wa jamii wa Masasi . Ni Mwambe huyu huyu ambaye juzi tulishuhudia akigawa magari matatu kwenye shule za sekondari za Marika ,Sululu na Temeke. Lengo mahsusi ni kutoa motisha kwa walimu na hii itasaidia kuleta matokeo chanya kwa wanafunzi.

Jamii ya watu wa kusini kilio kikubwa ni kutokuwa na elimu lakini unaona ambavyo Mwambe kaamua kulivalia njuga suala la elimu. Amekuwa akitumia nafasi yake ya ubunge kushawishi taasisi kusaidia suala la elimu. Tumeona ambavyo amekuwa akivutia taasisi kibao kama NMB, Vodacom kutoa ufadhili kwenye masuala ya elimu na afya.

Kwa Masasi tunaweza kusema Mwambe amekuwa game changer, ni mwanasiasa ambaye siasa zake kazielekeza kwenye utendaji zaidi kuliko kuzungumza tu kama ilivyozoeleka. Leo hii waislamu wa Masasi wanajivunia kuwa na Mwambe kwa kitendo cha kuhakikisha anafanikisha kupata mfadhili wa kuwajengea msikiti ambapo gharama yake ilikuwa milioni 500. Lakini ushawishi wake na moyo wake alifanikisha kumpata Bakhresa kufanya ufadhili huo. Mwambe kaamua kutumia akili na nguvu zake kuwapambania wana Masasi. Leo hii ndani ya Masasi kuna mabadiliko makubwa sasa hivi barabara nyingi zimejengwa kwa kiwango cha lami na huku vijijini barabara zinazidi kuboreshwa. Serikali ya awamu ya sita ya Mh Samia Suluhu Hassan imempata mwakilishi mzuri ndani ya Masasi mjini.

Huduma za kijamii zinazidi kuboreshwa ,zahanati zinajengwa. Hospitali ya Mkomaindo tumeshuhudia ikipokea vifaa tiba vya thamani ya mamilioni ambavyo vinasaidia kutoa huduma kwa ufasaha. Hospitali inaboreshwa na huku huduma ambazo awali zilikuwa hazitolewi zimeanza kutolewa baada ya Mwambe kuchukua jimbo.

Tumeona namna ambavyo amewatua ndoo wakina mama kwenye suala la maji. Kitongoji cha Ipiho Kata ya Marika kwa sasa wana maji ya kutosha ambapo ilikuwa haijawahi kutokea. Ukienda kijiji cha Chakama kata ya Matawale nako umejengwa mradi mkubwa wa maji kwa kushirikiana na Ruwasa ambao utasaidia wananchi kufaidika na maji. Suala la maji kilikuwa ni kilio cha muda mrefu lakini kwa sasa wananchi wananufaika na matunda ya serikali ya awamu yao ya sita.

Mwambe amekuwa tafsiri halisi ya kiongozi ndani ya Masasi. Akiahidi anatekeleza na amekuwa kiongozi mzuri wa kutatua yale ambayo miaka yote yalishindwa kutatuliwa. Na ni kiongozi ambaye anahakikisha kila sekta inafanya kazi vizuri. Amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha wakulima wa mikoa ya kusini wananufaika na zao la Korosho lakini mbali na hilo hata kwenye michezo amekuwa mstari wa mbele. Tuliona namna ambavyo amejitolea kuisaidia timu ya Mkuti Market Fc kwa vifaa vya michezo na gharama nyingine walipochukua ubingwa wa mkoa. Kwa sasa Mh Geofrey Mwambe amekuwa nembo halisi ya wana Masasi kutokana na kazi ambazo anazifanya kwenye jimbo lake.

Kwa hii miaka miwili ya ubunge wake ndani ya Masasi kashafanya vitu vingi. Kwa kasi hii baada ya miaka mitano tunaiona Masasi kama Dubai kama alivyosema awali wakati anachukua kijiti cha ubunge. Wana Masasi kwa Mwambe walilamba dume na hii itapelelekea Masasi kukimbia zaidi kimaendeleo.

1 NOVEMBER 2022


View attachment 2403696View attachment 2403697
Umeandika ujinga wa kiwango cha SGR yaani barabara kuwekwa lami ni fedha za mbunge?
Hospital kupata vifaa tiba ni fedha za mbunge?

Kwahiyo shule kupewa msaada wa magari hiyo ndiyo dawa ya kufaulisha wanafunzi?

Unataka kutuaminisha kuwa wanafunzi wanafundiswa kuendesha magari?

Wacha bhangi za kuvutia chooni.
 
