Masijala za Halmashauri kwanini hakuna Huduma kwa Wateja na Ukosefu wa Dawati Maalum? Pia hakuna 'provacy'

Masijala za Halmashauri kwanini hakuna Huduma kwa Wateja na Ukosefu wa Dawati Maalum? Pia hakuna 'provacy'

Mr DIY

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2016
Posts
1,188
Reaction score
2,553
Hili sijui naliona mimi pekee ni shida, kwanini ofisi nyingi za Masijala za halmashauri hazina dawati maalum ndani ya ofisi kwa ajili ya kuhudumia wateja wao ambao wengi wao huwa ni watumishi ila wao hupenda au hulazimisha huduma kufanyika dirishani, tena wenyewe wakiwa wamejifungia kwenye ac?
images (5).jpeg

Imagine unasimama hapa nje tena koridoni unatoa shida zako za kiofisi dirishani kwenye hizo nondo ukitoka kioo kinafungwa, hivi huu utaratibu alianzisha nani.

========================

Pia, hakuna usiri, unapokuwa na shida yako ya privacy, unapanga foleni hapo kama mpo wengi unaeleza shida yako hapohapo kwenye dirisha kila mtu anasikia, kama unawasilisha barua au nyaraka ya siri na unatakiwa kutoa maelezo, kila mtu anasikia unachokisema hapo.

Pia wengi wao wanaohusika na idara hii huku mtaani wanaitwa "Wakata umeme", wakiamua kupotezea nyaraka yako wanafanya hivyo, unajua suala lako linashughulikiwa kumbe wao wamepippiga chini na kuendelea na mambo yao.

Pia soma ~ Watumishi wa MASJALA katika halmashauri kadhaa nchini walalamikiwa kuwa na roho za uuwaji kiutumishi
 
Zile ofisi ndo zimebaba siri da mafile yote ya watumishi sasa ukalibishwe ndani ukanyofoe viambata kwenye mafile ya watumishi.
 
Masjara ya halmashauri gani hiyo yenye ulinzi kama kwa sonara?

mkuu, kila idara ina personal secretary kwa nini usianzie idara husika
 
Zile ofisi ndo zimebaba siri da mafile yote ya watumishi sasa ukalibishwe ndani ukanyofoe viambata kwenye mafile ya watumishi.

Unyofoe nyaraka au uibe faili zima ni upuuzi, halmashauri au watumishi wao wana usiri gani hadi uwe na thamani kiasi hicho

hata ikitokea missing PV, bado hakuna hoja ya kutisha
 
Sio tu wateja hata staff ambao sio wa masijala hawana ruhusa ya kuingia humo bali kwa ruhusa maalumu tu.
 
Back
Top Bottom