Mashujaa wa Mlima Kilimanjaro: Lucy Lameck na Yusuf Olotu

Mashujaa wa Mlima Kilimanjaro: Lucy Lameck na Yusuf Olotu

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Rafiki yangu Fredy Nyaluchi kaweka hapa barzani picha ya Lucy Lameck na maelezo kidogo ya maisha yake katika siasa za Tanzania.

Nataka kumuunga mkono kwa kuongeza kidogo katika maisha ya Lucy Lameck ili kujaza nyama katika mifupa ya historia ya TANU na harakati za uhuru.

Lucy Lameck aliibuliwa na Yusuf Olotu lakini akijulikana kwa jina la kazi yake, Yusuf Ngozi kwa kuwa alikuwa mfanyabiashara wa ngozi.

Lucy Lameck akaja kufahamika na kushika nyadhifa kadhaa lakini Yusuf Olotu kafa hakuna amjuaye licha ya mchango wake mkubwa katika kuasisi TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Nilikwenda kumuona Mzee Yusuf Olotu nyumbani kwake Moshi nyakati za jioni baada ya L’ Asr.

Nilimkuta Mzee Olotu ndani amelala kwa kuwa hali yake ya afya haikuwa njema sana.

Baada ya ujitambulisha alichangamka kwani nilipomtajia wazazi wangu wote akawa anawafahamu ingawa ni miaka mingi hawajaonana.

Mtoto wa Mzee Olotu Ahmed ni makamo yangu na tulicheza pamoja utotoni kwa kuwa nyumba zetu zilikuwa jirani Moshi Mtaa Chini.

Mzee Olotu alifurahi kusikia naandika kitabu cha historia yao wapigania uhuru wa Tanganyika.

Akanieleza kuwa walipita watu kwake miaka michache iliyopita wakitokea CCM na wakachukua nyaraka zake zote na picha wakidai kuwa wanakusanya nyaraka hizo na picha kwa ajili ya kuandika historia ya TANU na pia kutoa kifuta jasho kwa wale waliokuwa mstari wa mbele kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kwa masikitiko alinieleza kuwa hakuna kilichofanyika na hata alipokwenda ofisi ya CCM kuomba angalau wamrudishie nyaraka na picha zake aliishia kuzungushwa.

Tukaanza mazungumzo huku kinasa sauti changu kikizunguka taratibu.

Mzee Olotu alikuwa anasumbuliwa na kikohozi lakini alianza kuzungumza kwa utaratibu baada ya kuwaambia vijana wake waliokuwa nje kuwa ana mgeni muhimu na hataki kusumbuliwa.

Hatukufika mbali katika mazungumzo mvua kubwa ikaanza kunyesha ikasindikizwa na radi

Kwa miaka mingi badae kila nilipokuwa namsikiza Mzee Olotu katika kinasa sauti changu na nikisikia vile akinyamaza kuzungumza kwa ajili ya kikohozi kisha akireja kueleza historia ya uhuru sauti yake ikiingiliana na radi nilikuwa najiuliza – ile radi ilikuwa inaashiria nini?

Nilikuwa Arusha baada ya miaka kupita ndipo nilipopata taarifa kuwa Mzee Olotu amefariki na kazikwa jana yake.

Niliondoka siku ya pili yake kwenda Moshi kuhani.

Nasikitika kuwa Mzee Olotu hakukiona kitabu ambacho kimemtaja yeye na wenzake katika kuunda TANU Kilimanjaro, mwaka wa 1955 na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Uchagga ilikuwa chini ya utawala wa machifu waliokuwa wakijulikana kama Mangi.

Baadhi ya machifu hawa walikuwa katika Baraza la Kutunga Sheria na kwa ujumla wao walikuwa karibu na serikali ya kikoloni kuliko walivyokuwa na wananchi wanaowaongoza.

Hali ya siasa Jimbo la Kaskazini ilikuwa ngumu na ya kukatisha tamaa.

Wakati TANU inakabiliwa na Kura Tatu mgogoro wa ardhi ya Wameru ulikuwa umekwisha kwa wananchi kudhulumiwa haki yao.

Japhet Kirilo alikuwa amerudi kutoka Umoja wa Mataifa alikopeleka madai ya Wameru mikono mitupu.

Kirilo hakuwa na chochote cha kuwaonyesha Watanganyika.

Ilikuwa Yusuf Ngozi ndiye aliyeweza kuifanya TANU iingie kwanza Moshi mjini kwa vishindo na kutoka hapo mjini akaieneza vijijini.

Kupitia kumbukumbu za Mzee Yusuf ngozi ndipo unapokutana na historia za awali kabisa za wanasiasa maarufu waliopata majina na vyeo; na wengine kuwa mawaziri katika Tanganyika huru, kama Lucy Lameck, Enesmo Eliufoo na wengineo.

Ilikuwa Yusuf Ngozi ndiye pamoja na wazalendo wengine waliifanya TANU ishinde uchaguzi wa Kura Tatu mwaka 1958.