Mhe Geoffrey Mwambe Ni Mbunge wa viwango vikubwa sanaa Ana Busara, Hekima, Mzalendo wa kweli, Msomi, Mbobevu katika masuala ya Uwekezaji na uchumi hakika hiii ni Tunu ya taifa letu ni hazina kweli kweli anaifanya Masasi yetu kua Juu na hakika ni fahari yetu[emoji1488][emoji1488]
Hakuna chochote kipya alichokifanya zaidi ya nyinyi waramba asali kuamua kuwadanganya wadanganyika wa masasi.
 
Kweli mahaba ni ukichaa unaweza ita chongo kengeza.

Mwambe huyu huyu ambaye leo hii wana masasi wanalia na bei mbaya ya korosho..zao la korosho linaenda kumfia mikononi wakulima wanaenda kuangukia kwenye janga la umasikini hakuna wakuwasemea.

Barabara zinazojengwa ni barabara za mjini tu nazo ni chache sana..barbara temeke hola..barabra ya mbonde kwenda namkungwi hola na zingine nyingi kama ya nyasa kwenye vijiji vya tukaewote chakama barabara mbovu balaa.

Soko kuu mkuti nalo ni majanga matupu.
Stendi hakuna nalo ni janga..

Hali ya usafi wa mji wa masasi nalo janga mji wote hauna gari za kuzoa takataka kupeleka dampo.

Kuhusu ujenzi wa vituo vya afya na hospitali tunampongeza kwa kuendelea kutia nguvu..ila afahamu bado maeneo mengi ndani ya mji wa masasi na wananchi kwa ujumla yanahitaji kuangaliwa na kusimamiwa vizr kwa maendeleo ya wana masasi.

#MaendeleoHayanaChama
Nakuunga mkono hao wanao msifia wote ni wanufaika bnafsi wa Mwambe
 
Kwa Wana Masasi Mjini, Masasi, Mtwara na Kusini kwa ujumla, Mheshimiwa Geoffrey Idelphonce Mwambe(MB) ni tunu na lulu halisi.

Uzalendo na upendo wake kwa Wana Masasi Mjini ni kiashiria tosha kwamba anawahitaji sana Wana Masasi Mjini wamuunge mkono kutokana na dhamira njema aliyonayo ya kuijenga Masasi Mjini mpya ya maendeleo.

Ameamua kujipambanua kwamba yeye ni kiongozi wa namna gani. Wananchi wamjue kwamba yeye ni mwakilishi wa namna gani. Hii ni njia sahihi ya kuiambia jamii kwamba wewe ni wa aina gani ili wao wakupime kama wamepatia ama hawajapatia

Anaingia kwenye kundi la viongozi wengine wachache wa Kusini ambao waliishi maisha ya uongozi wao kwa sura hii.

Mheshimiwa Geoffrey Idelphonce Mwambe(MB) anaingia kwenye kundi la Hayati Mzee Benjamin William Mkapa, Hayati Mzee Lawi Sijaona Nangwanda, Hayati Dr Alex Halid Mtavala, Marehemu Ng'itu na wengine ambao sikuwataja hapa(nimewataja ambao ninaweza kuwaelezea angalau kwa machache ninayoyajua).

Hii ni fahari kwa Kusini na taifa letu. Jukumu letu ni kumuombea, kumpa ushirikiano na kumuunga mkono katika kila hatua ya utendaji na uwakilishi wake.

Ni wazi kwamba, kwa utendaji wa aina hii, lazima atajitengenezea maadui aidha kwa sababu ya chuki ama kwa sababu ya kuona anawatengenezea mgogoro na wananchi wao. Hili ni la kwetu, ili kila hatua atakayokuwa anaikanyaga awe salama dhidi ya chuki na husda za wanadamu wasiomtakia mema na wasioitakia mema Masasi Mjini na Kusini kwa ujumla.

MwenyeziMungu aendelee kumsimamia na kumuongoza kwenye majukumu yake ya kila siku(ya kwake binafsi na ya umma kama mwakilishi) ili aweze kuwakomboa Wana Masasi Mjini na Wana Kusini wote wanaopenda maendeleo.

Bravo Mheshimiwa Geoffrey Idelphonce Mwambe (MB).
Kawadaganye wajinga wenzenu
 
niliwahi kutana nae akiwa mtumishi wa BOT na Baadae wizara ya afrika mashariki alikuwa vizuri sana kwenye kujenga hoja... Sijui nani alimdanganya aingie kwenye siasa..... kwa CCM hii ya sasa hatoboi ,ni mmoja ya vijana watiifu wa mwenda zake
Kumbe alikuwa ni chawa?
 
Back
Top Bottom