Mashuleni na Vyuoni ni Kuchafu

Mashuleni na Vyuoni ni Kuchafu

Wordsworth

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2019
Posts
1,191
Reaction score
3,360
Hivi chuoni kunakuwaje na kunguni? Wanashindwaje kupiga dawa kila baada ya muda fulani? Kuna chuo cha afya hapa Nala Dodoma wanafunzi wanataka kuhama kwasababu kunguni wamezidi. Wakaguzi, wenye mamlaka, mpo wapi? Mnaacha hizi taasisi zijiendeshe na kufuga uchafu? Au mmeshiba rushwa mpaka mnashindwa kutembea?

Kwenye vyoo sasa ndio utakimbia. Kuna vyuo kadhaa vikubwa hapa nchini ukijichanganya ukaenda chooni kule kwa wanafunzi unaweza usile chakula wiki nzima. Ukiuliza sababu unaambiwa eti hamna maji. Maji yanatoka tu vyoo vya chini ukipanda ghorofa moja maji hayatoki. Hivi hadi huu mwaka wa 2022 mnashindwa kupandisha maji ghorofani na mnasomesha watu wa sayansi na uhandisi? Hii ni AIBU.

Ni muhimu sana hizi taasisi zenye kukutanisha watu wengi zisimamie usafi wa hali ya juu. Kwanzia kwenye chakula, chooni, darasani na maeneo yote. Serikali iache uvivu na blah blah, ifanye kazi yake ya kusimamia hizi taasisi.
 
Tatizo lipo kwa watumiaji wa vyoo
Hawajali kabisa tena utakuta mtu mzima lakini duh😂😂😂

Mamlaka zilizowekwa nazo hazitimizi wajibu wake.

Kiujmla. Watanzania hatuna tabia ya kujali na kufata utaratibu iwe nyumbani, makazini au sehemu yoyote ile.
 
Duh nchi hii tuna safari ndefu sana. Imagine watu hata basic hygiene hawawezi ku-control mambo makubwa itakuwaje?
 
Kunguni tena wajameni, mbona kisanga hichi wananzengo ngoja wausika waje
 
Vyuo vingi,kunguni ni wengi.Inaonyesha vyuo vyetu ni teaching based na siyo reseach based,tatizo la kunguni na maji,insshindikana kutatua kweli?Ukiangalia hapo Dodoma,water table iko juujuu sana,ila eti kuna shida ya maji,daah!
 
Yule mhadhiri wa UDSM alisema wanafunzi hawajui kuoga sembuse kwenda kukata gogoz itakuaje🤧🤧
 
Tatizo lipo kwa watumiaji wa vyoo
Hawajali kabisa tena utakuta mtu mzima lakini duh😂😂😂

Mamlaka zilizowekwa nazo hazitimizi wajibu wake.

Kiujmla. Watanzania hatuna tabia ya kujali na kufata utaratibu iwe nyumbani, makazini au sehemu yoyote ile.
Hapo kwenye usafi wa mtu binafsi ndio balaa lingine lilipo. Hawa wanafunzi hasa wa chuo ni wachafu mnooo sio wastaarabu hata kidogo, bora wa mashuleni wanakaguliwa usafi mara kwa mara.
 
SIKU HIZI MAFUNDI BOMBA NA WATAALAMU WA FUMIGATION WAPO WENGI ILA NDIO HIVYO PENYE MITI HAKUNA WAJENZI
Eti jamani. Huu mwaka wa 2022 tangu ujio wa Yesu Kristo bado watu wanashindwa kufanya plumbing ya uhakika? Chuo kama UDSM wana vitivo vya uhandisi lakini eti kwenye mabweni yao maji hayapandi ghorofani.
 
Duh nchi hii tuna safari ndefu sana. Imagine watu hata basic hygiene hawawezi ku-control mambo makubwa itakuwaje?
Huku kwenye basic hygiene tulitakiwa tuwe tumepita siku nyingi sana. Inasikitisha.
 
Vyuo vingi,kunguni ni wengi.Inaonyesha vyuo vyetu ni teaching based na siyo reseach based,tatizo la kunguni na maji,insshindikana kutatua kweli?Ukiangalia hapo Dodoma,water table iko juujuu sana,ila eti kuna shida ya maji,daah!
Hivi vyuo vyetu ni useless. Eti unawajuzi wakutosha wa mambo kadhaa lakini bado hamuwezi kuapply huo ujuzi kutatua matatizo madogo madogo mwenye jamii. Mtu unajigamba umesoma sana lakini chuo chako kinatatizo la maji na kunguni. Seriously? Utakuwa mzima wewe?
 
Watu wengi ustaarabu ziro kama kitu sio chake hakipi matunzo bora. Hivyo vyoo ukute hata koki walishang'oa ,kunguni wapo wanaotoka nao majumbani kwao
 
Yule mhadhiri wa UDSM alisema wanafunzi hawajui kuoga sembuse kwenda kukata gogoz itakuaje🤧🤧
Alisema ukweli. Hawa wanafunzi personal hygiene yao ni sifuri hata kuoga vizuri hawajui wanaishia kupaka cheap perfumes.
 
Nakumbuka UDSM vyooni ni shida unakutana na mizigo imerundikwa na inabidi uingie hivyo hivyo, tatizo sio la wanafunzi tatizo ni management, maji ni ya shida sana especially toilets za karibu na seminar rooms kwa udsm alumin mnavijua. Sasa mtu umebanwa haja unaenda toilet hamna maji utafanyaje? inabidi ujisaidie hivyo hivyo. Wa kulaumiwa ni management.
Wenye shida zaidi kweli ni viongozi wa chuo. Maji yakikosekana usafi ni wa shida sana. Lakini hawa wanafunzi nawajua wengi sio wastaarabu.
 
Back
Top Bottom