Masikio yananiwasha japo nayasafisha kila mara

juvenile davis

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2015
Posts
4,752
Reaction score
4,467
Kama heading inavojieleza hapo juu[emoji115].masikio tangu huwa yananiwasha mara kwa mara,nikifikicha na pamba au kidole huwa kunatoka vitu kama nta iliyogandia na kukauka.sasa sijajua tatizo ni nini?? Kuhusu suala la usafi kiukweli najitahidi sana.nasafisha kila mara na maji ,ila uchafu hauishi na ni kama ni bakteria fulani hivi maana nikifikicha huwa kunatoka harufu mbaya sana na huwa hizo nta au pumbapumba haziishi,,nifanyeje??
 
Tumia kitunguu saumu ponda/saga kisha paka kidogo
 
Naona ukiziwi ukikunyemelea ukifanya baadhi ya ushauri wa humo ndani. Kama upo mjini nenda kwenye klinik maalum za ENT wakusikilize.
 
ENT inakuhusu...

Nenda hospitali...labda una fungus au ugonjwa
 
Kuna njia ya kusafisha masikio hospital nenda kaonane na specialist wa maskio
 
Nenda hospitali. Halafu usiingize maji maskioni. Utakuwa na infection.
 
Duh! By experience, naonaga nikisafisha na pamba ndo yanazidi kuwasha nikiacha kudafisha nakuwa poa kbs, acha kusafisha hats week 2 uone itakuwaje
 
Sometimes ule unaosema ww ni uchafu uwa ndio kilainishi cha ngoma ya sikio, sasa unapoisafisha kila mara unaitoa hiyo na kuacha sikio likiwa dry then matatizo yanaongezeka badala ya kupungua.
Acha kusafisha sikio kabisa, kama uchafu toa ulio juu juu na sio ndani, nenda pharmacy ulizia dawa za kulainisha sikio au kule vijijini wanatumiaga mafuta ya kuku/simba na uwa inasaidia, kama unauwezo wa kupata hydrogen peroxide changanya tone moja kwa tone kama 2 za maji then nyunyiza ndani ya sikio kwa siku kadhaa inasaidia pia, hii ya mwisho nilifundishwa na dr wa watoto wangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…