Kupitia kumbukumbu zake halikadhalika ndipo kwa huzuni kubwa utakapokutana na mashujaa waliosahaulika kama yeye mwenyewe, mashujaa wa kike na wa kiume, wazalendo kama marehemu Mama Bint Maalim, Amina bint Kinabo, Halima bint Selengia, Juma Ngoma, Melkezedek Simon, Gabrieli Malaika na wengineo.

Hawa ndiyo mashujaa ambao kwa muda waliamua wasahau nguvu na utawala wa machifu wao na kujiweka chini ya TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
1082948

Lucy Lameck

MASHUJAA WA MLIMA KILIMANJARO: LUCY LAMECK NA YUSUF OLOTU

Rafiki yangu Fredy Nyaluchi kaweka hapa barzani picha ya Lucy Lameck na maelezo kidogo ya maisha yake katika siasa za Tanzania.

Nataka kumuunga mkono kwa kuongeza kidogo katika maisha ya Lucy Lameck ili kujaza nyama katika mifupa ya historia ya TANU na harakati za uhuru.

Lucy Lameck aliibuliwa na Yusuf Olotu lakini akijulikana kwa jina la kazi yake, Yusuf Ngozi kwa kuwa alikuwa mfanyabiashara wa ngozi.

Lucy Lameck akaja kufahamika na kushika nyadhifa kadhaa lakini Yusuf Olotu kafa hakuna amjuaye licha ya mchango wake mkubwa katika kuasisi TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

1082964

Yusuf Olotu

Nilikwenda kumuona Mzee Yusuf Olotu nyumbani kwake Moshi nyakati za jioni baada ya L’ Asr.

Nilimkuta Mzee Olotu ndani amelala kwa kuwa hali yake ya afya haikuwa njema sana.

Baada ya ujitambulisha alichangamka kwani nilipomtajia wazazi wangu wote akawa anawafahamu ingawa ni miaka mingi hawajaonana.

Mtoto wa Mzee Olotu Ahmed ni makamo yangu na tulicheza pamoja utotoni kwa kuwa nyumba zetu zilikuwa jirani Moshi Mtaa Chini.

Mzee Olotu alifurahi kusikia naandika kitabu cha historia yao wapigania uhuru wa Tanganyika.

Akanieleza kuwa walipita watu kwake miaka michache iliyopita wakitokea CCM na wakachukua nyaraka zake zote na picha wakidai kuwa wanakusanya nyaraka hizo na picha kwa ajili ya kuandika historia ya TANU na pia kutoa kifuta jasho kwa wale waliokuwa mstari wa mbele kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kwa masikitiko alinieleza kuwa hakuna kilichofanyika na hata alipokwenda ofisi ya CCM kuomba angalau wamrudishie nyaraka na picha zake aliishia kuzungushwa.

Tukaanza mazungumzo huku kinasa sauti changu kikizunguka taratibu.

Mzee Olotu alikuwa anasumbuliwa na kikohozi lakini alianza kuzungumza kwa utaratibu baada ya kuwaambia vijana wake waliokuwa nje kuwa ana mgeni muhimu na hataki kusumbuliwa.

Hatukufika mbali katika mazungumzo mvua kubwa ikaanza kunyesha ikasindikizwa na radi…

Kwa miaka mingi badae kila nilipokuwa namsikiza Mzee Olotu katika kinasa sauti changu na nikisikia vile akinyamaza kuzungumza kwa ajili ya kikohozi kisha akireja kueleza historia ya uhuru sauti yake ikiingiliana na radi nilikuwa najiuliza – ile radi ilikuwa inaashiria nini?

Nilikuwa Arusha baada ya miaka kupita ndipo nilipopata taarifa kuwa Mzee Olotu amefariki na kazikwa jana yake.

Niliondoka siku ya pili yake kwenda Moshi kuhani.

Nasikitika kuwa Mzee Olotu hakukiona kitabu ambacho kimemtaja yeye na wenzake katika kuunda TANU Kilimanjaro, mwaka wa 1955 na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Uchagga ilikuwa chini ya utawala wa machifu waliokuwa wakijulikana kama Mangi.

Baadhi ya machifu hawa walikuwa katika Baraza la Kutunga Sheria na kwa ujumla wao walikuwa karibu na serikali ya kikoloni kuliko walivyokuwa na wananchi wanaowaongoza.

Hali ya siasa Jimbo la Kaskazini ilikuwa ngumu na ya kukatisha tamaa.

Wakati TANU inakabiliwa na Kura Tatu mgogoro wa ardhi ya Wameru ulikuwa umekwisha kwa wananchi kudhulumiwa haki yao.

Japhet Kirilo alikuwa amerudi kutoka Umoja wa Mataifa alikopeleka madai ya Wameru mikono mitupu.

Kirilo hakuwa na chochote cha kuwaonyesha Watanganyika.

Ilikuwa Yusuf Ngozi ndiye aliyeweza kuifanya TANU iingie kwanza Moshi mjini kwa vishindo na kutoka hapo mjini akaieneza vijijini.

Kupitia kumbukumbu za Mzee Yusuf ngozi ndipo unapokutana na historia za awali kabisa za wanasiasa maarufu waliopata majina na vyeo; na wengine kuwa mawaziri katika Tanganyika huru, kama Lucy Lameck, Enesmo Eliufoo na wengineo.

