Mkuu ishu sio chekecheo tu? Maana wengine wanaweka size kubwa kweli ..ukiweka zile namba ndogo sijui ndo namba 1 unga unatoka soft!..operator hapa anahusikaje mkuu hebu nidadavulie!
Boss ipo hivi. Mashine inaendeshwa na operator/msagaji. Oparator ndiye nahodha wa chombo.Ndio maana mashine hasa za vijijini akiondoka oparatoŕ/msagaji akija mwingine utasikia "Joni anatoa chenga au anaiba unga,unga mweusi,hauivi,unachenga" ishu sio wizi ni umahiri wa oparator.
Kitaalam,Ubora wa unga wa mahindi unaanzia pale oparator anapoweka maji. Zipo mashine oparator ndie anaweka maji,oparator mjuzi hawezi kubali wewe uweke maji ataweka yeye. Yale maji yanakazi yake na yana kipimo chake ndiyo yanafanya mchawi wa unga/kapi litoke lote au libaki katika mahindi.
Pili katika kinu cha kukoboa chini ya "feeder" kuna "keys" ya kuruhusu mahindi kuingia katika chemba na key ya kuruhusu mahindi yatoke katika chemba ambazo kama mashine inafanya kazi utaona operator anacheza na hiyo keys,anakuwa kama anazibalance huku anashika mahindi yanayotoa wakati mwingine anayarudia pale anacheza na kisu na wembe kuhakikisha mbegu inalivua ganda/mchawi vizuri kwa ajiri ya kusagwa.
Kisu na wembe visipo menya lile ganda vizuri hata usage vipi utakula chenga tuu na ugali utasikia wakina mama kesho wamerudi kuleta feedback ya ugali kimeo.
Maana lile ganda lisipotoka lote likiingizwa kwenye kinu cha kusaga halisagiki linapenya kwenye chekecheo na hua halipenyi peke yake linapenya particles za mhindi hivyo kutengeneza chenga labda arudie sana unga napo kwa mbinde. Akirudia sana umeme hawezi kukubali hasara.
Chekecheo iwe B22 na M22 kama ganda la plastiki litabaki kwa kiasi kikubwa katika mahindi baada ya kukobolewa ndio mchawi wa unga,ukiruhusu liingie kwenye kinu cha kusaga linapenya kwenye chekecheo yeyote na likitoka linapulizwa na feni linatoka pamoja na unga likiwa na particles ambazo zinaitwa chenga na linaathari kuanzia kwenye unga/texture mpaka tumbo la mlaji.
Pia kwa nyongeza. Kazi ya kukoboa ni kutoa hilo ganda la plastiki/kapi lipo nje ya mhindi na kazi ya kusaga ni kusaga ni kusaga kile kinachobaki.
Oparator mzuri akibaini bado ganda hilo halijaisha atarudia mahindi na akiona bado atakwambia upepete hayo mahindi kutoa huyo mchawi wa unga.
Mashine nzuri ni ile inayoweza kutoa hilo ganda vizuri. Kusaga dona ni kutoa hilo ganda na kubakiza kiini tete,kusaga sembe ni kutoa kapi na kiini tete. Sasa watu wengi wanafikiri kusaga dona ni kusaga na hilo ganda/kapi kitu ambacho sio sahihi na hatari kwa afya. Hilo ganda halisagiki hata tumboni?
Dona ni unga ulio na kiini tete sio kapi au ganda au mchawi. Ukitaka upate dona nunua unga uliosagwa na mashine ya kisasa/hummer mill ambayo inaweza kutoa kapi na kubakiza kiini tete.