Mashabiki wa Tanzania ni wakosa subira wakubwa.

Mashabiki wa Tanzania ni wakosa subira wakubwa.

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Kwanza niweke rekodi sawa. Tanzania hakuna Wapenzi wengi wa Mpira wa Miguu kama wanavyoamini wengi wetu, bali kuna Mashabiki wengi wa Simba na wa Yanga.

Kwa isivyo bahati mashabiki wetu hawa wanachowazidi Mashabiki wa sehemu nyingine Duniani ni namna hata wanavyoshabikia hizi timu zao.

Leo hii Yanga au Simba wakipoteza mchezo au kushinda basi Mashabiki hapo hapo hugeuka Washauri, Wachambuzi, Wakosoaji, Wataalamu wa soka, Mahakimu n.k.

Wakati alipoondoka Kocha wa Simba mwishoni wa msimu uliopita timu ilikuwa chini ya Matola, na walipopata matokeo mazuri kwnye mechi zilizobakia kila Mtu aliimba na kutaka Matola akabidhiwe timu....lakini kwa sasa miezi takriban mitano baadae ni Mashabiki hao hao sasa wanataka Matola aondoke.

Hali ni hivyo hivyo kwa Wachezaji, juzi wanasema Mzungu tumepigwa, leo Mzungu anajua....kesho tena akiamka vibaya watamgeuka kusema tumepigwa.

Na sasa kumeanza wimbo wa kutaka Mgunda apewe timu, kisa tu kahinda mechi zote alizosimamia mpaka sasa, sasa ngoja apoteze uone atakavyoshambuliwa kama hawamjui.

Kwa maoni yangu Simba waendelee na mchakato wa kumpata Kocha na Mgunda na Matola waendelee kuwepo benchi la ufundi, au timu ya vijana n.k.

Kama ni kuachiwa timu basi iwe ni mbeleni huko, kamwe tusiendeshwe na Mashabiki hawa wasio na subira hata kidogo....ingawa hii haimaanishi kuwa siutambui mchango wa Mashabiki.
 
Ndugu mashabiki ndivyo wanavyotakiwa kuwa hivyo ili radha ya mpira iwe imasisimua, ilitaka kocha akifanya uzembe wakae kimya tu!! huu ndo utamaduni wetu kivyetuvyetu hatuhitaji na wala hatutaki kuiga vya ndugu zenu Wazungu huko, kama vipi watuige wao.

Simba na Yanga ni timu za matokeo sio kuvumiliana na kufundisha na namna ya kuchea.
 
Bila kelele za mashabiki,mugaku angekuwa bado simba,boko angekuwa first eleven,mkwasa angekuwa kocha wa yanga ,nchimbi angekuwa etricker wa yanga
Ni sawa lakini si wa kufuatisha kila kitu.

Leo wanakwambia Mzungu tumepigwa, kesho wanakwambia Mzungu anajua...sasa ukitaka kuwafuata si utachanganyikiwa Mkuu.
 
Wewe umeanza kushabikia mpira juzi?
Mkuu, mimi nashabikia mpira tangu enzi za kina Sunday Juma na Zuberi Magoha.

Ila pointi yangu hapa ni Viongozi kuwa makini wa kuchambua hoja za Mashabiki wasikurupuke.

Sasa hivi kila Shabiki anamtaka Mgunda akabidhiwe Mikoba, akipoteza mechi mbili wanamgeuka....Viongozi wawe makini wasipelekwe na kila upepo wa Mashabiki.
 
Tanzania hakuna mashabiki wa mpira kuna watu wenye mihemko ....!!


Hivi ukiwa na akili timamu kuna timu yeyote ya mpira ambayo haifungwi ?

Tanzania kuna mashabiki vilaza wengi sanaaa...Tena wapo simba na yanga
 
Me nafikiri kuhusu kelele za mashabiki zina maana sana nikupe mfano mtoa mada.
Kwa uwezo wa phiri na namna amefunga karibia mechi zote kasoro moja nafikiri, unawezaje kumuweka benchi au kocha aseme hafai? Au timu inahitaji matokeo kwanini umtoe chama ambae ameonesha uchezaji mzuri na mtu mwenye macho ya kuona upenyo wa pasi za magoli?

Labda mfano mwingine itazame game ya jana ya mwalimu mgunda, amewaanzisha okrah na chama na phiri which means unaona kabisa huyu kocha anahitaji matokeo na si vinginevyo.

So kocha asipofanya kwa namna inavyotakiwa atapigiwa kelele tu.
 
Labda mfano mwingine itazame game ya jana ya mwalimu mgunda, amewaanzisha okrah na chama na phiri which means unaona kabisa huyu kocha anahitaji matok
Labda mfano mwingine itazame game ya jana ya mwalimu mgunda, amewaanzisha okrah na chama na phiri which means unaona kabisa huyu kocha anahitaji matokeo na si vinginevyo.

Umesema hivyo kwa kuwa ushindi ulipatikana. Timu ingefungwa, ungesikia angeanza fulani au fulani.
 
Back
Top Bottom