kaka nguvuri3 kwanza nashukuru kwa kunifariji pili kwa ushauri wako juu ya kuonana na mabingwa .mkuu pia umesema Ningependa kufahamu sababu zilizopelekea masiko yako kutoboka. Je umewahi kuwaona wataalam wakathibitisha kuwa ngoma zimetoboka? [ Eardrum perforation].Pili unapotumia mashine unazosema, je hali inakuwaje katika usikivu. mkuu mimi ninahisi sababu zinaweza kuwa mbili kuu 1 nimewahi kufanya kazi kwenye mazingira ya kelele kama driller sehemu ambayo ilikuwa inalipua miamba kwa baruti 2niliwahi kuugua TB ambapo madaktari hawakuishitukia mapema wakawa wananitibu maralia kwakuwa sasa sikuwa napata nafuu waliamua kunichoma quinini ambazo ndo ziliniziba masikio hivyo nikawa sisikii tena. kuhusu mabingwa wa masikio nimeonana nao zaidi ya watano .bugando mmoja,muhimbili mmoja,ekenwa dispnsr mmoja,murugwanza mmoja,kahama hospital mmoja (huyu alikuja toka kenya) kifupi wote walikuwa wananipa moyo sana na nilijitahidi mno kuhudhulia kiliniki. vipimo vyao vilionyesha kwamba ngoma zimetoboka na sikio la kushoto linasikia kwa 20% huku jingine linasikia kwa 10%ningekuwa mtoto mdogo wangenipasua kisha wazibe ila kwa kuwa mimi ni mtu mzima haita saidia.wakanipa mfano mtu mzima akivunjika mguu kuunga huwa ni kazi ngumu sana. kuhusu hii mashine ninayoitumia nashukuru inanisaidia ila wakati mwingine huwa inazimika tu nakaa hata siku tatu siendi kazini kwakuwa sisikii na kazi zangu ni za ufundi hivyo wateja wangu ili wakupe kazi mpaka msikilizane mkubaliane. mashine yenyewe inauzwa bei ghari sana hivyo kumudu kununua mashine ingine kama spea ni kazi. kumbuka ni miaka mitatu tu iliyo pita tangu nipate tatizo hili. nashukuru kwa kunisoma.