Mashahidi 52 na Vielelezo 37 kutumika kesi ya mauaji ya Asimwe, yaelezwa baba Asimwe aliahidiwa Toyota V8

Mashahidi 52 na Vielelezo 37 kutumika kesi ya mauaji ya Asimwe, yaelezwa baba Asimwe aliahidiwa Toyota V8

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Snapinsta.app_458400362_485849400908626_1834200892084997784_n_1080.jpg
Kesi namba 17740 ya mwaka 2024 ya mauaji ya mtoto aliyekuwa na Ualbino Noela Asimwe Novath inayowakabili washitakiwa tisa akiwemo padri Elipidius Rwegoshora na wenzake imetajwa tena leo tarehe 6 Septemba 2024 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wilaya Bukoba mkoani Kagera vyelelezo 37 na maelezo ya mashahidi 52 ambayo yatatumika katika kesi hiyo yakisomwa Mahakama hapo.

Maelezo ya mashahidi hao 52 yamesemwa mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Elipokea Yona na mwendesha mashitaka wa mkoa wa kagera Waziri Magumbo pamoja na mawakili wengine wa serikali ambao ni Nassoro Katuga, Sabina Silayo, Erick Mabagala pamoja na Matrida Assey.

Kwa mujibu maelezo ya mashahidi 52 yaliyosomwa na mawakili wa serikali Mahakama hapo yamebainisha kuwa mshitakiwa namba moja ambaye ni padri Elipidius Rwegoshora alikili wakati alipohojiwa kuwa ndiye aliyepanga njama za kufanya utekaji na kufanya mauaji ya mtoto Noela Asimwe Novath kwa kumshawishi mshitakiwa namba 2 Novath Venant ambaye ni Baba wa mtoto huyo na kumuahidi iwapo atafanikiwa kupata baadhi ya viungo vya mtoto huyo atampa fedha za kitanzania milion 30, kumnunulia Gari nyeusi aina ya V-8 pamoja na kumwezesha kwenda kuishi katika jiji la Dar es Salaam yeye na mke wake.
Snapinsta.app_458699352_388457437621376_8599749911641892341_n_1080.jpg

Snapinsta.app_458609840_3440642966233516_8160213081670273499_n_1080.jpg
Aidha Maelezo mengine ya mashahidi 52 yaliyotolewa mahakamani hapo ni kwamba mshitakiwa namba moja padri Elipidius Rwegoshora wakati anamshawishi Baba Asimwe pamoja na washitakiwa wengine kufanya kitendo hicho cha kupata viungo vya mtoto huyo aliwaambia kuwa awatakiwi kumwambia mtu yeyote yule kwani yeye tayari ashaenda kwa mgaga wa kienyeji na wakimwambia mtu mwingine hilo dili watakufa.

Maelezo mengine ni kuwa washtakiwa baada ya kufanikiwa kumteka na kumuuwa mtoto Asimwe mshitakiwa namba moja ambaye ni padri Elipidius Rwegoshora aliwaambia washitakiwa wengine akiwemo Baba mzazi wa mtoto Asimwe kununua sumu ya panya na kukaa nayo mda wote ili wakikamatwa na polisi wanye sumu hiyo wafe ili wapoteze ushahidi na kuwaambia kuwa wao baada ya kufa angetunza familia zao ambapo katika Maelezo yaliyosomwa Mahakama hapo.
Snapinsta.app_458698229_366096236597033_5670921584699597535_n_1080.jpg

Chanzo: Global TV

~ Watuhumiwa 9 wa mauaji ya Asimwe wadai hawajui kosa lao

~ Kagera: Watuhumiwa tisa wa mauaji ya Asimwe Novart wafikishwa mahakamani na kusomewa shtaka la kuua kwa kukusudia
~ Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji
 
"Wakikamatwa na polisi wanywe sumu wafe ili wapoteze ushahidi na kuwaambia kuwa wao baada ya kufa angetunza familia zao".
Akili ni nywele....
 
Jamani ndugu zangu, wenye makampuni, viwanda au wenye ndugu, marafiki na wadau.
Naomba kazi hata ya kujitolea nipatw angalau experience ya kazi.. Nipo tayari kujitolea jamani, maana nikienda directly kuomba kazi na kupereka Cv narudishwa punde tu nikifika mapokezi, naambiwa nafasi hazipo hapa.

Mimi ni fresh graduate..
Nina degree ya Business IT.
Naweza kufanya kazi za database administration, business analysis, Business Intelligence, Business Process management, customer relationship management..
Pia nipo tayari kufanya kazi yoyote nitakayopewa na kampuni tofauti na mambo niliyosomea.

Nipo Dar es salaam. Ubungo RiverSide.
Mawasiliano; Normal call: 0616604372
Whatsap: 0620224372.
Jamani mnisaidie, sina pakuenda, sina ndugu yeyote anayefanya kazi serikalini walau wa kunisaidia kutafuta hata nafasi ya internship
 
Rwegashora unaona kunywa sumu mchezo, mbona wewe sasa unashindwa.Wanyongwe tuuu .
 
Mhaya sifa hadi kwenye uhai wa watu, et mtakunywa sumu mimi nitalea familia zenu. For how long? why are these people allowed to continue to live until now and continue to oppress the country by eating free food?
 
Mtu anakuambia umuue mwanao atakupa gari na ww ubakubali.Hujui kua huyo huyo anaweza kukuua hata ww kuna watu wanatamaa sana.
 
Mhaya sifa hadi kwenye uhai wa watu, et mtakunywa sumu mimi nitalea familia zenu. For how long? why are these people allowed to continue to live until now and continue to oppress the country by eating free food?
I don't know..aisee
 
Back
Top Bottom