Ilikuwa Yusuf Ngozi ndiye pamoja na wazalendo wengine waliifanya TANU ishinde uchaguzi wa Kura Tatu mwaka 1958.

Kupitia kumbukumbu zake halikadhalika ndipo kwa huzuni kubwa utakapokutana na mashujaa waliosahaulika kama yeye mwenyewe, mashujaa wa kike na wa kiume, wazalendo kama marehemu Mama Bint Maalim, Amina bint Kinabo, Halima bint
Selengia, Juma Ngoma, Melkezedek Simon, Gabrieli Malaika na wengineo.

Hawa ndiyo mashujaa ambao kwa muda waliamua wasahau nguvu na utawala wa machifu wao na kujiweka chini ya TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kwa kuhitimisha naweka hapa chini maneno aliyoandika Daisy Sykes katika kumbukumbu ya miaka 50 ya kifo cha baba yake akikumbuka yale aliyokuwa akiyaona nyumbani kwao ambako kila siku walikuwa wakija wazalendo viongozi wa TANU wapigania uhuru wa Tanganyika:

1082965

Mwami Theresa Ntare

''...it was also during this formative period in my life that I met the up and coming women nationalist leaders such as Bi Lucy Lameck from Moshi, Mary Ibrahim and the mainly Moslem women, such as Bibi Titi, Bi. Tatu biti Mzee, Bi. Hawa biti Maftaha from Dar es Salaam who all passed as my grannies.

All of these women were carefully selected for their courage and became prominent at political rallies, singing and shouting out nationalist slogans, a trend that was totally unexpected and untypical for a Moslem woman, who were supposed to be subdued, modest and who remained behind the scenes.

I overheard numerous discussions when my Dad and his colleagues discussed the names and occasions for which these women were to be brought in to build the political momentum.

But what has really stayed within my memory was frequent arrival of the leadership echelons of the pre independence era, the tribal chiefs and the leaders of the budding nationalist movements, trade unions and other government staff.

Hence, courtesy to my father’s fame and hospitality, I grew up to be no stranger to the famous tribal chiefs and royalty as I greeted and attended to the dignitaries who came home regularly.

Such high profile frequent guests included Mangi Mkuu Thomas Mareale, Chiefs Abdiel Shangali, John Maruma from Moshi, Adam Sapi Mkwawa from Iringa, Kidaha Makwaiya from Usukuma, Abdallah Fundikira, Harun Lugusha from Tabora, , Humbi Ziota from Nzega, Michael Lukumbuzya from Ukerewe and Patrick Kunambi from Morogoro among others.

They were normally accompanied by their very dignified looking wives who never ceased to mesmerize me.

I remember among the chiefs, was the one and only woman Chief Mwami Ntare from Kasulu Kibondo.''

(Daisy Sykes Buruku, ''Abdul Sykes that I Knew.'')

Picha: Lucy Lameck, Yusuf Olotu, Chief Marealle, Chief Abdiel Shangali, Chief John Maruma, Mwami Theresa Ntare, Chief Abdallah Said Fundikira, Chief David Kidaha Makwaia.
 

yangu Fredy Nyaluchi kaweka hapa barzani picha ya Lucy Lameck na maelezo kidogo ya maisha yake katika siasa za Tanzania.

Nataka kumuunga mkono kwa kuongeza kidogo katika maisha ya Lucy Lameck ili kujaza nyama katika mifupa ya historia ya TANU na harakati za uhuru.

Lucy Lameck aliibuliwa na Yusuf Olotu lakini akijulikana kwa jina la kazi yake, Yusuf Ngozi kwa kuwa alikuwa mfanyabiashara wa ngozi.

Lucy Lameck akaja kufahamika na kushika nyadhifa kadhaa lakini Yusuf Olotu kafa hakuna amjuaye licha ya mchango wake mkubwa katika kuasisi TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

1082954

Nilikwenda kumuona Mzee Yusuf Olotu nyumbani kwake Moshi nyakati za jioni baada ya L’ Asr.

Nilimkuta Mzee Olotu ndani amelala kwa kuwa hali yake ya afya haikuwa njema sana.

Baada ya ujitambulisha alichangamka kwani nilipomtajia wazazi wangu wote akawa anawafahamu ingawa ni miaka mingi hawajaonana.

Mtoto wa Mzee Olotu Ahmed ni makamo yangu na tulicheza pamoja utotoni kwa kuwa nyumba zetu zilikuwa jirani Moshi Mtaa Chini.

Mzee Olotu alifurahi kusikia naandika kitabu cha historia yao wapigania uhuru wa Tanganyika.

Akanieleza kuwa walipita watu kwake miaka michache iliyopita wakitokea CCM na wakachukua nyaraka zake zote na picha wakidai kuwa wanakusanya nyaraka hizo na picha kwa ajili ya kuandika historia ya TANU na pia kutoa kifuta jasho kwa wale waliokuwa mstari wa mbele kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kwa masikitiko alinieleza kuwa hakuna kilichofanyika na hata alipokwenda ofisi ya CCM kuomba angalau wamrudishie nyaraka na picha zake aliishia kuzungushwa.

Tukaanza mazungumzo huku kinasa sauti changu kikizunguka taratibu.

