jamani kuweni makini ardhi haiuzwi kama unanunua shati au nguo ubungo. Msije mkakurupuka. Just important tips unapotaka kununua ardhi ambayo imepimwa.
1. Hakikisha anayekuuzia ni mmiliki halala wa kiwanja au shamba
2. Awe anafahamika kwa mwenyekiti, mjumbe na mtendaji kata wa eneo husika kwamba yeye ndie mmiliki halali.
3. Kama ardhi imepimwa awe na hati au title ya hicho kiwanja au shamba
4. Kama hana tafuta land surveyor akusaidie kuangalia km hilo eneo kwenye master plan limepangiwa matumizi gani na km barabara haipiti kwenye kiwanja unachotaka kununua.
5. Kama ana hati au title ya kiwanja chukua title number mara nyingi ipo juu ya hati. Then nenda wizara ya ardhi kufanya title search pale utapata taarifa rasmi za kuthibitisha kama anayekuuzia ni mmliliki halali wa hicho kiwanja au shamba.
So due care and buyer be aware is needed when u r buying land