poposindege
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 453
- 175
Kwa mujibu wa utafiti ulioendeshwa na gazeti la Uhispania la AS, asilimia 32.2 ya mashabiki waReal Madrid wakoradhi kumwona mchezaji bora wa mwaka huu Christiano Ronaldo akiondoka.
Utafiti huo uliofanywa baada ya kichapo cha 1 kwa nunge kutoka kwa timu ya Athletic Bilbao uliwauliza mashabiki wa Real Madrid ni nani wangependa kumwondoa katika safu ya washambuliaji kati ya Ronaldo, Bale na Benzema.
Benzema alionekana kuwa kupenzi wa mashabiki kwani ni asilimia 21.7 tu ndio waliochagua kumwondoa ikilinganishwa na asilimia 32.2 walichagua kumwondoa Ronaldo na asilimia 46.1waliochagua kumwondoa Bale.
Mashabiki hao pia walipendelea mbinu ya 4-4-2 kuliko ile ya 4-3-3 anayotumia Ancelotti hivi sasa.
Safu ya ushambuliaji ya Christiano, Benzima na Bale almaarufu kama BBC huenda ikawa matatani.
Utafiti huo uliofanywa baada ya kichapo cha 1 kwa nunge kutoka kwa timu ya Athletic Bilbao uliwauliza mashabiki wa Real Madrid ni nani wangependa kumwondoa katika safu ya washambuliaji kati ya Ronaldo, Bale na Benzema.
Benzema alionekana kuwa kupenzi wa mashabiki kwani ni asilimia 21.7 tu ndio waliochagua kumwondoa ikilinganishwa na asilimia 32.2 walichagua kumwondoa Ronaldo na asilimia 46.1waliochagua kumwondoa Bale.
Mashabiki hao pia walipendelea mbinu ya 4-4-2 kuliko ile ya 4-3-3 anayotumia Ancelotti hivi sasa.
Safu ya ushambuliaji ya Christiano, Benzima na Bale almaarufu kama BBC huenda ikawa matatani.