Mzee Olotu alikuwa anasumbuliwa na kikohozi lakini alianza kuzungumza kwa utaratibu baada ya kuwaambia vijana wake waliokuwa nje kuwa ana mgeni muhimu na hataki kusumbuliwa.

Hatukufika mbali katika mazungumzo mvua kubwa ikaanza kunyesha ikasindikizwa na radi…

Kwa miaka mingi badae kila nilipokuwa namsikiza Mzee Olotu katika kinasa sauti changu na nikisikia vile akinyamaza kuzungumza kwa ajili ya kikohozi kisha akireja kueleza historia ya uhuru sauti yake ikiingiliana na radi nilikuwa najiuliza – ile radi ilikuwa inaashiria nini?

Nilikuwa Arusha baada ya miaka kupita ndipo nilipopata taarifa kuwa Mzee Olotu amefariki na kazikwa jana yake.

Niliondoka siku ya pili yake kwenda Moshi kuhani.

Nasikitika kuwa Mzee Olotu hakukiona kitabu ambacho kimemtaja yeye na wenzake katika kuunda TANU Kilimanjaro, mwaka wa 1955 na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Uchagga ilikuwa chini ya utawala wa machifu waliokuwa wakijulikana kama Mangi.

Baadhi ya machifu hawa walikuwa katika Baraza la Kutunga Sheria na kwa ujumla wao walikuwa karibu na serikali ya kikoloni kuliko walivyokuwa na wananchi wanaowaongoza.

Hali ya siasa Jimbo la Kaskazini ilikuwa ngumu na ya kukatisha tamaa.

Wakati TANU inakabiliwa na Kura Tatu mgogoro wa ardhi ya Wameru ulikuwa umekwisha kwa wananchi kudhulumiwa haki yao.

Japhet Kirilo alikuwa amerudi kutoka Umoja wa Mataifa alikopeleka madai ya Wameru mikono mitupu.

Kirilo hakuwa na chochote cha kuwaonyesha Watanganyika.

Ilikuwa Yusuf Ngozi ndiye aliyeweza kuifanya TANU iingie kwanza Moshi mjini kwa vishindo na kutoka hapo mjini akaieneza vijijini.

Kupitia kumbukumbu za Mzee Yusuf ngozi ndipo unapokutana na historia za awali kabisa za wanasiasa maarufu waliopata majina na vyeo; na wengine kuwa mawaziri katika Tanganyika huru, kama Lucy Lameck, Enesmo Eliufoo na wengineo.

Ilikuwa Yusuf Ngozi ndiye pamoja na wazalendo wengine waliifanya TANU ishinde uchaguzi wa Kura Tatu mwaka 1958.

Kupitia kumbukumbu zake halikadhalika ndipo kwa huzuni kubwa utakapokutana na mashujaa waliosahaulika kama yeye mwenyewe, mashujaa wa kike na wa kiume, wazalendo kama marehemu Mama Bint Maalim, Amina bint Kinabo, Halima bint Selengia, Juma Ngoma, Melkezedek Simon, Gabrieli Malaika na wengineo.

Hawa ndiyo mashujaa ambao kwa muda waliamua wasahau nguvu na utawala wa machifu wao na kujiweka chini ya TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
Rafiki yangu Fredy Nyaluchi kaweka hapa barzani picha ya Lucy Lameck na maelezo kidogo ya maisha yake katika siasa za Tanzania.

Nataka kumuunga mkono kwa kuongeza kidogo katika maisha ya Lucy Lameck ili kujaza nyama katika mifupa ya historia ya TANU na harakati za uhuru.

Lucy Lameck aliibuliwa na Yusuf Olotu lakini akijulikana kwa jina la kazi yake, Yusuf Ngozi kwa kuwa alikuwa mfanyabiashara wa ngozi.

Lucy Lameck akaja kufahamika na kushika nyadhifa kadhaa lakini Yusuf Olotu kafa hakuna amjuaye licha ya mchango wake mkubwa katika kuasisi TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.



Nilikwenda kumuona Mzee Yusuf Olotu nyumbani kwake Moshi nyakati za jioni baada ya L’ Asr.

Nilimkuta Mzee Olotu ndani amelala kwa kuwa hali yake ya afya haikuwa njema sana.

Baada ya ujitambulisha alichangamka kwani nilipomtajia wazazi wangu wote akawa anawafahamu ingawa ni miaka mingi hawajaonana.

Mtoto wa Mzee Olotu Ahmed ni makamo yangu na tulicheza pamoja utotoni kwa kuwa nyumba zetu zilikuwa jirani Moshi Mtaa Chini.

Mzee Olotu alifurahi kusikia naandika kitabu cha historia yao wapigania uhuru wa Tanganyika.

Akanieleza kuwa walipita watu kwake miaka michache iliyopita wakitokea CCM na wakachukua nyaraka zake zote na picha wakidai kuwa wanakusanya nyaraka hizo na picha kwa ajili ya kuandika historia ya TANU na pia kutoa kifuta jasho kwa wale waliokuwa mstari wa mbele kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kwa masikitiko alinieleza kuwa hakuna kilichofanyika na hata alipokwenda ofisi ya CCM kuomba angalau wamrudishie nyaraka na picha zake aliishia kuzungushwa.

