martial jb
JF-Expert Member
- Oct 21, 2021
- 863
- 1,462
Habari wakuu,
Katika hali inayoonekana si ya kawaida, shabiki mmoja wa Simba ameambulia kichapo kutoka kwa mashabiki wawili wa Yanga jana mnamo saa 2 usiku, pale Keko(Temeke, Dar Es Salaam).
Mashabiki hao awali inasemeka walikuwa wakibishana kawaida tu, ila shabiki wa Simba alionekana kuwatania sana Yanga huku akiwaita majina yanayokera na kuudhi mashabiki hao wa Yanga.
Baada ya muda inasemekana wana Yanga hao uvumilivu uliwashinda ndipo mmoja kati yao alipotoa lugha ya kuonya kurusha ngumi endapo mwana Simba huyo ataendelea na utani. Jambo ambalo lilitimia baada ya shabiki huyo kumpiga ngumi kijana huyo iliyompeleka chini, na ndipo wote wawili hao walionekana kumchangia kwa kumpiga kwa hasira mwana Simba huyo na kutokomea.
Mpaka watu wa pembeni wanaenda kutetea ugomvi huo, tayari yule shabiki alishachakazwa vibaya huku wana Yanga hao wakionekana kukimbia mbio mbali na eneo hilo.
ANGALIZO: Mashabiki kuweni makini na utani wenu, isifikie hatua kama hiyo inayotaka kufikia kwakweli.
Pia kuweni makini na wana Yanga, maana kwa sasa ni kweli wana msongo wa mawazo na wamechanganyikiwa na hali halisi, MSIWATANIE SANA maana siyo vizuri na ni hatari.
Pia mashabiki wa Yanga, jaribuni kuwa na busara za kimichezo, jambo kama hili ni la kipuuzi, hata kama una hasira.
Katika hali inayoonekana si ya kawaida, shabiki mmoja wa Simba ameambulia kichapo kutoka kwa mashabiki wawili wa Yanga jana mnamo saa 2 usiku, pale Keko(Temeke, Dar Es Salaam).
Mashabiki hao awali inasemeka walikuwa wakibishana kawaida tu, ila shabiki wa Simba alionekana kuwatania sana Yanga huku akiwaita majina yanayokera na kuudhi mashabiki hao wa Yanga.
Baada ya muda inasemekana wana Yanga hao uvumilivu uliwashinda ndipo mmoja kati yao alipotoa lugha ya kuonya kurusha ngumi endapo mwana Simba huyo ataendelea na utani. Jambo ambalo lilitimia baada ya shabiki huyo kumpiga ngumi kijana huyo iliyompeleka chini, na ndipo wote wawili hao walionekana kumchangia kwa kumpiga kwa hasira mwana Simba huyo na kutokomea.
Mpaka watu wa pembeni wanaenda kutetea ugomvi huo, tayari yule shabiki alishachakazwa vibaya huku wana Yanga hao wakionekana kukimbia mbio mbali na eneo hilo.
ANGALIZO: Mashabiki kuweni makini na utani wenu, isifikie hatua kama hiyo inayotaka kufikia kwakweli.
Pia kuweni makini na wana Yanga, maana kwa sasa ni kweli wana msongo wa mawazo na wamechanganyikiwa na hali halisi, MSIWATANIE SANA maana siyo vizuri na ni hatari.
Pia mashabiki wa Yanga, jaribuni kuwa na busara za kimichezo, jambo kama hili ni la kipuuzi, hata kama una hasira.