Wana JF
Taarifa tulizopata kwa wiki hii nzima hasi leo, zomebainishwa yafuatayo:-
1. Lilian Mashaka amekuwa akitoa mambo yanayohusu TAKUKURU na Hosea ili akamaate uongozi wa TAKUKURU,
2. Lilian Mashaka alikuwa na uhusiano wa karibu na KAMAZIMA ndiyo akajiandaa kumrithi,
3. Mwarabu aitwaye AWADH MOHAMED amekuwa akitumiwa na mama huyu kummaliza Hosea,
4. Kuna waandishi wa habari kumbe ni wanaJF wametoa habari hizi tata kwenye mtandao huu kwenye hoja ya 'HOSEA ATAKWEPA DHAMBI HII?',
5.Vita ya rushwa pia imeiingiliwa na wabunge wenye tuhuma kwa TAKUKURU,
6. Kuna uhusiano kati ya Mashaka, Awadhi, Mahalu na Mwakyembe.
7. Hoja zilizotokana na hoja ya 4. hapo juu, imekwama baada ya watu kushindwa kutoa kifungu cha sheria ya kuzuia rushwa kinachoongelea HARUFU NA KIWINGU CHA RUSHWA kwa mjibu wa sheria ya 1971,
8. Kama si majungu, Dr Mwakyembe ameshindwa kutupatia orodha ya watuhumiwa wa rushwa na kwa taarifa yake makini,
Wana JF tujadili kwa makini maana tunaweza kujenga na kuibomoa TAKUKURU na inawezekana RAIS JK naye akawa ni mwana JF mwenzetu pia.
Karibuni kwa hoja.
Mrisho Shaban Be professional.
Ulichokieleza hapo juu ni Riwaya sawa na ile riwaya ya Shaban Robert ya Kufikirika.
Maelezo yako yamejengwa katika majungu ya wezi waliozoea kusema wao ni watu wa system.
Inaonekana wazi kwamba kibano cha maneno kimewakwida kweli kweli sasa manaona ni bora mvae sura za huzuni muonewe huruma.
Janja yenu haiwezi kuwasaidia hata kidogo, kwa sababu tumeamka kutoka usingizini, safari hii kila mtu atabeba furushi lake la dhambi hadi kuzimu.
Inaelekea kuna mambo kede kede ya Takukuru msiyo penda sisi walala hoi tusikie sasa mtu akisema mnamuona ni nduli.
Tueleze kwa kirefu mnaficha nini huko Takukuru, ambacho mnahisi Lilian amekuwa akikitoa nje ya Takukuru tofauti na dhamira zenu?
Kifungu cha 2 na cha 3 umejikanyaga sana!
Anaye taka kumwondoa Hosea ni Liliani Mashaka, sasa iweje Awadhi amtumie Lilian Mashaka kumwondoa Hosea?
Kwa hiyo una maana Lilian anatumiwa na Awadhi siyo? Kwa maana kwamba Awadhi ndiye anayetaka cheo cha Hosea, au kwa maana ya Awadhi kupenda Liliani awe Bosi?
Kama Lilian ana ambition za kuwa Bosi wa Takukuru ni vipi tena anatumiwa na Mwarabu Awadhi kumwondoa Hosea.
yeye Awadhi hana nguvu hiyo?
Hosea akiondoka yeye Awadhi atapata cheo hicho?
Je kama Lilian anajua Awadhi pia anakitaka cheo hicho kwa nini akubali Awadhi amtumie?
Maelezo yako yamejikanyaga yenyewe, kiasi kwamba swali langu kwako ni hili.
Wewe kama siyo Hosea, ni nani katuma uje umtetee Hosea kimajungu jungu hapa JF?
Nani kakwambia hili ni jamvi la majungu?
Habari Tata kuhusu Hosea ni zipi?
Hivi watu wakienda kinyume na Mazoa yenu ya kulindwa na mkiitacho system mfanyapo makosa ndiyo mnaziita habari hizo ni tata?
Mmezoea kunyofoa shingo sasa mkichinjiwa mimacho inawatoka eeH?!
Vita ya Rushwa imeingiliwa na Wabunge wenye tuhuma kwa Takukuru??
Lete List yako hapa ya wabunge wanao tuhumiwa na Takukuru.
Ina maana List ya wala Rushwa mnayo sasa mmeiweka kwenye Mafaili ili Muitumie Ku Blackmail watu?
Hiyo ni Takukuru au Tawi la Mafia au lile genge la maharamia wa YAKUZA toka Japan?
Takukuru si chombo cha kutuhumu watu juu ya Rushwa. Takukuru ni chombo cha kuchunguza Rushwa na Mazingira yake.
Sasa najua kwa nini wewe ndugu yangu na wenzio akina Hosea mlisema mambo yote RDC ni shwari[ swanu].
Sababu kubwa ni kwamba chombo chenu mmekigeuza kuwa cha kutuhumu watu badala ya kupeleleza na kuthibitisha, sijui kazi kuthibisha rushwa mnamwachia nani?
Kazi ya Dr Mwakyembe haikua kutafuta wala Rushwa na kuwaorodhesha,kazi ambayo kwa asili ni yenu.Kazi yake kubwa ilikuwa ni kutafuta ukweli juu ya RDC na mazingira iliyo jisimika Tanzania kazi ambayo ameifanya vizuri sana.
Mmezoea kuvurunda mambo ya kuyalundika yavunde ndo maana mtu akiuweka wazi uoza wenu mnanuna na kutaka kupigana kama si kuua.
Sasa kama watu wa Takukuru mnataka kupewa List ya wala Rushwa si afadhari Mmuombe Rais aivunje Takukuru tubakie na CID ya Polisi?
Kazi yenu Takukuru ni kuchunguza tuhuma ili kubaini ukweli wa tuhuma hizo.
Tupe kwa undani uhusiano wa Lilian, Awadh, Dr Mwayembe na Prof Mahalu, ukiacha uweli Mahalu na Mwakyembe wote wamefundisha chuo kikuu.
Mimi utanitisha sana tu Ukisema Mwenye enzi yote Muumba wa mbingu na nchi,Mungu, naye ni mmoja wa wana JF na amekuwa akitoa michango yake in personal.
Kama Ibili na jeshi lake lote ni mmoja wetu au kiumbe yeyote wa ajabu ni member wa JF sisi hatumwogopi hata kidogo, kinyume chake ni yeye ndiye mwenye hofu, ndiyo maana kaja kutaka kujua tunaongea nini hapa.
Hapa haogopwi Rais wa nchi wala mtu yeyote ndani ya serikali Tanzania.
Hapa JF pia hapendwi mtu kwa mamlaka aliyo nayo wala mkwara wake wa kijivuni.
Hapa inapendwea hoja yenye kusimama kwa miguu miwili na mwelekeo wa kujenga nchi na watu wake.
Mrisho Shaban tupe maelezo ya maana na yenye ushahidi kuhusu tuhuma zako au kaa kimya milele.