Tukaanza mazungumzo huku kinasa sauti changu kikizunguka taratibu.

Mzee Olotu alikuwa anasumbuliwa na kikohozi lakini alianza kuzungumza kwa utaratibu baada ya kuwaambia vijana wake waliokuwa nje kuwa ana mgeni muhimu na hataki kusumbuliwa.

Hatukufika mbali katika mazungumzo mvua kubwa ikaanza kunyesha ikasindikizwa na radi…

Kwa miaka mingi badae kila nilipokuwa namsikiza Mzee Olotu katika kinasa sauti changu na nikisikia vile akinyamaza kuzungumza kwa ajili ya kikohozi kisha akireja kueleza historia ya uhuru sauti yake ikiingiliana na radi nilikuwa najiuliza – ile radi ilikuwa inaashiria nini?

Nilikuwa Arusha baada ya miaka kupita ndipo nilipopata taarifa kuwa Mzee Olotu amefariki na kazikwa jana yake.

Niliondoka siku ya pili yake kwenda Moshi kuhani.

Nasikitika kuwa Mzee Olotu hakukiona kitabu ambacho kimemtaja yeye na wenzake katika kuunda TANU Kilimanjaro, mwaka wa 1955 na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Uchagga ilikuwa chini ya utawala wa machifu waliokuwa wakijulikana kama Mangi.

Baadhi ya machifu hawa walikuwa katika Baraza la Kutunga Sheria na kwa ujumla wao walikuwa karibu na serikali ya kikoloni kuliko walivyokuwa na wananchi wanaowaongoza.

Hali ya siasa Jimbo la Kaskazini ilikuwa ngumu na ya kukatisha tamaa.

Wakati TANU inakabiliwa na Kura Tatu mgogoro wa ardhi ya Wameru ulikuwa umekwisha kwa wananchi kudhulumiwa haki yao.

Japhet Kirilo alikuwa amerudi kutoka Umoja wa Mataifa alikopeleka madai ya Wameru mikono mitupu.

Kirilo hakuwa na chochote cha kuwaonyesha Watanganyika.

Ilikuwa Yusuf Ngozi ndiye aliyeweza kuifanya TANU iingie kwanza Moshi mjini kwa vishindo na kutoka hapo mjini akaieneza vijijini.

Kupitia kumbukumbu za Mzee Yusuf Ngozi ndipo unapokutana na historia za awali kabisa za wanasiasa maarufu waliopata majina na vyeo; na wengine kuwa mawaziri katika Tanganyika huru, kama Lucy Lameck, Enesmo Eliufoo na wengineo.

Ilikuwa Yusuf Ngozi ndiye pamoja na wazalendo wengine waliifanya TANU ishinde uchaguzi wa Kura Tatu mwaka 1958.

Kupitia kumbukumbu zake halikadhalika ndipo kwa huzuni kubwa utakapokutana na mashujaa waliosahaulika kama yeye mwenyewe, mashujaa wa kike na wa kiume, wazalendo kama marehemu Mama Bint Maalim, Amina bint Kinabo, Halima bint Selengia, Juma Ngoma, Melkezedek Simon, Gabrieli Malaika na wengineo.

Hawa ndiyo mashujaa ambao kwa muda waliamua wasahau nguvu na utawala wa machifu wao na kujiweka chini ya TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.


Kwa kuhitimisha naweka hapa chini maneno aliyoandika Daisy Sykes katika kumbukumbu ya miaka 50 ya kifo cha baba yake akikumbuka yale aliyokuwa akiyaona nyumbani kwao ambako kila siku walikuwa wakija wazalendo viongozi wa TANU wapigania uhuru wa Tanganyika:

''...it was also during this formative period in my life that I met the up and coming women nationalist leaders such as Bi Lucy Lameck from Moshi, Mary Ibrahim and the mainly Moslem women, such as Bibi Titi, Bi. Tatu biti Mzee, Bi. Hawa biti Maftaha from Dar es Salaam who all passed as my grannies.

All of these women were carefully selected for their courage and became prominent at political rallies, singing and shouting out nationalist slogans, a trend that was totally unexpected and untypical for a Moslem woman, who were supposed to be subdued, modest and who remained behind the scenes.

I overheard numerous discussions when my Dad and his colleagues discussed the names and occasions for which these women were to be brought in to build the political momentum.

But what has really stayed within my memory was frequent arrival of the leadership echelons of the pre independence era, the tribal chiefs and the leaders of the budding nationalist movements, trade unions and other government staff.

Hence, courtesy to my father’s fame and hospitality, I grew up to be no stranger to the famous tribal chiefs and royalty as I greeted and attended to the dignitaries who came home regularly.

Such high profile frequent guests included Mangi Mkuu Thomas Mareale, Chiefs Abdiel Shangali, John Maruma from Moshi, Adam Sapi Mkwawa from Iringa, Kidaha Makwaiya from Usukuma, Abdallah Fundikira, Harun Lugusha from Tabora, , Humbi Ziota from Nzega, Michael Lukumbuzya from Ukerewe and Patrick Kunambi from Morogoro among others.

