Unatumia nguvu kubwa kuaminisha jambo ambalo si la kweli.
Nani anatumia nguvu kati yangu ninayeandika peke yake na wewe unaehangaika kuweka screenshots?
Views YouTube wewe ndo ulianza kuleta hoja hiyo kwa kujaribu Ku compare hizi nyimbo mbili(Seduce me and zilipendwa) alafu uka conclud kuwa Alikiba ana fans wachache ndo maana anapitwa views
Sasa kama nili-compare Zilipendwa na Seduce Me, hayo ma-screenshot ya ENeka na zingine yanahusika vp? And remember, hizo zinaonekana zina views chache kwa sababu ni Diamond lakini Kiba hizo ndo level zake!
The only video ya Kiba iliyofikisha 10M ni Mwana ya miaka takribani 3 iliyopita na ina views less than 12M. Views zaidi ya 10M kwa Diamond ni jambo la kawaida!!!
lakini ukasahau kuwa wimbo wa zilipendwa una jumla ya artists 6 ambao wote wanafanya vizuri.
I hate to say this but ni mtu mwenye matatizo ya uelewa tu ndie anaweza kuamini kwamba views nyingi kwenye Zilipendwa zinatokana na hao wasanii wengi uliowataja!!
Kujaribu kulinganisha views ni kufanya mistake kubwa sana.
Kumbe unatumia vigezo gani kwamba Kiba ana mashabiki wengi kuliko Diamond?
Kukuonyesha kuwa views halisi wa Diamond as solo artist kwa kuangalia nyimbo zake za hivi karibuni nakushangaa unabadili maada dio views halisi wa diamond au unakataa na hili..
Hovyo kabisa! Kwahiyo video zingine za nyuma sio za kwake na hazistahili kuwa sehemu ya kupima nguvu zake? Hivi we jamaa unajua unachoongea lakini?!
Sasa mwambieni huyo Kiba aachie ngoma 3 mfululizo muone hata kama hizo 3M Views atapata!!! Mtu kakaa zaidi ya mwaka, boost kila mahali lakini ndo kwanza ngoma Seduce Me inakimbizwa na watu ambao kila wakati wanatoa ngoma!
Nadhani ili kupima maendeleo ya kitu/jambo lolote tunategemea litoke from lower stage to the higher stage kama alikuwa ana pata view wengi kipindi cha nyuma why sasa hivi anaporomoka kumsingizia Alikiba ni kutafuta majibu mepesi na dalili za mtu mvivu na mwenye chuki.
Kama hujui kwamba hoja zako ndo hoja nyepesi basi una matatizo si kidogo!!! Kiba yupo kwenye game zaidi ya miaka 10 halafu bila aibu unasema kupima maendeleo ni kutoka lower to higher stage huku maendeleo yenyewe ukipima kwenye views za Seduce Me!! Now what about Diamond ambae kupata views 10M+ ni jambo la kawaida huku Kiba akiwa amefikisha 10M mara moja tu tangu azaliwe!!!!
Labda nikukumbushe kipindi cha zamani tuzo kwa tasnia ya mziki wetu hazikuwa dili sana kuna wasanii wengi walifanya vizuri kuliko alikiba lakini hawana tuzo.Dulli Sykes hakuwa kupata tuzo,Mr blue na wengine wengi tu.Baada ya Alikiba kurudi kwenye industry alichukuwa tuzo 5 za KTMA ambazo zilikuwa ziende kwa Diamond. .
Acha uongo wako wewe!!! Kwahiyo unataka kusema tuzo zilikuwa na deal baada ya Kiba kupata tuzo 5 na huko nyuma kwavile alikua anatoka mikono mitupu, ndo hazikuwa na deal?! Hata aibu huoni!!!
Na ungekuwa na aibu ungetafuta jibu kwanini baada ya Kiba kuchukua tuzo 5, wadhamini wakaaachana kabisa na kudhamini tuzo zenyewe baada ya kuona ujinga uliofanywa na waandaji!!!
Na kuonesha kwamba tuzo zilijaa figisu figisu, ndo maana badala ya KTMA, Mond akaenda kuchukua Channel O tuzo 3, MTV Afrca na MTV Europe bila kusahau matuzo mengine kiba ya Kinigeria!!! Hiyo rekodi sio Kiba tu bali hakuna msanii yeyote Tanzania ambae amewahi kuifikia!
Tangu arudi kwenye industry ameshachukuwa tuzo nyingi tu kwa kipindi kifupi hiki ndo kipimo cha maendeleo Mkuu
Tuzo nyingi zipi? Za KTMA? Kwani wakati Diamond anachukua MTV Africa na MTV Europe Kiba alikuwa hajarudi?! Au unatakiwa kukumbushwa kwamba Kiba alirudi 2014?