Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu, mambo yameamka huku
====
Jana Machi 4, 2025 Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam chini ya Jaji Kirekiano iliwaachia huru MASHEIKH 12, walio kaa gerezani miaka 10, kwa tuhuma za Ugaidi.
Baada ya hukumu hiyo Shura ya Maimamu Tanzania ilitoa taarifa ya kuachiwa huru Masheikh hao.
Wakati taarifa hiyo ikitolewa Masheikh hao walikua wako chini ya itifaki za watu wa usalama na ndugu walitakiwa kwenda kituo cha Polisi cha stakishari kwaajili ya kukamilisha itifaki hizo.
Hata hivyo majira ya magharibi ndugu walipofika stakishari waliambiwa masheikh hao hawajafikishwa pale.
Aidha leo asubuhi ndipo zilipopatikana taarifa kuwa ndugu Masheikh hao wapo katika gereza la Ukonga walilpokuwapo awali.
Ni wazi baada ya Mahakama kuwaachia huru Masheikh hao, watu wa usalama walitumia mbinu mbalimbali wakafanikiwa kuwakamata tena na kuwafungulia mashtaka mapya bila ya ndugu zao kufahamu.
Kwa hakika tukio hili linadhihirisha jinsi ambavyo serikali iliyopo madarakani isivyojali haki za binadamu. Watu hawa wamekamatwa toka 2015, mpaka leo serikali imeshindwa kuthibitisha tuhuma dhidi yao lakini inaendelea kuwanyima haki za msingi na kuwatesa.
Pia soma: Pre GE2025 - Masheikh 12, waliokaa gerezani miaka 10, kwa tuhuma za Ugaidi waachiwa huru
Katika taarifa ya jana tumeeleza madhila yaliyowakuta baadhi yao ikiwa ni pamoja na kupoteza wenziwao na wengine kufia gerezani.
Hivi viongozi wetu wanashindwa kuvihoji vyombo vyao juu ya matukio haya yaliyo kinyume na sheria na utu.
Hivi inaingia akilini mzee Sleiman Ulatule miaka 90, achukue familia yake ya zaidi ya watu 7, waende kuvamia kituo cha polisi?
Katika wasifu huo watawala watakua na uso gani wa kusimama mbele ya wananchi wakiwemo Waislamu kuwaomba ridhaa ya kuongoza nchi.
Ni zuzu wa kiasi gani atakayewapa ridhaa watawala wasio zingatia haki za binadamu, uhuru na haki za kuishi zinazolindwa na Katiba ya nchi.
Aidha tutumie fursa hii kuwaomba Waislamu wote nchini kutumia fursa hii ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kuomba dua makhsusi na kumkabidhi Mwenyezi Mungu Mtukufu atoe hukumu kwa haya wanayotendewa wanyonge nchini Tanzania.
Atakayeacha kuomba dua hii maana yake ameridhia haya wanayotendewa binadamu wenzake wasio na hatia yoyote.
Shura ya Maimamu Tanzania
====
Jana Machi 4, 2025 Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam chini ya Jaji Kirekiano iliwaachia huru MASHEIKH 12, walio kaa gerezani miaka 10, kwa tuhuma za Ugaidi.
Baada ya hukumu hiyo Shura ya Maimamu Tanzania ilitoa taarifa ya kuachiwa huru Masheikh hao.
Wakati taarifa hiyo ikitolewa Masheikh hao walikua wako chini ya itifaki za watu wa usalama na ndugu walitakiwa kwenda kituo cha Polisi cha stakishari kwaajili ya kukamilisha itifaki hizo.
Hata hivyo majira ya magharibi ndugu walipofika stakishari waliambiwa masheikh hao hawajafikishwa pale.
Aidha leo asubuhi ndipo zilipopatikana taarifa kuwa ndugu Masheikh hao wapo katika gereza la Ukonga walilpokuwapo awali.
Ni wazi baada ya Mahakama kuwaachia huru Masheikh hao, watu wa usalama walitumia mbinu mbalimbali wakafanikiwa kuwakamata tena na kuwafungulia mashtaka mapya bila ya ndugu zao kufahamu.
Kwa hakika tukio hili linadhihirisha jinsi ambavyo serikali iliyopo madarakani isivyojali haki za binadamu. Watu hawa wamekamatwa toka 2015, mpaka leo serikali imeshindwa kuthibitisha tuhuma dhidi yao lakini inaendelea kuwanyima haki za msingi na kuwatesa.
Pia soma: Pre GE2025 - Masheikh 12, waliokaa gerezani miaka 10, kwa tuhuma za Ugaidi waachiwa huru
Katika taarifa ya jana tumeeleza madhila yaliyowakuta baadhi yao ikiwa ni pamoja na kupoteza wenziwao na wengine kufia gerezani.
Hivi viongozi wetu wanashindwa kuvihoji vyombo vyao juu ya matukio haya yaliyo kinyume na sheria na utu.
Hivi inaingia akilini mzee Sleiman Ulatule miaka 90, achukue familia yake ya zaidi ya watu 7, waende kuvamia kituo cha polisi?
Katika wasifu huo watawala watakua na uso gani wa kusimama mbele ya wananchi wakiwemo Waislamu kuwaomba ridhaa ya kuongoza nchi.
Ni zuzu wa kiasi gani atakayewapa ridhaa watawala wasio zingatia haki za binadamu, uhuru na haki za kuishi zinazolindwa na Katiba ya nchi.
Aidha tutumie fursa hii kuwaomba Waislamu wote nchini kutumia fursa hii ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kuomba dua makhsusi na kumkabidhi Mwenyezi Mungu Mtukufu atoe hukumu kwa haya wanayotendewa wanyonge nchini Tanzania.
Atakayeacha kuomba dua hii maana yake ameridhia haya wanayotendewa binadamu wenzake wasio na hatia yoyote.
Shura ya Maimamu Tanzania