They were normally accompanied by their very dignified looking wives who never ceased to mesmerize me.

I remember among the chiefs, was the one and only woman Chief Mwami Ntare from Kasulu Kibondo.''

(Daisy Sykes Buruku, ''Abdul Sykes that I Knew.'')

Picha ya kwanza ni Lucy Lameck, Yusuf Olotu, Chief Marealle, Chief John Maruma na Chief Abdiel Shangali, Mwami Theresa Ntare, Chief Abdallah Said Fundikira, Chief David Kidaha Makwaia.

Ingia hapo chini kiuangalia picha:
 
Mkuu ungempa na Credit Japhet Kirilo kama shujaa.

Nafikiri kuwaunganisha Wameru wote kisha kuwachangisha ela mpaka zikajaa Kiroba kama nauli ya kwenda UN kudai uhuru wao katika mzingira ya permanent settlement Agriculture sio jambo ndogo ni ushujaa wakupigiwa makofi!

Nachokiona ni kwamba kulikua na aina nyingi za vuguvugu la kudai uhuru. TANU ilikua kama kiumganishi cha mavugu vugu tofauti nchi nzima. Na hii imetokea nchi nyigi za Kiafrica watu wanaungana kumtoa mtu mweupe maana akuna aliekua akifurahia uwepo wake.
 
Big up mkuu
Mkuu ungempa na Credit Japhet Kirilo kama shujaa.

Nafikiri kuwaunganisha Wameru wote kisha kuwachangisha ela mpaka zikajaa Kiroba kama nauli ya kwenda UN kudai uhuru wao katika mzingira ya permanent settlement Agriculture sio jambo ndogo ni ushujaa wakupigiwa makofi!

Nachokiona ni kwamba kulikua na aina nyingi za vuguvugu la kudai uhuru. TANU ilikua kama kiumganishi cha mavugu vugu tofauti nchi nzima. Na hii imetokea nchi nyigi za Kiafrica watu wanaungana kumtoa mtu mweupe maana akuna aliekua akifurahia uwepo wake.
 
  • Thanks
Reactions: Oxx
Oxx,
Japhet Kirilo
ni shujaa wetu wala hilo halina wasiwasi na nimeeleza
historia yake katika kitabu cha Abdul Sykes.

1083006

Kulia wa kwanza ni Japhet Kirilo 1955

Japhet Kirilo ndiyo Mtanganyika wa kwanza kuzungumza UNO 1952.

Wakati wa mgogoro wa Land Meru Case Abdul Sykes ndiye alikuwa
Secretary and Acting President wa TAA.

Nimekutana na Kirilo ndani ya Nyaraka za Sykes mapema sana kupitia
stakabadhi ya fedha alizopelekewa na Mweka Hazina Msaidizi wa TAA
Ally Sykes.

Mweka Hazina alikuwa John Rupia.

Fedha hizi alipelekewa Usa River ilikuwa ni Money Order lakini kwa kuwa
Usa River hapakuwa na Posta Kirilo hakuweza kuzitoa hizo fedha hapo.

Kirilo yeye akiishi Usa River.

Mwaka wa 1989 nilikwenda nyumbani kwa Japhet Kirilo kumhoji bahati
mbaya alikuwa amesafiri.

Fedha hizi alipelekewa kama masurufu ya safari afike Dar es Salaam ili
aungane na wanakamati wenzake - Saadan Abdul Kandoro na Abbas
Sykes
kwa safari ya kutembea kwenye majimbo.

Uongozi wa TAA uliunda kamati hii ya watu watatu kwa nia ya kuwaeleza
wananchi dhulma za ukoloni kuwa wanaweza wakachukua ardhi za watu
na isiwe chochote.

Lakini kulikuwa na agenda kuu nyuma ambayo Abdul Sykes na viongozi
wenzake walikuwa wameipanga nayo ilikuwa kuwatayarisha wananchi
majimboni kwa ujio wa TANU waliyokuwa wamekusudia kuunda.

Abdul Sykes alifanyakazi karibu sana na Kirilo chini ya Meru Citizens Union
iliyokuwa inashughulika na mgogoro ule na zipo barua ambazo Abdul alikuwa
akiandikiana na Sablak wa Meru Citizens Union.

Bahati mbaya huyu mzalendo katika nyaraka anatokea kwa jina moja tu hilo
la Sablak.

Abdul Sykes ndiye aliyezungumza na Earle Seaton ili aisaidie Meru Citizens
katika kutayarisha, ''petition,'' kwenda UNO, New York.

Earle Seaton alikuwa rafiki wa Abdul Sykes na ndiye aliisaidia TAA kuandika
mapendekezo ya mwaka wa 1950 yaliyopelekwa kwa Gavana Edward Twining
mapendekezo yaliyotayarishwa na TAA Political Subcommittee.

Waingereza walimnyima Kirilo passport ili asiweze kusafiri na ikabidi Abdul Sykes
aingilie kati na mwishowe serikali ilimpa Kirilo passport.

Kamati ya Kirilo, Saadan Abdu Kandoro na Abbas Sykes ilisafiri sehemu nyingi
za Tanganyika na kufanya mikutano ya hadhara na ikichangisha fedha pia kwa ajili
ya TAA.

Mafanikio makubwa ya kamati hii yalipatikana Kanda ya Ziwa ambako Paul Bomani
alihutubia mikutano pamoja na kamati.

Historia hii ya Japhet Kirilo ndilyo iliyomfanya awemo katika waasisi 17 walioasisi
TANU mwaka wa 1954.
 

yangu Fredy Nyaluchi kaweka hapa barzani picha ya Lucy Lameck na maelezo kidogo ya maisha yake katika siasa za Tanzania.

Nataka kumuunga mkono kwa kuongeza kidogo katika maisha ya Lucy Lameck ili kujaza nyama katika mifupa ya historia ya TANU na harakati za uhuru.

Lucy Lameck aliibuliwa na Yusuf Olotu lakini akijulikana kwa jina la kazi yake, Yusuf Ngozi kwa kuwa alikuwa mfanyabiashara wa ngozi.

Lucy Lameck akaja kufahamika na kushika nyadhifa kadhaa lakini Yusuf Olotu kafa hakuna amjuaye licha ya mchango wake mkubwa katika kuasisi TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.


Nilikwenda kumuona Mzee Yusuf Olotu nyumbani kwake Moshi nyakati za jioni baada ya L’ Asr.

Nilimkuta Mzee Olotu ndani amelala kwa kuwa hali yake ya afya haikuwa njema sana.

Baada ya ujitambulisha alichangamka kwani nilipomtajia wazazi wangu wote akawa anawafahamu ingawa ni miaka mingi hawajaonana.

Mtoto wa Mzee Olotu Ahmed ni makamo yangu na tulicheza pamoja utotoni kwa kuwa nyumba zetu zilikuwa jirani Moshi Mtaa Chini.

Mzee Olotu alifurahi kusikia naandika kitabu cha historia yao wapigania uhuru wa Tanganyika.

Akanieleza kuwa walipita watu kwake miaka michache iliyopita wakitokea CCM na wakachukua nyaraka zake zote na picha wakidai kuwa wanakusanya nyaraka hizo na picha kwa ajili ya kuandika historia ya TANU na pia kutoa kifuta jasho kwa wale waliokuwa mstari wa mbele kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kwa masikitiko alinieleza kuwa hakuna kilichofanyika na hata alipokwenda ofisi ya CCM kuomba angalau wamrudishie nyaraka na picha zake aliishia kuzungushwa.

Tukaanza mazungumzo huku kinasa sauti changu kikizunguka taratibu.

Mzee Olotu alikuwa anasumbuliwa na kikohozi lakini alianza kuzungumza kwa utaratibu baada ya kuwaambia vijana wake waliokuwa nje kuwa ana mgeni muhimu na hataki kusumbuliwa.

Hatukufika mbali katika mazungumzo mvua kubwa ikaanza kunyesha ikasindikizwa na radi…

Kwa miaka mingi badae kila nilipokuwa namsikiza Mzee Olotu katika kinasa sauti changu na nikisikia vile akinyamaza kuzungumza kwa ajili ya kikohozi kisha akireja kueleza historia ya uhuru sauti yake ikiingiliana na radi nilikuwa najiuliza – ile radi ilikuwa inaashiria nini?

Nilikuwa Arusha baada ya miaka kupita ndipo nilipopata taarifa kuwa Mzee Olotu amefariki na kazikwa jana yake.

Niliondoka siku ya pili yake kwenda Moshi kuhani.

Nasikitika kuwa Mzee Olotu hakukiona kitabu ambacho kimemtaja yeye na wenzake katika kuunda TANU Kilimanjaro, mwaka wa 1955 na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Uchagga ilikuwa chini ya utawala wa machifu waliokuwa wakijulikana kama Mangi.

Baadhi ya machifu hawa walikuwa katika Baraza la Kutunga Sheria na kwa ujumla wao walikuwa karibu na serikali ya kikoloni kuliko walivyokuwa na wananchi wanaowaongoza.

Hali ya siasa Jimbo la Kaskazini ilikuwa ngumu na ya kukatisha tamaa.

Wakati TANU inakabiliwa na Kura Tatu mgogoro wa ardhi ya Wameru ulikuwa umekwisha kwa wananchi kudhulumiwa haki yao.

Japhet Kirilo alikuwa amerudi kutoka Umoja wa Mataifa alikopeleka madai ya Wameru mikono mitupu.

Kirilo hakuwa na chochote cha kuwaonyesha Watanganyika.

Ilikuwa Yusuf Ngozi ndiye aliyeweza kuifanya TANU iingie kwanza Moshi mjini kwa vishindo na kutoka hapo mjini akaieneza vijijini.

Kupitia kumbukumbu za Mzee Yusuf ngozi ndipo unapokutana na historia za awali kabisa za wanasiasa maarufu waliopata majina na vyeo; na wengine kuwa mawaziri katika Tanganyika huru, kama Lucy Lameck, Enesmo Eliufoo na wengineo.

Ilikuwa Yusuf Ngozi ndiye pamoja na wazalendo wengine waliifanya TANU ishinde uchaguzi wa Kura Tatu mwaka 1958.

Kupitia kumbukumbu zake halikadhalika ndipo kwa huzuni kubwa utakapokutana na mashujaa waliosahaulika kama yeye mwenyewe, mashujaa wa kike na wa kiume, wazalendo kama marehemu Mama Bint Maalim, Amina bint Kinabo, Halima bint Selengia, Juma Ngoma, Melkezedek Simon, Gabrieli Malaika na wengineo.

Hawa ndiyo mashujaa ambao kwa muda waliamua wasahau nguvu na utawala wa machifu wao na kujiweka chini ya TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.
We mzee kariakoo umeishi mnanyumba na moshi pia ? Doh sasa kwa wachaga ulifwata nini enzi hizo na kila MTU maarufu nchi hii wamjua na umeongea nae mmmh
 
We mzee kariakoo umeishi mnanyumba na moshi pia ? Doh sasa kwa wachaga ulifwata nini enzi hizo na kila MTU maarufu nchi hii wamjua na umeongea nae mmmh
Alizungumza nao zaidi wakati akiandaa/andika kitabu chake. Pia Maalim kapata fursa ya kuishi na hao wazee wengi was enzi za TANU yeye akiwa kijana mdogo,
 
Alizungumza nao zaidi wakati akiandaa/andika kitabu chake. Pia Maalim kapata fursa ya kuishi na hao wazee wengi was enzi za TANU yeye akiwa kijana mdogo,
Nimeanza shule Lutheran Primary School, Moshi 1958 nikiwa na miaka 6. Mwalimu wangu wa kwanza alikuwa Mwalimu Paul na darasa lilikuwa ndani ya kanisa. Sababu ya kuhamishwa Dar es Salaam kuletwa Moshi ni kuwa mwaka wa 1956 mwezi June mama yangu alifariki dunia. Ikaonekana niondolewe Dar es Salaam nikaanze shule Moshi kwa mama yangu mdogo aliyekuwa akifanya kazi Moshi Nursing Home kwa daktari wa Kigiriki jina lake Dr. Georgiadis. Hospitali hii ilikuwa inatazamaba na Boma na hii nyumba hadi leo ipo. Dr.

Georgiadis alikuwa na mwanae umri kama wangu akiitwa Cregory. Huyu alikujakuwa rafiki yangu tukicheza pamoja na aki-share toys zake na mimi. Ni kisa kirefu cha kuvutia sana.
 
Nimeanza shule Lutheran Primary School, Moshi 1958 nikiwa na miaka 6. Mwalimu wangu wa kwanza alikuwa Mwalimu Paul na darasa lilikuwa ndani ya kanisa. Sababu ya kuhamishwa Dar es Salaam kuletwa Moshi ni kuwa mwaka wa 1956 mwezi June mama yangu alifariki dunia. Ikaonekana niondolewe Dar es Salaam nikaanze shule Moshi kwa mama yangu mdogo aliyekuwa akifanya kazi Moshi Nursing Home kwa daktari wa Kigiriki jina lake Dr. Georgiadis. Hospitali hii ilikuwa inatazamaba na Boma na hii nyumba hadi leo ipo. Dr. Georgiadis alikuwa na mwanae umri kama wangu akiitwa Cregory. Huyu alikujakuwa rafiki yangu tukicheza pamoja na aki-share toys zake na mimi. Ni kisa kirefu cha kuvutia sana.
Huyu Bwana alichokiandika ni kweli kabisa,huko Moshi tumecheza soote Mtaa chini na huyo kijana wa Mzee Yussuf Ngozi ndiye huyu Mzee Chilo msanii wa Bongo Movies
 
Hakika Dunia tunapita tu, hawa wote walishatangulia mbele ya haki imebaki historia
 
Hakika Dunia tunapita tu, hawa wote walishatangulia mbele ya haki imebaki historia
Mputa,
Naam wote hawa wamepita kama vile hawakuwapo imebakia historia.
Lucy Lameck ametajwa katika Wasifu wa Julius Nyerere lakini Yusuf Olotu hakuna amjuaye.
 
Mputa,
Naam wote hawa waempita kama vile hawakuwapo imebakia historia.
Lucy Lameck ametajwa katika Wasifu wa Julius Nyerere lakini Yusuf Olotu hakuna amjuaye.
Mkuu ni wengi sana historia imewafunika ingawa walifanya makubwa, mfano mwingine ni Ndugu Okelo, shujaa aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar lakini kamwe hatajwi popote
 
Mkuu ni wengi sana historia imewafunika ingawa walifanya makubwa, mfano mwingine ni Ndugu Okelo, shujaa aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar lakini kamwe hatajwi popote
Mputa,
Suala la John Okello si kama wewe unavyodhania lilivyo.
Mchango wa Okello katika mapinduzi ya Zanzibar si mkubwa kiasi hicho.

Karume asingeweza kupindua serikali ya Zanzibar achilia mbali John Okello.
Wala usiamini kuwa ASP na Umma Party walipanfa mapinduzi yale.

Ukitaka kuijua historia ya Zanzibar inakubidi usome kitabu cha Harith Ghassany, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' (2010).

Utakayojifunza humo yatakushangaza.
Kitabu nakuwekea hapo chini:

Free Downloading ya Kitabu
 
Back
Top Bottom